Nini asili ya neno 'Zeluzelu'?

Nini asili ya neno 'Zeluzelu'?

kidole007

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2012
Posts
3,094
Reaction score
1,877
Wataalamu wa lugha ya kiswahili husikeni na kichwa hapo juu. Tumezoea kuwaita ndugu zetu wenye albinism zeruzeru, nini asili (etiology) ya neno hili?
 
Dah mbona mtihani wa kiswahili zelu zelu au zeru zeru
 
Hahahaaaa zelu zelu, r inakusumbua ngoja wataalum waje waanze na ww
 
Kuna mtu alilianzisha ndio ikapewa maana hiyo na ndio mwanzo wake.
 
Lugha nyingi za kibantu hutumia neno zeru, nzeru,izeru nk. Ili kumaanisha nyeupe au enye weupe, so nahic walitumia hilo neno kumaanisha MTU mweupe,
 
ukichunguza utagundua kuwa herufi "eru" ni msingi wa neno linalotumiwa na baadhi ya waongeaji wa kibantu kumaanisha "eupe" (white)

kwa wahaya utapata "rweru" makabila mengine utapata "nzeru" "nderu" "ng'eru" nk...so nina imani kabisa kwa kuwa albino ni weupe (at least kwa umaskini wa majina ya rangi kwenye kiswahili) basi neno zeru zeru litakuwa lina chimbuko lake hapo kumaanisha weupe usiomithilika
 
Siku chache zilizopita nilijadiliana na ndugu mmoja kuhusu maana za maneno yafuatayo:

1) JINSI/NAMNA

Yule ndugu anadai kwamba maneno hayo yana maana tofauti:

"Bwana X hebu nieleze NAMNA/AINA ya mapokezi uliyopewa na wenyeji wako ulipotembelea Dar".

"Bwana X hebu nieleze JINSI ulivyoupenda mji wa Dar"

Licha ya hayo NAMNA siku hizi lina maana ya "a hidden agenda":

"Bw. X kuwa anakwenda kusini mwa Tanzania kila mwaka, kuna NAMNA siyo bure!!!"

"Hebu tumuulize ni NAMNA gani aliweza kupafahamu kusini mwa Tanzania?"

"Hebu nino atueleze ni JINSI gani mtu anaweza kufika kusini mwa Tanzania kwa kutumia usafiri wa Basi na ni NAMNA gani anaweza kukabiliana na misukosuko ya njiani."

2) -TIA/-WEKA

Yule ndugu anadai kwamba:

"Wazanzibari wanapendelea -TIA, lakini watanzania wengine wanapendelea -WEKA, kwa sababu neno 'kutia' lina maana ya 'kutomba' na wazanzibari wanapenda uchezeaji wa maneno"

3) DURU/MZUNGUKO

Yule ndugu anadai kwamba:

"kwenye mchezo wa mpira matumizi ya 'duru' ni sawa, lakini kwenye mchezo wa bao inafaa kutumia 'mzunguko' kwa sababu watu wengi wanachanganya 'duru ya' na 'duru za'"

Ningependa sana kusoma maoni yenu.
Asanteni.

Umenitoa tongo tongo
 
ukichunguza utagundua kuwa herufi "eru" ni msingi wa neno linalotumiwa na baadhi ya waongeaji wa kibantu kumaanisha "eupe" (white)

kwa wahaya utapata "rweru" makabila mengine utapata "nzeru" "nderu" "ng'eru" nk...so nina imani kabisa kwa kuwa albino ni weupe (at least kwa umaskini wa majina ya rangi kwenye kiswahili) basi neno zeru zeru litakuwa lina chimbuko lake hapo kumaanisha weupe usiomithilika

Umenena vizur japo sina uhahika kma makabila yote yenye asili ya kibantu neno nzeru linamanisha nyeupe
 
Umenena vizur japo sina uhahika kma makabila yote yenye asili ya kibantu neno nzeru linamanisha nyeupe

Usiwe kichwa ngumu ndugu,hakuna alipoandika makabila yote.Amesema baadhi ya waongeaji wa wa lugha za kibantu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom