JOSEPHAT J BAZA
Member
- May 4, 2013
- 27
- 22
Wanaharakati, wasomi wa sheria na wanataaluma wa lugha ya kiswahili naomba mnisaidie maana sahihi ya neno "uchochezi". Nimeamua kuomba msaada huu wa tafsiri sahihi ya neno "uchochezi" ili niwe salama ninapotoa maoni na mtazamo wangu juu ya mambo mbalimbali katika jamii yetu. Kwa mujibu wa katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 ibara ya 18 inasema hivi: Every person-
(a) has a freedom of opinion and expression of his/her ideas:
(b) has a right to seek, receive and, or disseminate information regardless of national boundaries. Kutokana na haki hizo tulizopewa na katiba kinachonishangaza ni kwamba leo hii katika nchi yetu ukitoa maoni yanayolenga kukosoa utawala na vyombo vyake unakamatwa na kufunguliwa kesi ya "uchochezi" sasa najiuliza, useme nini ili usionekane "mchochezi" ? Katika nchi inayofuata mfumo wa vyama vingi vya siasa kutofautiana kiitikadi na kimawazo si uadui ni mwanzo wa upanuzi wa demokrasia na kuleta maendeleo. Watawala wetu wanapaswa kujua kuwa mitazamo na mawazo tofauti ndiyo imeifanya dunia yetu kupiga hatua ktk uvumbuzi wa teknolojia mbalimbali.
(a) has a freedom of opinion and expression of his/her ideas:
(b) has a right to seek, receive and, or disseminate information regardless of national boundaries. Kutokana na haki hizo tulizopewa na katiba kinachonishangaza ni kwamba leo hii katika nchi yetu ukitoa maoni yanayolenga kukosoa utawala na vyombo vyake unakamatwa na kufunguliwa kesi ya "uchochezi" sasa najiuliza, useme nini ili usionekane "mchochezi" ? Katika nchi inayofuata mfumo wa vyama vingi vya siasa kutofautiana kiitikadi na kimawazo si uadui ni mwanzo wa upanuzi wa demokrasia na kuleta maendeleo. Watawala wetu wanapaswa kujua kuwa mitazamo na mawazo tofauti ndiyo imeifanya dunia yetu kupiga hatua ktk uvumbuzi wa teknolojia mbalimbali.