Wana JF heshima kwenu? Ninajua wapo kati yetu tunaompenda Magufuli kupitiliza hali kadhalika wale baina yetu tusiompenda hata kumuita majina kama Dikteta. Demokrasia inawaruhusu wote kufanya hayo hivyo sitawaingilia. Kubwa ninalotaka kusema ni kuwa mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Magufuli ni muwazi sana. Kwa mfano, hivi majuzi aliutoa uwazi wa viwango vya juu mno ingawa nimeshangaa watu kama hawakuuelewa. Kwa kifupi alisema CCM yake ni kama zizi ambalo ndani yake kuna ng'ombe wengine wana mikia wengine mikia yao imekatwa. Bila kuingia katika discussion ya mikia, ninataka tufocus katika uwazi huu kwamba kwake wanachama wa CCM ni ng'ombe. Sie tunaotoka kanda ya ziwa na kwingine kwenye jamii ya wafugaji tunajua haki za ng'ombe ni zipi. KWa kifupi, ng'ombe huwa anasagwa kokote mfugaji anataka waende. Wakikaidi wanakula mijeledi warudi kwenye mstari. Kwa maana nyingine, mheshimiwa rais alikuwa nasema mang'ombe wasubiri kusagwa kwa kuambiwa nini waseme, wapi waende nk. Hii ndio maana halisi ya kudumu fikra sahihi za mwenyekiti wa chama, hali kadhalika chama kushika hatamu (steering devise ya mifugo). Hiki ndicho kinachoendelea sasa ingawa tulikuwa hatujajua details zake. Hongera zote kwa mwenyekiti wa chama.