Nisaidie maelezo rahisi ya Square meter( m²)

Farolito

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2018
Posts
15,126
Reaction score
35,498
Habari wakuu,

Kama eneo lina square meter 100 (100 m²) tafsiri yake rahisi ni ipi?
Je maana yake kila upande uko sawa kwa mita 100 kwa maana ya urefu na upana?

Au eneo linakua kubwa au dogo zaidi ya mita 100? Kwa kila upande?

Naomba kufahamishwa.

Ahsante.
 
10m*10m
 
10m x 10m = 100m²
Au
20m x 5m = 100m² n.k
Pia kumbuka kanuni za hisabati kuwa
10m x 10m=100m²
(10x10)x(m x m)=100m²
m x m=m²
Then,
(100) x (m²)=100m²

Therefore
100m²=100m²
Hence shown

Maana yake eneo Lina miraba 100 yenye ukubwa wa 1m x 1m
 
Square(mraba) uwe na urefu na upana wa mita moja
Inamaana sasa kama eneo ni la 100m²,maana yake lina miraba 100 yenye urefu na upana wa mita moja kila mmoja.

Au cheki mchoro huu hapa ila vyumba vyote marefu na mapana yanatakiwa yawe sawa yaani urefu mita moja na upana mita moja, Ukihesabu vyote utakuta vyumba 100. Sasa hamishia mawazo ya kwenye uwanja pia rejea comment namba 5 utaelewa zaidi sasa halafau leta mrejesho kama imeingia kumkichwa
 
Asante mkuu nimepata vizuri kwa maelezo yako nikijazia na #5
Kiuhalisia kumbe hili ni eneo dogo tu kama ni ardhi(kwa maana ya 10m*10m)Square meter kumi kila upande.
 
... haihitaji pande zote kuwa sawa! Inaweza kuwa square-shaped, rectangular, triangular, circular, or any polygon or shape as long as the combined areas sum to that size. Tanzania ina ukubwa wa sijui 945,000 sq. km. Does it mean the country is square-shaped?
 
Umenifanya nicheke. Safi sana hence inaaply 50 metres mara 2metres, 25meters mara 4 metres etc. Naamini umeelewa sasa!
 
Wrong! Not always the case. Unamkaririsha mwenzio kwamba 100sq.m sharti urefu na upana wa eneo viwe sawa - wrong!
 
OK i stand tovbe corrected nimemwambia asome pia comment no 5 tupe uelewa wako wa square
Wrong! Not always the case. Unamkaririsha mwenzio kwamba 100sq.m sharti urefu na upana wa eneo viwe sawa - wrong!
 
OK i stand tovbe corrected nimemwambia asome pia comment no 5 tupe uelewa wako wa square
... soma comment no. 11; nimeandika hivi:-

... haihitaji pande zote kuwa sawa! Inaweza kuwa square-shaped, rectangular, triangular, circular, or any polygon or shape as long as the combined areas sum to that size. Tanzania ina ukubwa wa sijui 945,000 sq. km. Does it mean the country is square-shaped?
 
Hapo hap o kuna square tu no rectangular imetajwa
 
Wenye F za hesabu darasa la saba tunasoma comments tu,japo hata nyie wenye A bado hamuelewani
 
Natumaini vilaza wenzanu wa hesabu tupo makini kusoma maelezo na bado hatuelewi.... Tuendelee kutumbua macho mazee tusubiri maelezo rahisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…