Nitajie wachezaji watatu waliokuhamasisha kuupenda mchezo wa soccer

Na mimi nikajifunza kupiga kama yeye, siku moja kwenye michezo shuleni sekondari wakati wa mazoezi mwalimu akatenga mpira akaniambia nipige, alishika kichwa hakuamini!
Aliniambia “Nifah, hata wavulana kwenye kikosi chetu hawapigi hivi. Kwanini hukuwa mwanaume?, hiki ni kipaji” Heheee
Ingekuwa zama hizi nafikiri ungejiunga Yanga princess
 
1. Roberto Carlos
2. Roberto Carlos
3. Roberto Carlos

Napenda sana Mashuti hata nikiwa kwenye 6×6 napenda sana kupiga Mashuti
 
1. roberto baggio akiichezea juventus

2. youri djorkaeff akiichezea internazionale milano

3. ian wright akiichezea arsenal
 
Na mimi nikajifunza kupiga kama yeye, siku moja kwenye michezo shuleni sekondari wakati wa mazoezi mwalimu akatenga mpira akaniambia nipige, alishika kichwa hakuamini!
Aliniambia “Nifah, hata wavulana kwenye kikosi chetu hawapigi hivi. Kwanini hukuwa mwanaume?, hiki ni kipaji” Heheee
Hahaaa kumbe na wewe ushawahi kuwa Ball bender, sasa si ungeingia kwenye mpira tu pengine saa hii ungekuwa Ulaya, na jina lako lingekuwa linaimbwa kama kina Asisat Oshoala huko
 
Ronaldo de lima na zidane.. ronaldinho is my favourite player of all time ila alikuja badae kipindi ambacho nishakua mlevi wa soka.
 
1. Hamisi Kinye
2. Ahmed Amasha
3. Athumani Juma Chama

Mijinga itakuja kuuliza na kushangaa.
 
Inatosha kusema wengi waliochangia huu uzi ni 33+

Miaka inaenda wakuu

Timu ya taifa ya Brazil ilinifanya nilipende sana soka, hasa fainali ya World Cup ya 1994 walikichafua sana, Brazil vs Italy

Sikuitazama hii mechi nilikuwa bado chalii ila mzee alikuwa na VHS tape ya hiyo fainali nilipokuwa nikiitazama mara kwa mara nikaanza kujiita Rivaldo nilipokuwa nacheza mpira na wenzangu

Ronaldinho akafanya niipende Barça
 
Mwingine aliyenifanya nipende mpira miaka ile ya mwanzoni 80...alikuwa ni mtambo wa magoli pale spain akifahamika kama Hugo sanchez marquez...vijana wa sasa hamwezi kumjua huyu...jamaa alisajiliwa kwa mkopo pale atletico madrid kisha baada ya kukiwasha wakamchukua huyu jamaa mazima ..alikuwa ni hatari sana ktk kuzifumania nyavu mpk Real madrid ikamsajili na akakiwasha vilevile....jamaa alikuwa ni fundi wa kukaa kwenye nafasi na alikuwa na magical touch aisee tulioangalia la liga miaka ya 80 tulifaidi sana kuona vipaji vya mpira ambavyo havitakaa vijirudie.
Legendary na miaka yako 60
 
1. Said Maulid SMG alinifanya nikaipenda Yanga 2000
2. Thiery Henry, nikawa shabiki wa Arsenal 2004
3. Kama sio Henry, huenda ningekuwa shabiki wa Man U sababu ya Beckham, ila akanipeleka Madrid.
Beckham ndio sababu mpaka leo napenda mipira ya free kick.
Lete ubuyu wao basi.😀😃😄😁😆 mi ni Edibily Lunyamila miaka ya 1993 na mpaka wakawa wananiita Lunyamila wa huku kwetu nyakatuntu keisho Karagwe. Tulikuwa tukisikiliza Mpira kwenye RTD kipindi hiko.

Baadaye niliipenda Yanga baada ya Edo kuja YANGA na pale yanga ilipokuwa na akina Costantine kimanda, Nonda Shabani "Papii" Anwar Awadh n.k Hapo ndipo niliipenda Yanga rasmi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom