Nini kifanyike kufanya mapinduzi makubwa ya kiuchumi Tanzania

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,872
28,156
Amani iwe kwenu wadau, natumai wote mu wazima wa afya tele.

Kama kawaida nimekuwa na mfululizo wa kuleta thread mbalimbali kwa ajili ya kuchangia mawazo yangu katika jukwaa hili nikiamini kuna siku wahusika watayaona na kuyafanyia kazi kwa kiwango kikubwa sana na mwisho tutapata matokeo chanya kama taifa.

Moja ya mambo ambayo nimaamini yameirudisha Tanzania nyuma kimaendeleo ni Sera za ujamaa zilizoingizwa nchini mwaka 1967 nchi ikiwa ni changa mno.

Kwa maono yangu niamini kuwa sera hizi ziliwafunga akiri jamii ya watanzania kiasi cha kuamini kila kitu ni Serikali tu kwa sababu moja ya nguzo kuu ya ujamaa ni Serikali kumiliki njia zote za kibiashara na kiuwekezaji.

Ujamaa pia unawafanya watu wasifikiri juu ya uwezo wao binafsi katika kujiondolea changamoto za kimaisha.

Kwa nini nasema ujamaa ndio umeiangusha Tanzania kiuchumi?

Kwa wale msiojua kabla ya sera za ujamaa Tanzania kulikuwa na wafanyabiashara na wawekezaji wengi sana, wazawa na wasio wazawa. Wawekezaji hawa waliwekeza kwenye Elimu, Kilimo, Ujenzi na Biashara.

Mfano ni mzungu Steyn aliyeleta kashikashi ya ndege zetu Africa Kusini. Pia kulikuwa na wakulima wakubwa Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Iringa na hata mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Kulikuwa pia na wawekezaji waliojenga mashule kama wakatoliki na taasisi za Dini na pia walikuwepo wawekezaji wa kiasi a waliowekeza kwenye majengo maeneo ya Mzizima (Dar es Salaam), Mwanza, Kagera, Dodoma, Mbeya, Iringa, Tanga, Kilimanjaro, Arusha n.k.

Sera ya ujamaa ilitaifisha sehemu kubwa ya mambo yote hapo juu na hapo ndipo tatizo lilipoanza.

Matokeo ya Sera za ujamaa kwa Watanzania:

1. Ni kuondoa uwezo wa wananchi kufikiria juu ya uwezo wao binafsi katika kutatua changamoto za kimaisha

2. Kuharibu njia zote nzuri za kiuchumi zilizowekwa na wakoloni ambazo zilikuwa thabiti. Viwanda vilikufa, mashamba na biashara zilikufa.

3. Ambalo ni kubwa zaidi ni kuwepo kwa Fikra mfu kuwa mtu kuwa na pesa ni dhambi, beberu na mnyanyasaji

4. Kuharibu fikra za watanzania mpaka wanaoajiliwa serikalini kutowaza kibiashara na kiuwekezaji. Waajiliwa wengi wa Serikali na taasisi zake hawaoni thamani ya Biashara, hawawazi kibiashara na kupelekea uwekezaji mzuri kukwama kutokea Tanzania na wawekezaji kuikimbia Tanzania.

Nini Kifanyike:

1. Mtaala wa Elimu kuanzia shule za msingi hadi chuo ubadirishwe. Wanafunzi wafundishwe kujiajili, maana ya kazi binafsi na pia wafundishwe skills zaidi kuwawezesha kuwaza na kutenda kibiashara na kuona changamoto za kidunia

2. Sera za nchi zinadirishwe, uwekezaji wa ndani na nje ndo iwe first priority kwa taifa. Watu wawaze biashara, watende biashara na wafanye kila kitu kibiashara

3. Serikali iondoe influence kwenye uwekezaji na biashara. Sera zisiwe zinabadirishwa kila uchao ili kutengeneza confidence kwa wawekezaji wa ndani na wa nje.

Nawatakia weekend njema.
 
