Nimetoka ukweni Kigoma, ila kama hii ndiyo aina ya wazee acha wabaki na watoto wao!

Na
Siungekufaa ukija Kwa sisi wamasai na umemzalisha mtoto wao bila kuoa naungepigwa mpaka usirudi Tena .

1.kwa ambaye ni bikra hajasoma ni ng'ombe 25 ambapo ukipiga mahesabu ya haraka ni ml 25
Kama ulimzalish ni ml 6 fine so 31ml .

2. Sasa awe na elimu na ni bikra huwezi mchukua kabisa kama sio ml 60 unaitoa Kwa macho

3.kama ameshatenguliwa na unamwona na anaelimu ni ml 15 bila chenga kama umemzalisha basi utaota kumi 5ml mahari na 5ml fine .

So hiyo 4.5 ni ndogo hapo hujatoa madebe 6 ya pombe ml 1 kujitambulisha
Umetoka ukoo gani na umekuja kufanya Nini
Nanyori mambo!
 
Nimekuwa kwenye mahusiano na mwanamke kutoka Kigoma tangu 2020, tulikutana chuo, na penzi likakolea haswaa!

Kipindi cha Covid penzi lilinoga zaidi kwani "Working from home" ilifanya muda wote tuwe pamoja, ilikuwa mwendo wa kwenda sokoni kununua mazaga zaga pamoja, tinaweka ndani then kila baada ya mlo ni mnyanduano tu, hatimaye binti akashika mimba!

Baada ya mimba kufikisha miezi minne bibie akaniambia ni bora aende kwao kwanza kwani kubaki tukiwa wawili hatuwezijua complications za mimba, nilikubaliana nae, nikajipiga kwa kadri ya uwezo wangu nikamkatia tiketi na vizawadi kidogo vya wazee akaenda kwao!

Akiwa kwao mawasiliano yetu yalikuwa vizuri kabisa mpaka akajifungua salama salmin, na mimi niliwajibika haswa mpaka dk. ya mwisho, hatimaye tukapata mtoto wa kiume.

Bibie baada ya mtoto kufikisha miezi 6 bila mimi kwenda kujitambulisha akatoa wazo la kurudi kwangu kwani alikuwa amechoka kuishi nyumbani kwao, nikamkaribisha tukaendelea na maisha ya sogea tuishi.

Mwaka jana December, ilitokea msiba kwao akalazimika kwenda msibani, nikamfanyia maandalizi vizuri kabisa, akaondoka.

Amekaa huko tangu December, mpaka juzi nilipoamua kufuata taratibu za kwenda kwao ili tusiendelee kuishi kimya kimya (tufanye kuwa official), nikajiandaa kwa mambo kadhaa kama nilivyokuwa nimeng'atwa sikio na mpenzi wangu.

Nimeanza safari kutoka Dar kwenda Kigoma (kwao), nikiwa nimeambatana na brother wangu wa damu, aisee kwao ni mbali, maana tulitembea siku 2 njiani, tulipofika mjini, safari ya kwenda kwao ikachukua masaa mengine 8, vumbi kali hatari, tulipofika Kijijini kwao tukaambiwa Burundi ni mwendo wa kutembea nusu saa tu.

Brother akaniuliza, "Hivi dogo hukuona wanawake mikoa yote tuliyopita mpaka kuja huku?" Nikamwambia mapenzi yana nguvu bro, sikuwahi kufikiria kama kuna siku ningesafiri umbali namna hii kufuata mwanamke tu. Tulipofika mjini tulitafuta mzee mwenyeji, anayejua mila na desturi za Kiha ili mambo yasiwe magumu.

Basi bwana, tumefika pale tumepokelewa vizuri wakaandaa utaratibu wa mjadala, mshenga akatambulisha na kuanza mazungumzo rasmi, hapo nilikuwa na zawadi ya baba mkwe na mama mkwe, nilinunua tangu Dar kwa upendo kabisa.

Wakataja kiasi cha mahari kuwa wanataka mil. 4.5, hapo tukashtuka kweli, kabla hatujakaa sawa wakataja mkaja wa mama sh. laki saba, jumla wanataka 5.2 Milioni!

Yule mzee tuliyeenda naye akaomba twende nje kwa mazungumzo, akatuuliza kama tulipewa mwongozo na tuliyekwenda kumuoa, nikamjibu ndiyo (alisema mahari kwao haizidi Milioni moja) na mkaja wa mama huwa ina-range kuanzia 100k - 200k, na mimi niliandaa 200k kama mkaja wa mama! Mzee akasema hapa kuna tatizo, huku haijawahi kutokea mahari kubwa kiasi hiki, akasema tutasimamia kwenye hiyo 1M na mkaja wa mama 200k, tukarudi ndani!

