Saharavoice
JF-Expert Member
- Aug 30, 2007
- 3,882
- 2,374
Baada ya sakata la misamaha ya kodi kwa mashirika ya dini kumalizika kwa serikali kusalimu amri, nimebaki na maswali mengi bila majibu. ukifikiri kwa undani sana utagundua kwamba ni kweli misamaha hii iko abused kwa kiwango cha hali ya juu sana na hapo ndipo tunaona jinsi tunavyopoteza mamilioni ya kodi.
Wajanja wengi walianzisha na wanaendelea kuanzisha mashirika ya dini kwa ajili ya kufaidi misamaha kama hii na kwa kweli si kwa ajili ya kuwasaidia wananchi bali ni kwa sababu ya kufanya biashara.
Lakini nimejiuliza maswali mengine pia kwamba: Iwapo mashirika haya yanapata misamaha ya kodi mbona karo za shule za seminari ziko juu sana ukilinganisha na private schools zingine zisizopata misamaha ya aina hii? Mbona baadhi ya hospitali za mashirika ya dini zinatoza viwango vikubwa vya matibabu kuliko private hospitals zingine????. Hivi waliosoma Seminari zamani walilipa karo za kiwango kikubwa kama cha sasa?
Wakati naendelea kufikiri hivi, najiuliza tena je huko makanisani na misikitini kuna Ufisadi unaendelea? Au Dini zetu zimegeuka za kibiashara badala ya huduma?? wakati naendelea kujiuliza, mimi huyo kiguu na njia nakutana na mheshimiwa Mbunge rafiki yangu, namuuliza maswali yangu kuhusu hili, anakubaliana na mawazo yangu lakini ananiambia mzee ukitaka usipate ubunge tena basi unga mkono serikali katika hili. "mimi hili sichangii" anasisitiza.
Mwishowe nabaki nimeduwaa, political impact!!!!!!!
Wajanja wengi walianzisha na wanaendelea kuanzisha mashirika ya dini kwa ajili ya kufaidi misamaha kama hii na kwa kweli si kwa ajili ya kuwasaidia wananchi bali ni kwa sababu ya kufanya biashara.
Lakini nimejiuliza maswali mengine pia kwamba: Iwapo mashirika haya yanapata misamaha ya kodi mbona karo za shule za seminari ziko juu sana ukilinganisha na private schools zingine zisizopata misamaha ya aina hii? Mbona baadhi ya hospitali za mashirika ya dini zinatoza viwango vikubwa vya matibabu kuliko private hospitals zingine????. Hivi waliosoma Seminari zamani walilipa karo za kiwango kikubwa kama cha sasa?
Wakati naendelea kufikiri hivi, najiuliza tena je huko makanisani na misikitini kuna Ufisadi unaendelea? Au Dini zetu zimegeuka za kibiashara badala ya huduma?? wakati naendelea kujiuliza, mimi huyo kiguu na njia nakutana na mheshimiwa Mbunge rafiki yangu, namuuliza maswali yangu kuhusu hili, anakubaliana na mawazo yangu lakini ananiambia mzee ukitaka usipate ubunge tena basi unga mkono serikali katika hili. "mimi hili sichangii" anasisitiza.
Mwishowe nabaki nimeduwaa, political impact!!!!!!!