Nini kinaendelea juu la gawio TTCL?

Nini kinaendelea juu la gawio TTCL?

mkimagii

Member
Joined
Oct 16, 2013
Posts
34
Reaction score
58
Habari mkuu,
Baada ya gawio la TTCL kwa Serikali siku ya leo,kumekuwa na baadhi ya watu wanasema kwamba sio vyema kugawa gawio wakati huo huo TTCL wanaitaji pesa. Lakini upande mwingine,kumekuwa na watu wanasema kwamba Ugawaji wa gawio wa TTCL ni jambo lakujivunia maana linaonesha uwajibikaji.

Mimi nadhani sio kosa kutoa gawio kidogo,wametoa 2.1B ambayo ni 1.2%.Hii ni sehemu ndogo sana ya faida(100%) ambayo huwezi kusema kwamba inaweza kutela mabadiliko(effects) kwenye malengo ya kukusanya hiyo 1.7Trillion.Hii ni kwasababu 2.1B ni 0.1% ya 1.7Trillion, kama unavyoona ni kwamba hili gawio halina effect yeyote kwenye malengo.

Kawaida watu huwa wanapenda au kuvutiwa kuwekeza sehemu ambazo wanategeneza faida na kupunguza uwekezaji kwenye sehemu amabazo hazina faida.Kama ni hvyo,bila shaka mkurugenzi ameweza kucheza karata yake vyema, amemuonjesha mwekezaji(Serikali) asilimia ndogo ili kumpa moyo azidi kuwekeza. Wakati huo huo atakuwa anatetea ajira yake au hata kuwa na uwezekano wakupandishwa cheo.

Badala ya kuangalia kampuni ya Vodacom Tanzania,nimegunduwa mwaka 2017 na 2018 ilipata faida ya 48B na 170B. Wakati huo TTCL ilipata 119B na 167B. Kwa kuangalia hizi tarakimu,bila shaka TTCL inaonekana kanakwamba wanafanya vizuri kuliko Vodacom -Tanzania. Hapa tutakubaliana kwamba ni kitu kinacho leta mashaka. Kama tunavyo juwa TTCL haina coverage kubwa kama Voda com-Tanzania kwenye nyanja za Masoko(marketing campaign) na wateja.

Kama ni hivyo,TTCL kufanya vizuri kuliko Vodacom ni kitu kitacho leta Walakini. Kuna uwezekano wa mahesabu kupikwa,mfano wanaweza kutolipa au kusogeza mbele gharama fulani kubwa ili kuongeza faida. Sina uwakika sana juu ya hili paka tuwe na chapisho ya mahesabu(Financial statements) ambazo kwa sasa ZIMEFICHWA hazipo kabisa online.

**Kutokana na kukosekana kwa machapisho ya mahesabu(Financial statements) ya TTCL ni ngumu kuweza kupata picha halisi au ukweli wa hili swala.Kama ni hivyo, mawazo yangu hapo juu yanaweza kuwa sio ya kweli. Nakaribisha mawazo mengine.
Asanteni.
 
Habari mkuu,
Baada ya gawio la TTCL kwa Serikali siku ya leo,kumekuwa na baadhi ya watu wanasema kwamba sio vyema kugawa gawio wakati huo huo TTCL wanaitaji pesa. Lakini upande mwingine,kumekuwa na watu wanasema kwamba Ugawaji wa gawio wa TTCL ni jambo lakujivunia maana linaonesha uwajibikaji.

Mimi nadhani sio kosa kutoa gawio kidogo,wametoa 2.1B ambayo ni 1.2%.Hii ni sehemu ndogo sana ya faida(100%) ambayo huwezi kusema kwamba inaweza kutela mabadiliko(effects) kwenye malengo ya kukusanya hiyo 1.7Trillion.Hii ni kwasababu 2.1B ni 0.1% ya 1.7Trillion, kama unavyoona ni kwamba hili gawio halina effect yeyote kwenye malengo.

Kawaida watu huwa wanapenda au kuvutiwa kuwekeza sehemu ambazo wanategeneza faida na kupunguza uwekezaji kwenye sehemu amabazo hazina faida.Kama ni hvyo,bila shaka mkurugenzi ameweza kucheza karata yake vyema, amemuonjesha mwekezaji(Serikali) asilimia ndogo ili kumpa moyo azidi kuwekeza. Wakati huo huo atakuwa anatetea ajira yake au hata kuwa na uwezekano wakupandishwa cheo.

Badala ya kuangalia kampuni ya Vodacom Tanzania,nimegunduwa mwaka 2017 na 2018 ilipata faida ya 48B na 170B. Wakati huo TTCL ilipata 119B na 167B. Kwa kuangalia hizi tarakimu,bila shaka TTCL inaonekana kanakwamba wanafanya vizuri kuliko Vodacom -Tanzania. Hapa tutakubaliana kwamba ni kitu kinacho leta mashaka. Kama tunavyo juwa TTCL haina coverage kubwa kama Voda com-Tanzania kwenye nyanja za Masoko(marketing campaign) na wateja.