Jiwe atolewe tu Madarakani. Katiba ya Warioba ianze kuwa Implemented, hakika tunaweza aanza hata Kuwaza Kuifikia Kenya na hata Kuipiku kabisa.
 
Jiwe atolewe tu Madarakani. Katiba ya Warioba ianze kuwa Implemented, hakika tunaweza aanza hata Kuwaza Kuifikia Kenya na hata Kuipiku kabisa.
Sidhani kama tutakuwa tumeondoa Tatizo. Hata huyo jiwe akifanyia kazi haya kama nchi lazima tubadirike na kuona matokeo chanya kwa kiasi kikubwa sana
 
1. Elimu

2.Elimu

3. Elimu

4. Katiba , serikali kuu ipunguziwe nguvu na madaraka, sera za taifa ziwekewe misingi imara kuliko viongozi n.k.....

6. Mazingira bora kwa ukuaji wa sekta binafsi kama punguzo la kodi na mchakato rahisi wa kurasimisha biashara.

8. Neno la Nyerere "Huwezi kuwaendeleza watu ila unawapa nyenzo muhimu kujiendeleza wenyewe"..
 
Sidhani kama tutakuwa tumeondoa Tatizo. Hata huyo jiwe akifanyia kazi haya kama nchi lazima tubadirike na kuona matokeo chanya kwa kiasi kikubwa sana
No, kwa Kiasi Kikubwa Mateso yote haya Yameletwa na CCM. Kubali ama ukatae, huo ndiyo Ukweli!
 
Sidhani kama tutakuwa tumeondoa Tatizo. Hata huyo jiwe akifanyia kazi haya kama nchi lazima tubadirike na kuona matokeo chanya kwa kiasi kikubwa sana
Ukiandika wazo lolote ni vizuri kuhakikisha unatumia maneno sahihi ili kuwashawishi wasomaji. Mtu anaposoma na kukutana na maneno kama tubadirike (tena nyingi kweli kweli) na waajili badala ya waajiri basi anakuweka kwenye kundi la mbumbumbu na wazo lako halitakuwa na ushawishi. Unaweza kuona ni jambo dogo (kama wabongo wengi wanavyodhani) ila linatia doa kweli kweli ulichoandika.
 
No, kwa Kiasi Kikubwa Mateso yote haya Yameletwa na CCM. Kubali ama ukatae, huo ndiyo Ukweli!
Ni ukweli usiopingika kuwa CCM wana sehemu katika kuchangia haya kwa sababu walishindwa kumshawishi Nyerere juu ya sera za ujamaa. Pia walishundwa kuiga vizuri kwa wenzao chama tawala cha China ambacho kiliamua kubadiri sera zake baada ya kuona dunia inabadirikiwa kwa kasi.

Ndo mana leo China ni second largest economy in the world na soon he will be first.
 
Ukiandika wazo lolote ni vizuri kuhakikisha unatumia maneno sahihi ili kuwashawishi wasomaji. Mtu anaposoma na kukutana na maneno kama tubadirike (tena nyingi kweli kweli) na waajili badala ya waajiri basi anakuweka kwenye kundi la mbumbumbu na wazo lako halitakuwa na ushawishi. Unaweza kuona ni jambo dogo (kama wabongo wengi wanavyodhani) ila linatia doa kweli kweli ulichoandika.
Asante kwa kunirekebisha ndugu. Ila sio sahihi kuwa uandishi wa r na l unamfanya mtu awe mbumbumbu. Just get the message mzee. Hivyo ndo vitu watanzania tunazingatia na havina msingi wowote.
 
