Nina wasi wasi na hali ya usalama Kanisa la Ufufuo na Uzima

Tulimumu

JF-Expert Member
Mar 11, 2013
14,409
13,262
Mimi si muumini wa kanisa la ufufuo na uzima lakini ni mkristo. Siku moja nilifika pale kanisani. Ukifika pale unapoingia upande wa kushoto kuna banda limejengwa kama ghorofa likiwa limewekewa chuma za mataaluma kama zile za reli kama nguzo zake. Sasa wanaposali kule juu huwa wanasali huku wanatembea na kuruka ruka. Niliona lile banda linayumba sana kutokana na watu waliokuwa kule juu kusali huku wakiruka ruka na kucheza. Nilipoangalia vizuri zile chuma nikaona kwa chini zimeshaliwa na kutu kiasi kwama kuna siku isiyokuwa na jina inaweza kutokea ajali ya lile banda kudondoka wakati kwa chini kuna watu wamekaa kwani lile kanisa ni finyu lakini waumini ni wengi sana.

Ninaomba uongozi wa kanisa uchukue tahadhari kwani ukiangalia uimara wa zile chuma na mzigo wa watu kule juu ni kwamba zile chuma znazidiwa na wakati huo huo kwa upande wa chini huwa kunakuwa na waumini wakiwa wanasali sasa likija kuanguka litaua watu wengi sana. Tusingoje mpaka litokee la kutokea kama kule Nigeria ndipo tuanze kuunda tume. Naomba pia uongozi utafute sehemu nyingine yenye nafasi kwani pale ni padogo kutokana na wingi wa waumini wanaokuja kusali pale kwani pia kuna sehemu wameunga unga tu lakini kuna bonde. Vile vile eneo la parking ni dogo kiasi kwamba waumini wanapaki barabarani. Majeshi majeshi! Majeshi ya Bwana!
 
Mimi si muumini wa kanisa la ufufuo na uzima lakini ni mkristo. Siku moja nilifika pale kanisani. Ukifika pale unapoingia upande wa kushoto kuna banda limejengwa kama ghorofa likiwa limewekewa chuma za mataaluma kama zile za reli kama nguzo zake. Sasa wanaposali kule juu huwa wanasali huku wanatembea na kuruka ruka. Niliona lile banda linayumba sana kutokana na watu waliokuwa kule juu kusali huku wakiruka ruka na kucheza. Nilipoangalia vizuri zile chuma nikaona kwa chini zimeshaliwa na kutu kiasi kwama kuna siku isiyokuwa na jina inaweza kutokea ajali ya lile banda kudondoka wakati kwa chini kuna watu wamekaa kwani lile kanisa ni finyu lakini waumini ni wengi sana.

Ninaomba uongozi wa kanisa uchukue tahadhari kwani ukiangalia uimara wa zile chuma na mzigo wa watu kule juu ni kwamba zile chuma znazidiwa na wakati huo huo kwa upande wa chini huwa kunakuwa na waumini wakiwa wanasali sasa likija kuanguka litaua watu wengi sana. Tusingoje mpaka litokee la kutokea kama kule Nigeria ndipo tuanze kuunda tume. Naomba pia uongozi utafute sehemu nyingine yenye nafasi kwani pale ni padogo kutokana na wingi wa waumini wanaokuja kusali pale kwani pia kuna sehemu wameunga unga tu lakini kuna bonde. Vile vile eneo la parking ni dogo kiasi kwamba waumini wanapaki barabarani. Majeshi majeshi! Majeshi ya Bwana!
Usahwapa watu sababu ya kulifungia. Walikuwa wanaitafuta kwli hii.
 
WE NDIO ULIOENDA JUMAPILI KUSIKIA ANASEMAJE ILI UPATE LA UMBEA,
UMELIKOSA SASA UKAAMUA KUTAFUTA KASABABU HAKO
 
Kwaivyo ulishindwa hata kuwaona wasimamizi pale ukawajulisha hadi uje uweke hapa wakt unajua kabsa mungu wa dar akiona atapata sababu
 
Usahwapa watu sababu ya kulifungia. Walikuwa wanaitafuta kwli hii.


Yaani kwa taarifa hii, Gwajima na kanisa lake siku zao zimehesabiwa. Kwanza watakuja Bodi ya Wakandarasi, kama haitoshi TanRoads nao haooo, usishangae Jiji nao wakafunga tela! Mwisho wa siku wataambiwa hilo eno ni dogo kiusalama kwa idadi ya watu hao na inawapasa aidha wagawe kanisa au watafute mahali pengine ---Kibahaaaa au Bwagamoyo maana Dar hakuna viwanja.... Nawaza tu!!
 
Back
Top Bottom