Jumanne Mkota
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 2,994
- 1,770
Salaam WanaJamvi,
Kuna thread humu JF inayomhusu Paul Makonda mjumbe wa Baraza kuu la UVCCM.
Huyu Bwana ni Msomi wa Chuo Kikuu, sina uwezo wa kujua alikuwa nasomea digrii gani pale Ushirika lakini alikuwa kiongozi wa Vijana pale MUccobs.
Aliwahi kuandaa kongamano kubwa la vijana kwa kulipa sura ya siku ya UVCCM na pia Kumuenzi Mwalimu Nyerere pale kwenye Uwanja wa Ushirika Moshi. Ilikuwa ni Mwaka 2009. Mimi nikiwa ni miongoni mwa Vijana wa UVCCM Kipindi hicho.
Kwenye Kongamano hilo walikuwepo watu wafuatao;
Nadhani waheshimiwa wote hao mnawafahamu na mirengo yao. Pia kwa fikra za karibu, labda ukimuondoa Mzee Mengi hao wote ni wazee wa CCJ.
Kuonyesha kuwa huyu bwana ana mapenzi makubwa na fedh, alipewa fedha za maandalizi kiasi cha tsh 7m na Makala, 5m na mzee Mengi na Tsh 4 na Mzee Ndesamburo. Sisi kama UVCCM kipindi hicho tukijisafirisha wenyewe kutoka kwenye wilaya zetu.
Wakati mkutano unaendelea, baada ya wageni waalikwa kujitambulisha akiwemo Nape, Mengi, engineer, Harrison, tulisikia mngurumo mkali wa chopa.
Kwa wanaoijua Jiografia ya Moshi, Chuo cha Ushrika kipo juu mlimani kidogo, hivyo unaliona bonde la Kiborloni kwa chini vizuri mahali ambapo ndipo mitaa ilipo hotel ya Keys.
Baada ya Mgeni Rasmi kuanza kuhutubia vijana, huku Makonda mwenyewe akiwa bize na simu yake, Chopa lile lilikuja likatua uwanjani kwa mbwembwe likiwa limemleta Mzee Ndesamburo. Tukio ambalo lilikatisha Hotuba ya Amos Makala.
Baada tu ya kutua, Mzee Ndesa akapanda jukwaani akiwashambulia vilivyo wakina Makala.
Baada ya tukio hilo, ndilo lililofungua jina la Makonda kwenye media za hapa nchini na kujikuta ni miongoni wa mastaa hapa TZ. Tukio ambalo lilichoma TZS 6m, pesa za UVCCM mkoa wa Kilimanjaro kwa ajili ya kwenda Dar kwenye media kumkanusha Makonda kuwa sio kiongozi wa UVCCM mkoa wa Kilimanjaro.
Sasa huyo ndio Paulo Makonda, bingwa wa kuchonganisha watu na Mjasiriamali wa kisiasa. CDM mna hiyari ya kumchukua na kumfanya maarufu zaidi.
Kuna thread humu JF inayomhusu Paul Makonda mjumbe wa Baraza kuu la UVCCM.
Huyu Bwana ni Msomi wa Chuo Kikuu, sina uwezo wa kujua alikuwa nasomea digrii gani pale Ushirika lakini alikuwa kiongozi wa Vijana pale MUccobs.
Aliwahi kuandaa kongamano kubwa la vijana kwa kulipa sura ya siku ya UVCCM na pia Kumuenzi Mwalimu Nyerere pale kwenye Uwanja wa Ushirika Moshi. Ilikuwa ni Mwaka 2009. Mimi nikiwa ni miongoni mwa Vijana wa UVCCM Kipindi hicho.
Kwenye Kongamano hilo walikuwepo watu wafuatao;
- Nape Nnauye
- Reginald Mengi
- Amos Makala (ambaye alikuwa mgeni rasmi)
- Engineer Sytella Manyanya
- Harison Mwakyembe
Nadhani waheshimiwa wote hao mnawafahamu na mirengo yao. Pia kwa fikra za karibu, labda ukimuondoa Mzee Mengi hao wote ni wazee wa CCJ.
Kuonyesha kuwa huyu bwana ana mapenzi makubwa na fedh, alipewa fedha za maandalizi kiasi cha tsh 7m na Makala, 5m na mzee Mengi na Tsh 4 na Mzee Ndesamburo. Sisi kama UVCCM kipindi hicho tukijisafirisha wenyewe kutoka kwenye wilaya zetu.
Wakati mkutano unaendelea, baada ya wageni waalikwa kujitambulisha akiwemo Nape, Mengi, engineer, Harrison, tulisikia mngurumo mkali wa chopa.
Kwa wanaoijua Jiografia ya Moshi, Chuo cha Ushrika kipo juu mlimani kidogo, hivyo unaliona bonde la Kiborloni kwa chini vizuri mahali ambapo ndipo mitaa ilipo hotel ya Keys.
Baada ya Mgeni Rasmi kuanza kuhutubia vijana, huku Makonda mwenyewe akiwa bize na simu yake, Chopa lile lilikuja likatua uwanjani kwa mbwembwe likiwa limemleta Mzee Ndesamburo. Tukio ambalo lilikatisha Hotuba ya Amos Makala.
Baada tu ya kutua, Mzee Ndesa akapanda jukwaani akiwashambulia vilivyo wakina Makala.
Baada ya tukio hilo, ndilo lililofungua jina la Makonda kwenye media za hapa nchini na kujikuta ni miongoni wa mastaa hapa TZ. Tukio ambalo lilichoma TZS 6m, pesa za UVCCM mkoa wa Kilimanjaro kwa ajili ya kwenda Dar kwenye media kumkanusha Makonda kuwa sio kiongozi wa UVCCM mkoa wa Kilimanjaro.
Sasa huyo ndio Paulo Makonda, bingwa wa kuchonganisha watu na Mjasiriamali wa kisiasa. CDM mna hiyari ya kumchukua na kumfanya maarufu zaidi.