Nipe katiba yako kwanza ili nitoe maoni

maliki marupu

Member
Nov 5, 2011
8
0
katika hali isiyo ya kikawaida viongozi wengi wa vyama vya siasa wamekuwa wakidai uwepo wa katiba mpya kama chachu ya kuleta mabadiliko ya kisiasa katika nchi yetu ya Tanzania.maono hayo ni sahihi kwa kuwa ni wajibu wa kila mtanzania kuwa na fikra zamivu zenye ueredi wa kuleta mabadiliko.Viongozi wa kisiasa na asasi za kiraia wamekuwa wakitoa mitazamo mizuri juu ya uundwaji wa katiba mpya kwa madai kuwa katiba mpya ndio mkombozi wa watanzania.wasiwasi mkubwa ni juu ya matakwa ya wanasioasa na wanahalakati kuwa ni muundo upi wa katiba unaostahili.Na ni vifungu vipi vya kikatiba vinavyoweza kuleta mabadiliko ktk nchi ya Tanzania.usawa na haki za msingi vinavyokosekana ktk katiba hii.Mtuonyeshe katiba za vyama vyenu vya siasa ili tupate ueredi yakinifu kuwa ni kwa kiasi gani katiba zenu zinawapa uhuru na haki za msingi wanachama wenu katika Asasi za kiraia na vyama vya kisiasa.Ili watanzania wajue haki na wajibu tunaoumba umeutendaje kwa vitendo katika vyama vyenu.Watanzania wanayo haki ya kuuliza na kupata ufumbuzi yakinifu asanteni sana
 
Napenda maneno matatu ya kwanza ya katiba ya US "WE THE PEOPLE" je sisi tutaanza na maneno gani "WE CCM"
 
Back
Top Bottom