Nitashangaa sana Emmanuel Masonga ukisaliti Chadema

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
137,721
Reaction score
272,662
Nakufahamu kwa namna ulivyopigania Chadema kwa muda mrefu tena kwa gharama ya damu

Ulifungwa jela kwa kesi ya uongo Ukiwa Pamoja na. Sugu, najua unanifahamu vizuri n.a. unafahamu ushirikiano wetu ulipokuwa Katibu wa Kanda ya Nyasa, naujua uwezo wako na heshima ambayo watu wa Njombe wamekupa

Nitashangaa sana Ukisaliti siasa za Ukombozi.
 
Ondoa Makelele yako hapa wewe. Kama unataka nenda nyumbani kwake ukampikie ndio umwelezage na Umbeya wako.
 
Reactions: Tui
Hii biashara haramu imeanza tena halafu naona kama inashika kasi
 
Mkuu Wacha wanaotaka kuondoka waondoke, maana wakibaki itakuwa tatizo. Kama Slaa, Msigwa, Halima Mdee nk walizingua, itakuwa huyo. Kwa sasa iko kwa wananchi sio kwa viongozi wasaka maslahi binafsi.
 
Naye kaunga mkono juhudi? Ila nadhani tuwaache tu waende uzuri wale chadema maslahi wanajichuja ili wabaki pure ambao wapo serious na mageuzi kuliko hawa waliopo chadema kusubiri bahasha za maridhiano, ubunge, na udiwani pekee.
Safi sana, sioni haja yoyote wa kuwabembeleza hao Wahuni.
 
Acha kulia lia. Kila mtu ana haki ya kufikiri anavyotaka😁
 
Reactions: Tui
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…