Swali la muhimu la kujiuliza, Je, dakika 5 zilimtosha rais kuielewa report hii kwa kina na kuitolea maamuzi au alipewa kabla akaisoma leo tar 24.5.2017 ni makabidhiano tu?.
Nitakuwa wa mwisho kumpongeza rais au nisimpongeze kabisa kwa sababu zifuatazo:
1. Nilikuwa wa kwanza kumpongeza polepole kwenye ishu ya katiba mpya hususani alipokuwa akisema nafasi za ukuu wa wilaya, mkoa hazina tija na athari za rais kupewa majukumu/maamuzi makubwa! leo hii najisikia aibu machoni pa watu waliokuwa wananisikia nikitoa big up kwake.
2. Huyu prof Muhongo ambaye leo rais anamwona mbaya bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania lilishamwona hafai toka muda mrefu ndiyo maana liliazimia kwa pamoja achukuliwe hatua. Hivyo rais kutengua uteuzi wake ni kukiri kosa alilolifanya kwenye uteuzi wake. Kwa hili sina sababu ya msingi ya kusema big up.
3. Nitakapoona mali za mafisadi na wahujumu uchumi na watu wao wa karibu wote zinafilisiwa baada ya kubainika na kosa.
4. Kumtumbua prof Muhongo ni sawa na kufukua makaburi, hivyo marais waliopita/wastaafu kama walihusika katika sakata hili wakachukuliwa hatua kama watuhumiwa wengine. Wengi wanasema katiba hairuhusu! Tujiulize mbona tunavunja katiba kwa mambo ambayo wakati mwingine hayana tija kwanini tusivunje katiba kwa suala la msingi kama hili? Uhusika mmoja wapo wa marais wastaafu ni usiri wa mikataba kama mamikataba yangekuwa wazi mambo mengi yangekuwa wazi.
Mwisho yatupasa kutambua mbele ya Mungu hakuna dhambi kubwa wala ndogo japo tunajifunza dhambi ya kumkashifu roho mtakatifu ndiyo dhambi isiyosameheka. Kwa Mungu hakuna mkubwa wala mdogo kwa maana ya umri, nafasi au kipato!
Nitakuwa wa mwisho kumpongeza rais au nisimpongeze kabisa kwa sababu zifuatazo:
1. Nilikuwa wa kwanza kumpongeza polepole kwenye ishu ya katiba mpya hususani alipokuwa akisema nafasi za ukuu wa wilaya, mkoa hazina tija na athari za rais kupewa majukumu/maamuzi makubwa! leo hii najisikia aibu machoni pa watu waliokuwa wananisikia nikitoa big up kwake.
2. Huyu prof Muhongo ambaye leo rais anamwona mbaya bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania lilishamwona hafai toka muda mrefu ndiyo maana liliazimia kwa pamoja achukuliwe hatua. Hivyo rais kutengua uteuzi wake ni kukiri kosa alilolifanya kwenye uteuzi wake. Kwa hili sina sababu ya msingi ya kusema big up.
3. Nitakapoona mali za mafisadi na wahujumu uchumi na watu wao wa karibu wote zinafilisiwa baada ya kubainika na kosa.
4. Kumtumbua prof Muhongo ni sawa na kufukua makaburi, hivyo marais waliopita/wastaafu kama walihusika katika sakata hili wakachukuliwa hatua kama watuhumiwa wengine. Wengi wanasema katiba hairuhusu! Tujiulize mbona tunavunja katiba kwa mambo ambayo wakati mwingine hayana tija kwanini tusivunje katiba kwa suala la msingi kama hili? Uhusika mmoja wapo wa marais wastaafu ni usiri wa mikataba kama mamikataba yangekuwa wazi mambo mengi yangekuwa wazi.
Mwisho yatupasa kutambua mbele ya Mungu hakuna dhambi kubwa wala ndogo japo tunajifunza dhambi ya kumkashifu roho mtakatifu ndiyo dhambi isiyosameheka. Kwa Mungu hakuna mkubwa wala mdogo kwa maana ya umri, nafasi au kipato!