Mzee (mshenga) akaanza kuzungumza, kuwa sisi tuna mahari 800k na mkaja wa mama 100k, lakini pia tuna zawadi kwa ajili ya baba na mama, ambazo si sehemu ya mahari, ni zawadi tu ya kijana wetu kwenu, mzee akatoa zile zawadi akaweka mezani.

Mshenga wao akashukuru na kuanza kuzungumzia mahari yetu kuwa angalau tufanye mahari mil.4 mkaja wa mama 500k.

Kabla hajamaliza akasimama baba mkwe, akionyesha kukasirika akasema "Sitaki mjadala wa kitoto hapa, mimi ndiye baba wa x, mkaja wa mama laki 5, mahari yangu nataka Milioni 4, Sitaki mjadala wala kusikia kupunguziana, kwanza unabeba zawadi kutuletea nani amekutuma utununulie, tumekuomba sisi utuletee zawadi zako?"

"Kwanza huyu kijana anadharau sana, tangu mtoto azaliwe hajawahi kufika hapa nyumbani, anaishia kumtumia mwenzake pesa tu, sisi hajawahi kututumia pesa hata mara moja, tumepata msiba hajawahi kuja kutupa pole zaidi ya kupiga visimu vyake tu, sasa mimi nimeshasema mkaja wa mama laki tano, mahari Milioni 4, sitaki mjadala!"

Aisee nilijikuta nimejaa hasira mpaka basi, mshenga wetu akatutaka twende nje, akasema "huyu mzee inaonekana ana lake jambo, tusiingie kwenye mtego wake, iweni wapole, tuondoke salama, watu wa huku ni hatari sana, tukiwa na hasira tunaweza tusirudi salama, hii si dalili nzuri."

Tukajadili tuvyojiandaa pale, mzee akasema muhimu tuanze na mkaja wa mama, tuwawekee hiyo 500k then tutawapa faini za mbuzi mbuzi, na vingine vidogo vidogo, baada ya hapo mahari tuwaambie kuwa tunaenda kuitafuta then mtaangalia wenyewe baada ya kufika nyumbani!

Tuliporudi ndani tukakuta mzee anaonyesha kuwa na hasira hasira tu, kiasi kwamba mshenga wao akawa ameduwaa tu, basi mshenga wetu akaanza kujitetea pale, akaweka mezani sh. 500k mkaja wa mama, akawaambia mbuzi watatu wa uchafuzi 300k sijui koti la mjomba, mara blanketi ya wazee na vikolo kolo vingine kwa Kadri ya taratibu zao, ile pesa tuliyoenda nayo ikawa imekata!

Muda huo wote Nina hasira vibaya mnooo, ila najitahidi kuificha japo mpnz wangu aligundua kabisa kuwa nimechukia!

Tukawaambia hiyo mil. 4 tunaenda kuitafuta, mzee akasema "mkaitafute muilete hapa, au mutanitumia kwenye simu" tukawaambia sawa.

Muda wa kutoka nikakuta mpnz wangu ameshabeba mabegi anataka tuondoke wote, nikamwambia hapana unapswa kubaki nitakuja kuwachukua nikimalizia mahari, akagoma akawa analia wakati wote akiwa amenikumbatia, anaomba radhi kwa kilichotokea ila anaomba tuondoke wote, yeye hawezi kubaki Kijijini tena, nikamwambia hapana, unapswa kubaki mpaka tumalizane n'a mzee, akagoma kata kata, akawa amepiga magoti huku amekumbatia miguu yangu,machozi yanamtoka tuuu

Mzee wake alipotoka akaona mwanaye analia akasema "kama mnaobdoka wote nendeni tu" Mara mama mkwe akaja na dogo (mtoto wangu) akamshusha nilipokuwa, nikambeba mtoto nikamwambia mama mtoto asimame, bro na mshenga wetu wakaniita pembeni, mshenga akasema tuondoke nao, tukimuacha na wakahisi kuwa Kuna dalili za sisi kutorudi, watamuua huyu mtoto.

Basi kiahingo upande, tukawakubalia kuondoka nao, mama mkwe akaleta maharage na jogoo akataka tuondoke navyo, nikakataa kuchukua, nikamwambia tutabeba wakati mwingine, akagundua bado nina hasira, akamuita mtoto wake, akamwambia "mwambie mumeo amsamehe bure baba yako, amekosea sana, n'a mimi mama naomba atusamehe tu)

Tukaondoka zetu, kichwani nikiwa nimejaa mawazo mengi mnoo, kiasi kwamba sikuweza kujua niamue nini, tumefika Dar lakini moyoni nimejikuta sina tena interest ya kutengeneza undugu na familia ya mpnz wangu, japo yeye binafsi hana shida, lakini kwa namna tulivyopokelewa na tulivyoondoka, nilijisemea moyoni kwamba SITOKAA NIRUDI KIGOMA, WALA SITOKAA NIPELEKE HIYO MAHARI WALIYOSEMA, nasubiri mwanangu akue kue kidogo nimwambie mama mtoto kwamba hakuna namna naweza kuunganisha undugu na familia yake, japo namhurumia ila ndiyo hivyo tena!

