Huwa nacheka sana nnaposikia mtu akinadi upya,uimara etc wa gari kwa kutumia suala la namba la usajili eti inaanzia B,C au D upya au uimara wa gari kwa kutumia kigezo cha namba ni kujidanganya....tumia vigezo kama gari lipo katika mazingira gani kwa maana ya barabara za eneo hilo ni lami,barabara za vumbi? mmiliki wa gari alikuwa analitumia kwa kazi gani na yeye mwenyewe ni mtunzaji mzuri? gari lilisha wahi kupata ajali? gari limetembea umbali gani(mileage)? huwa linafanyiwa service au mpaka liharibike ndo lipelekwe garage? Usidanganyike namba ya gari siyo kipimo