1. Elimu

2.Elimu

3. Elimu

4. Katiba , serikali kuu ipunguziwe nguvu na madaraka, sera za taifa ziwekewe misingi imara kuliko viongozi n.k.....

6. Mazingira bora kwa ukuaji wa sekta binafsi kama punguzo la kodi na mchakato rahisi wa kurasimisha biashara.

8. Neno la Nyerere "Huwezi kuwaendeleza watu ila unawapa nyenzo muhimu kujiendeleza wenyewe"..
Nakubaliana na wewe ndugu. China walipogundua Dunia inabadilika waliamua kupeleka vijana wao wengi sana nje kwenda kusoma ikiwemo ulaya na America akiwemo huyu raisi wa sasa Xi jiping.
Hawa ndo walienda kuiba akili za wazungu ulaya na america na kuzipeleka China
 
Amani iwe kwenu wadau,
Natumai wote mu wazima wa afya tele. Kama kawaida nimekuwa na mfululizo wa kuleta thread mbalimbali kwa ajili ya kuchangia mawazo yangu katika jukwaa hili nikiamimi kuna siku wahusika watayaona na kuyafanyia kazi kwa kiwango kikubwa sana na mwisho tutapata matokeo chanya kama taifa.

Moja ya mambo ambayo nimaamini yameirudisha Tanzania nyuma kimaendeleo ni Sera za ujamaa zilizoingizwa nchini mwaka 1967 nchi ikiwa ni changa mno.

Kwa maono yangu niamini kuwa sera hizi ziliwafunga akiri jamii ya watanzania kiasi cha kuamini kila kitu ni Serikali tu kwa sababu Moja ya nguzo kuu ya ujamaa ni Serikali kumiliki njia zote za kibiashara na kiuwekezaji.
Ujamaa pia unawafanya watu wasifikiri juu ya uwezo wao binafsi katika kujiondolea changamoto za kimaisha.

Kwa nini nasema ujamaa ndo umeiangusha Tanzania kiuchumi
.
Kwa wale msiojua kabla ya sera za ujamaa Tanzania kulikuwa na wafanyabiashara na wawekezaji wengi sana, wazawa na wasio wazawa. Wawekezaji hawa waliwekeza kwenye Elimu, Kilimo, Ujenzi na Biashara.
Mfano ni mzungu Steyn aliyeleta kashikashi ya ndege zetu Africa KUSINI. Pia kulikuwa na wakulima wakubwa Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Iringa na hata mikoa ya kanda ya ziwa. Kulikuwa pia na wawekezaji waliojenga mashule kama wakatoliki na taasisi za Dini na pia walikuwepo wawekezaji wa kiasi a waliowekeza kwenye majengo maeneo ya Mzizima(Dar es Salaam), Mwanza, Kagera, Dodoma, Mbeya, Iringa, Tanga , Kilimanjaro, Arusha n.k. Sera ya ujamaa ilitaifisha sehemu kubwa ya mambo yote hapo juu na hapo ndipo tatizo lilipoanza.

Matokeo ya Sera za ujamaa kwa Watanzania
1. Ni kuondoa uwezo wa wananchi kufikiria juu ya uwezo wao binafsi katika kutatua changamoto za kimaisha

2. Kuharibu njia zote nzuri za kiuchumi zilizowekwa na wakoloni ambazo zilikuwa thabiti. Viwanda vilikufa, mashamba na biashara zilikufa.

3. Ambalo ni kubwa zaidi ni kuwepo kwa Fikra mfu kuwa mtu kuwa na pesa ni dhambi, beberu na mnyanyasaji

4. Kuharibu fikra za watanzania mpaka wanaoajiliwa serikalini kutowaza kibiashara na kiuwekezaji- Waajiliwa wengi wa Serikali na taasisi zake hawaoni thamani ya Biashara, hawawazi kibiashara na kupelekea uwekezaji mzuri kukwama kutokea Tanzania na wawekezaji kuikimbia Tanzania.

Nini Kifanyike.
1. Mtaala wa Elimu kuanzia shule za msingi hadi chuo ubadirishwe. Wanafunzi wafundishwe kujiajili, maana ya kazi binafsi na pia wafundishwe skills zaidi kuwawezesha kuwaza na kutenda kibiashara na kuona changamoto za kidunia

2. Sera za nchi zinadirishwe, uwekezaji wa ndani na nje ndo iwe first priority kwa taifa. Watu wawaze biashara, watende biashara na wafanye kila kitu kibiashara

3. Serikali iondoe influence kwenye uwekezaji na biashara. Sera zisiwe zinabadirishwa kila uchao ili kutengeneza confidence kwa wawekezaji wa ndani na wa nje.


