''Nipo kwenye dilemma ..ushauri please''

Kukaribia 30 Ndo kuchelewa kuanzisha familia? Mi nadhani hujaelewa maana ya familia kuna msemo wa kiswahili kosea kujenga nyumba usikosee kuoa. Unadhani walimaanisha nn?
1. Usioe/usiolewe na mtu ambae moyo wako haujaridhia
2. Usikimbilie kwenye ndoa kisa umri umefika.
3. Usioe/usiolewe kisa umevutiwa na umbo shepu n.k
Umri sahihi wa kuoa ni upi labda? Tuanzie Hapo ila don't settle for less than what you deserve

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeongea ukweli kabisa two years afu huna hisia nae labda ana matatzo huyu jamaa

Sent using Jamii Forums mobile app
...labda tatizo ni kwamba tulianza kama marafiki wa kawaida kama miez miwili au mitatu hv so kuna yale mazoea yalijengeka mwanzo ...pamoja baadae tulikuwa wapenz lakin bado yale mazoea ya kirafiki yapo na ndio imechangia kudumu muda wote huo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanaume nyie, muwe na huruma, yani unadate na mtu for 2 yrs Kwa kujilazimisha duuh, kwann usimwambie ukweli mwanzoni kabla hamjafika mbali ili afahamu kabisa hamna future hapo. Huenda binti Wa watu anakutegemea mtafika mbali(ndoa) kumbe wewe unajilazimisha aisee

Anyways ndoa ni kifungo cha maisha, hivo usiingie Kwa kubip bip, hakikisha kweli mmependana na huyo mfungwa mwenzio. Kama unaona kabisa hutoweza kuendana naye huyo binti mwambie ukweli ataumia lkn atamove on, lkn ukikaa kimya mda utazidi kwenda mtafika miaka 3.. bila malengo yoyote tena.

Pia umri sahihi wa kuingia kwenye ndoa ni ule ambao unajiona uko tayari na umepata mwenzi sahihi. So unaweza ingia ukiwa na 30s, or 20s nk. Ila Make sure umepata mtu sahihi.




Sent using Jamii Forums mobile app
 

acha kupanic brother mbona 30 bado kabisa u still have a window ya miaka mitatu mingine so usipate tabu. wewembwage tuu maana kumbuka mke ni for the remainder of ur life, so chukua kitu ambacho yaani ukimuona tuu mnara unasoma. achana na story za kijiweni kuwa wazuri sio wakuoa...itakula kwako kaka. wewe kaoe mwanamke mzuri ambaye full time mzuka upo ufurahie life.
 
Tafuta yule utakaekuwa na hisia nae ila namna ya kuvunja hyo ni ubunifu wako anza kupunguza mawasiliano mdogo mdogo.It hurts though na sio fair.i once was in a situation kama yako ila nilitafuta excuse toka kwake nikabwaga chini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mke/Mume ni zaidi ya hisia...fikiria umepofuka macho kwa ajali na huwezi kujisaidia mwenyewe unafikiri ni hisia au upendo wa kweli ndio utakaokusaidia?
 
Haya sasa...
Kumuoa dada watatu hutaki, kumuacha nayo hutaki.

Miaka miwili ni mingi sana kukaa na mtu ambae unadai 'HUMFEEL' (sijui wenzangu mnawezaje😳😳) wakati the whole time yeye ulimuaminisha kinyume na hapo. Sasa umefika muda wa wewe kutaka kutimiza malengo yako binafsi (kuoa/familia) wala hutaki kujua yake ni yapi.

Just...stop being selfish and make a decision like a real man!!!
 
Hatua muhimu utafutapo mwenza. - JamiiForums
 
Karibu kwetu Tarime mkuu
 
Nimekupa likes 100
 
Kuliko uje umtese badae kwenye ndoa ni bora umuite uzungumze nae vizuri kwa upole mpka akulewe ikiwa bado haujachelewa hapo hata Mungu atakuelewa.
Heri nusu shari kuliko shari kamili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niko kwenye situation kama yako umri wangu mm pia ni kama wako. Mwanamke niliyenaye mm naweza sema ana kila sifa ya mke mwema, tatizo likawa kama lako No feelings at all,,ilinisumbua sana akili nikajipa mda wa kufikiria wakat huo namtafutia sababu za kumwacha lkn wapp sikupata sababu yy ndo kwanza akazid kua mpole kwang,,nikafikir tena wakat huo miez inaenda nikaomba ushaur kwa wazoefu wa ndoa jibu walilonipa MKATAA PEMA PABAYA PANAMWITA mhh nikaona nalo neno wakat huo kuna videm vingine Nina mahusiano navyo,,, nikapima hali ya maisha ya sasa ilivyo nikaona bora kutumia akili kuliko kupelekeshwa na hisia,,, muda ukasonga akapata mimba tukapata mtto was kiume,,, kwasababu ss wote ni watumish serikalin maisha yanasonga tunamlea mwenetu bila matatizo,,,USHAUR,,kwa ww ni dhahir kabisa Huyo dada atakua anakupenda kwa dhat tatitzo atakua hajakidhi vigezo vya maumbile unavyovitaka ndio maana unadai huna hisia nae,,acha kuangalia maumbile zile ni nyama tu ,,,,uzur ni ubatili Bali mwanamke atakaemcha bwana ndie atakaesifiwa,, Ukimwacha utalipa machoz atakayolia utatanga na hii dunia mpaka uchoke mpenz yatakua kama mwiba kwako ,,,, NIMEMALIZA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…