Plato
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 420
- 94
Nashindwa kufanya maamuzi.nisaidieni mawazo.yanisaidie kufanya maamuzi. Nina wasichana 2,mmoja ni mchumba wangu,uchumba wetu una miaka 3 sasa,na tumetoa zaidi ya mahari.nilimpromisse kumuoa mwaka kesho akasema atanisubiri na amefanya hivyo.ninampenda sana.nadhani naye ananipenda.lakini upande mwingine rafiki yangu wa miaka mingi(msichana) mhitimu wa university ambaye aliachana na boyfriend wake na akakaa zaidi ya mwaka bila uhusiano.ikatokea tumezoeana sana ndg zake wengi wakanijua tukawa kama ndugu.mwaka jana nikiwa na mchumba tayari tukaanza kuwa na mahusiano ya mapenzi.akawa anaongea kuwa anaridhika nami hata nikimuoa kwani ananifahamu.sasa imetokea akapata mimba,na yeye kafurahi kwamba si nitamuoa.hajui habari za mchumba wa tangu kabla yake.mimba ina miezi 4 sasa.UTATA: Nimuoe nani kati yao,inaniwia vigumu kuvunja promisse kwa mchumba aliyenivumilia kwa miaka 3 sasa,wakati huohuo inaniwia vigumu kumtelekeza niliyempa mimba na kubadili maisha yake.pili nafikiri nn kitatokea kwa uamuzi wowote nitakaochukua.kwangu limekuwa zito,nishaurini.asante