Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,762
Jamani nimezama kwa mapenzi sijui kama nitazuka naiona hali yangu taabani,wenzangu nawauliza nini dawa ya mepenzi waganga nimemaliza wa makombe na hirizi ,ilahi mola muweza ataniafu mwenyezi.
Nimezama kwa mapenzi sijui kama nitazuka,kujikwamua siwezi taabani nateseka ilahi mola mwenyezi ataniafu rabuka.nimezama mwenzenu katika kina nimebaki natizama lakutenda sina tena,Ilahi mola karima ataniafu rabbana.
Nimezama nimezama katika kina kirefu kila nikijitazama moyoni napata hofu,ilahi mola karima ndie mwenye kuniafu.nimezama nimezama kwenye bahari ya huba moyo wangu walalama unalia ,ilahi mola karima taniepushia adhabu,naiona hali yangu mimi nimedhoofika.
Nini dawa ya apenzi ?
Nimezama kwa mapenzi sijui kama nitazuka,kujikwamua siwezi taabani nateseka ilahi mola mwenyezi ataniafu rabuka.nimezama mwenzenu katika kina nimebaki natizama lakutenda sina tena,Ilahi mola karima ataniafu rabbana.
Nimezama nimezama katika kina kirefu kila nikijitazama moyoni napata hofu,ilahi mola karima ndie mwenye kuniafu.nimezama nimezama kwenye bahari ya huba moyo wangu walalama unalia ,ilahi mola karima taniepushia adhabu,naiona hali yangu mimi nimedhoofika.
Nini dawa ya apenzi ?