Nawatakia weekend njema.
Sera za kijamaa wafanye masikini ili utatawale kirahisi
 
Kilimo kipewe kipaumbele
Kweli Kabisa.
Moja ya njia nzuri za kukipa kilimo kipaumbele ni kuruhusu uwekezaji mkubwa wa teknolojia kubwa na nzuri kwenye kilimo. Hili litaleta mazao bora yenye ushindani kwenye soko la kimataifa. Hili lazima liletwe kwa kuruhusu ushindani kwenye kilimo

Tumeshindwa hata kuruhusu watu kuweka teknolojia bora kwenye mifugo yetu ili kuwa fanya watu wetu wafuge kisasa kwenye maeneo madogo na kibiashara.
 
Sera Za Mabenki kuwa rafiki, Sera Za TRA kuwa rafiki Miundombinu kama umeme, maji lazima vipatikane kwa uhakika mfano mtu anaweza pewa mkopo akimaliza masomo yake akiwa na good busness plan dhamana yake viwe vyeti vyake.
 
Mkuu Mtoa Mada, hakuna Namna, ila tusogee Mbele lazima CCM iondoke Madarakani. Kuna makosa mengi saana yanayoendelea ikiwa ni pamoja na Siasa Kushika hatamu kuliko kuoambania Uchumi. Halafu Mbaya Zaidi Viongozi hata Wafanye Madudu hakuna Mfumo wa Kufanya Wajutie kwa lazima ili wa Nyuma yao wasiingie huko.
 
Mkuu Mtoa Mada, hakuna Namna, ila tusogee Mbele lazima CCM iondoke Madarakani. Kuna makosa mengi saana yanayoendelea ikiwa ni pamoja na Siasa Kushika hatamu kuliko kuoambania Uchumi. Halafu Mbaya Zaidi Viongozi hata Wafanye Madudu hakuna Mfumo wa Kufanya Wajutie kwa lazima ili wa Nyuma yao wasiingie huko.
Ni kweli kuwa CCM wana sehemu kubwa ya kulaumiwa kwa haya. Ila hata wao wana nafasi ya kuyaona haya na kuyachukulia hatua za haraka. Still wana nafasi
 
Mitaala ya elimu haifai unamfundisha kijana kiswahili na history mpaka form six alafu unamtaka akajianiri,

badili mitaala ya hizi secondary schools kuwa vocation training.
Weka vocation centre kila kata.
 
Sera Za Mabenki kuwa rafiki, Sera Za TRA kuwa rafiki Miundombinu kama umeme, maji lazima vipatikane kwa uhakika mfano mtu anaweza pewa mkopo akimaliza masomo yake akiwa na good busness plan dhamana yake viwe vyeti vyake.
Kweli kabisa- ila kufanikisha haya lazima kwanza mentality za watu zinadilishwe. Kuna jambo kubwa sana linatakiwa lifanywe tena kitaifa kubadilisha mentality za watu wawaze na kufikiri kibiashara. Hayo yatawezekana tu pale watu watakapoanza kuanza kuwaza na kufikiri kibiashara
 
Mitaala ya elimu haifai unamfundisha kijana kiswahili na history mpaka form six alafu unamtaka akajianiri,

badili mitaala ya hizi secondary schools kuwa vocation training.
Weka vocation centre kila kata.
Inasikitisha ndugu. Alafu badae anakuja kuwa afisa Ardhi wizarani, anamzungusha muwekezaji miaka 2 kupata tu hatimiliki ya kiwanja tu ili ajenge kiwanda.
Yote ni kwa sababu hajui kuwa muwekezaji ana hela na anakuja kutengeneza ajila na kulipa kodi
 
Back
Top Bottom