Kama ni hivyo,TTCL kufanya vizuri kuliko Vodacom ni kitu kitacho leta Walakini. Kuna uwezekano wa mahesabu kupikwa,mfano wanaweza kutolipa au kusogeza mbele gharama fulani kubwa ili kuongeza faida. Sina uwakika sana juu ya hili paka tuwe na chapisho ya mahesabu(Financial statements) ambazo kwa sasa ZIMEFICHWA hazipo kabisa online.

**Kutokana na kukosekana kwa machapisho ya mahesabu(Financial statements) ya TTCL ni ngumu kuweza kupata picha halisi au ukweli wa hili swala.Kama ni hivyo, mawazo yangu hapo juu yanaweza kuwa sio ya kweli. Nakaribisha mawazo mengine.
Asanteni.
IMG-20190521-WA0029.jpeg
 
Kukumbuka ttcl ndio wamiliki wa mkongo wa taifa
So kwa maoni yangu ni kama wao ndio supplier mkubwa wa data kwenye makampuni ya simu, mabenk na wengine wengi
 
ttcl wamejitahidi sana,faida zaidi ya bilioni 100 sio mchezo,hata vodacom hawafuati hapo,,kwanza vodacom mtaji wake wote hauzidi bilioni 10
 
Kwa hiyo ulitaka aseme kuwa TTCL imo ICyuuu inaomba msaada wa oxygen?? Acheni watu wajieleze wawezavyo tupone
 
Kabiashara kangu kaliniingizia faida ya 1M (T shillings) mwaka jana Ila kama jumatatu inavyoitangulia jumanne,
TTCL hii yetu haikutengeneza hata nusu ya faida niliyotengeneza mimi. It is simply NOT POSSIBLE.
 
Hivi kweli inakuingia akilini kuwa TTCL ilipata faida ya 119 Bilion na 167 Bilion kwa mwaka 2017 na 2018 ???. Kweli hili ni taifa la wadanganyika
Kuna faida na mauzo ya jumla,kwenye mauzo ya jumla unatoa gharama unabaki na faida ,katika hiyo faida ndio Kiasi hicho kimetolewa serikalini kama gawio
 
Sasa kama wewe unauza jumla unashangaa vipi kuwapita wauza rejareja?
Pesa ipo kwenye data hiyonmitandqo mingine si inanunua kwa TTCL data jumla halafu wanatuuzia sisi reja reja?
Yaani Tulewe Bar iipite kiwanda kinachozalisha serengeti kwa mauzo ya serengeti?
 
Kama wana amini wanabiashara nzuri kwanini wasiende kukopa bank au wauze hisa za kampuni sokoni kwa watanzania kupata huo mtaji.

Huku ni kuchezea tu ovyo hela za walipa kodi wakati hakuna hata jitahada za marketing kama wenzao wanavyofanya kutafuta wateja.

Wao wanataka serikari iwafanyie kila kitu iwape wateja na hela juu za walipa kodi kwenye biashara ambayo hakuna financial statement wanayotoa kuonyesha umahiri wao.

Magu ni mtu rahisi kumrubuni kwenye maswala ya biashara if anything ni bora awe anaambiwa asitoe ushauri wa kibishara kabisa.
 
Kukumbuka ttcl ndio wamiliki wa mkongo wa taifa
So kwa maoni yangu ni kama wao ndio supplier mkubwa wa data kwenye makampuni ya simu, mabenk na wengine wengi
TTCL sio mmiliki ni msimamizi tu na yeye anakodi njia,mmiliki ni serikali kupitia NICTBB.
Pili kuhusu Data makampuni yamevuta Cable zao za Mkongo (Fiber Optics) direct kutoka Baharini kupitia kwa kampuni ya SEACOM East Africa.
Kama kuna vitu watakuwa wanachukua TTCL maybe ni nje ya hayo
 
Kukumbuka ttcl ndio wamiliki wa mkongo wa taifa
So kwa maoni yangu ni kama wao ndio supplier mkubwa wa data kwenye makampuni ya simu, mabenk na wengine wengi


Sijui ni formula ipi unatumia ili kufikia hitimisho hilo? Kwanza una uhakika makampuni yote ya simu yanapata huduma ya internet toka TTCL? Unataka kumaanisha wakulima ni matajiri kuliko wafanyabishara wa mazao kisa wao ndio wanawauzia mazao hao wafanyabiashara? Pitia tena formula yako as you my be living in a wrong formula.
 
Kukumbuka ttcl ndio wamiliki wa mkongo wa taifa
So kwa maoni yangu ni kama wao ndio supplier mkubwa wa data kwenye makampuni ya simu, mabenk na wengine wengi
asante kwa kulisema hili wengi huwa hawalikumbuki
 
Back
Top Bottom