Nina matatizo au ana matatizo? Sielewi

Nina matatizo au ana matatizo? Sielewi

Bunyu

Senior Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
119
Reaction score
32
Nahitaji kupewa thamani kama mume kutoka wake!
Nikimpigia simu asiongee na mm huku akiendelea kuongea na waliokaribu nae kwakuwa Mimi huwa sifanyi hivo!

Tukimaliza kuongea tuagane vzr na siyo kunikatia simu eti kisa alikuwa amemaliza mazungumzo! Kwakuwa huwa sifanyi hivo!

Jukumu la kulinda mustakabali wa mapenzi yetu upo mikononi mwetu sote so ni jukumu la kila mmoja wetu kuzungumza na mwenzie kunapotokea mmoja anakuwa hayupo normal.
Lkn mwenzangu huyu hata kama yeye ndo kanikwaza hashughuliki kutatua tatizo badala yake ananiangalia tu na hata akimbiwa kwamba amenikwaza anakuwa mgumu kuelewa na kutoelewa kwamba hali hiyo inaniathiri na inanifanya nisimuone rafiki Yangu tena!

Hivi mlooa muda mrefu hivi ndivyo muishivyo?
Au hilo siyo tatizo? Mi linaniathiri lkn!
 
Umejaribu kuongea na huyo mwenzako kwanza ?
 
hahahahahahahahahaaaaa....pole mangi....ndoano yako ina muda gani?........duh..wanazingua hawa mbavu zetu!!!,,,,yaani akishaingia kunako ndoa......sauti ya mziki inaongezeka twice......hahahahahhahaaaaa........wengi wetu huwa tunajilipua tuu.....nyumbani kama kituo cha geshi bana....
 
Sasa badala ya kumwambia mwenyewe unakuja kutuambia sisi, dah!

Sisi tutakusaidia nini sasa kumbadilisha, mwenzio yuko na mchepuko wake, wewe unasumbua sumbua.

Alikuwa hai hai ili asiulizwa huyo nani, na mkianza kuagana yatakuja mambo ya nakupenda wakati pembeni kuna mchepuko.

Ndo mapenzi ya mbali hayo.
 
Unajua mnapokutana wote mna meno 32 ni kazi sana lazima mkubali kuchukuliana na kusameheana la sivo ndowa mtaisikia kwenye bomba
 
Kama mwanzo hakuwa hivyo basi anatatizo la kisaikolojia linalohitaji ukaribu wako kwake au ni mimba changa.
Chunguza.Jipe muda. Mapenzi yanahitaji sayansi na sanaa inayohitaji upya.
 
Yupo hivyo tangu zamani au ndo amekuwa kuwa hivyo sasa hivi? Umeshawahi kukaa naye ukamueleza jinsi unavyojisikia kutokana na hiyo tabia yake?
 
pole sana ndoa ni uvumilivu sio lele mama jitahidi kuongea nae ujue tatizo liko wapi
 
Inawezekana wote Hamna tatizo...watu Wengine hawajalelewa kuwa na ustaarabu huo.....kuna watu unamwambia naumwa anakujibu tu 'okay' hajui kusema pole...au ugua pole...mfundishe taratibu ...
 
hahahahahahahahahaaaaa....pole mangi....ndoano yako ina muda gani?........duh..wanazingua hawa mbavu zetu!!!,,,,yaani akishaingia kunako ndoa......sauti ya mziki inaongezeka twice......hahahahahhahaaaaa........wengi wetu huwa tunajilipua tuu.....nyumbani kama kituo cha geshi bana....

Mbavu wetu hawazingui mkuu ukiona anazingua ujue uliiba ubavu wa mtu mwingine.
 
Inawezekana wote Hamna tatizo...watu Wengine hawajalelewa kuwa na ustaarabu huo.....kuna watu unamwambia naumwa anakujibu tu 'okay' hajui kusema pole...au ugua pole...mfundishe taratibu ...

Mimi huwa nachukia, mtu unamwambia ninaskia njaa, naye anakujibu hata mimi pia; au ninahisi vibaya basi na yeye anajibu hivyo. Kwanini asikuambie pole kwanza halafu ndio naye aseme shida yake. Sababu ya kumwambia ni kupata tulizo na si kuongezewa matatizo.
 
Mwanaume haipendezi kulalamika hivyo, duh.
 
Back
Top Bottom