Kweli tembea uone, all the way from Dar to Kigoma, naenda kukutana na aibu tu, anyway!
Pole sana. Ila huyo mwanamke usimuache, huyo ndie chaguo lako. Narudia tena usimuache, huyo ni mke mwema kabisa kwako. Mambo ya baba mkwe achana nayo, hayo yanatokea tu kila sehemu. Mshukuru MUNGU sana huyo mwanamke anakupenda na anaupendo wa kweli.

Iliwahi tokea Kwa mdogo wangu alikuwa anaowa Mwanza, siku ya Mahali tulikutana na kizingiti kikubwa sana, ila mjomba wake na Binti alisawazisha mambo na kuwaambia maisha yanaendelea na yanaendelea l, hivyo Mahali aliyonayo atoe, tukatoa 1.4 million badalaa ya 4 million. Na mchakato ulikuwa mgumu sana na tulitoka mbali (Iringa).

NEEMA YA BWANA WETU YESU KRISTO NA UPENDO WA MUNGU BABA NA USHIRIKA WA ROHO MTAKATIFU ZIWASHUKIE NA KUKAA NANYI DAIMA.
 
Waende wazee kutoka Dar mpaka Kigoma halafu ndo niende mimi tena?why???
Karma haijawahi kumuacha mtu salama mkuu...!

Kumuacha mke kwa makosa ya mzazi wake...na kumsababishia maumivu...hiyo karma itakuandama popote uendako....

kwa maumivu utayokuwa umemsababishia.....

If you truly love her...... embrace her...

Pesa zinatafutwa chief.....Lakini kutafuta na kumpata mtu mnaependana kwa dhati.....!
Hilo ni jambo jingine kabisaa!....

Pia....Kwa ninavyofahamu.....Mahari inaweza kulipwa kwa awamu.

Hata marehemu baba enzi za uhai wake....aliwahi niambia kuwa bado ana deni la mahali kwa mama yangu....

Kikubwa ni malipo ya awali tu...maana vingine umeshatekeleza.

The Choice is Yours....!Akili kumkichwa
 
Siungekufaa ukija Kwa sisi wamasai na umemzalisha mtoto wao bila kuoa naungepigwa mpaka usirudi Tena .

1.kwa ambaye ni bikra hajasoma ni ng'ombe 25 ambapo ukipiga mahesabu ya haraka ni ml 25
Kama ulimzalish ni ml 6 fine so 31ml .

2. Sasa awe na elimu na ni bikra huwezi mchukua kabisa kama sio ml 60 unaitoa Kwa macho

3.kama ameshatenguliwa na unamwona na anaelimu ni ml 15 bila chenga kama umemzalisha basi utaongeza kumi 5ml mahari na 5ml fine .

So hiyo 4.5 ni ndogo hapo hujatoa madebe 6 ya pombe ml 1 kujitambulisha
Umetoka ukoo gani na umekuja kufanya Nini
Hzo faini lengo lake ni nn hasa...👣
 
Siku moja nilienda shambani kwangu nikakuta kijana wangu wa shamba mkewe hayupo, nikamuuliza vipi mbona uko pekeyako? Akanijibu we acha tu…. Akasema wajomba wa mkewe wamekuja kundi la watu kumfuata mtoto wao (huyo mkewe)

Nikamuuliza kwahiyo wamesemaje? Akajibu wameniambia niende nikalipie utamu la sivyo mke harudi. 😂

Enzi hizo mimi naishi bila ndoa natoa tu utamu bure bure, nikajisemea kumbe I’m selling myself short. 🤣 anyways masuala ya mahari huko vijijini ni very big deal.
 
Ngoja niweke busara za kupaka rangi maneno na kuyelemba kando. Nikupe busara za kiutawala na ubabe.

Hapo hakuna ishu ya mzee kuwa na hasira wala nini, hapo ni Game ya Utawala. Mzee karusha kete zake, ukiingia huo mtego wake, atakubulizaa hasaaa. Busara zake zero, mtu kaonyesha unyenyekevu kutoka alipo unaishia kufoka na kusema hakuna mjadala .

Wewe huna majukumu ya ku solve matatizo yake, kiuchumi, au kijamiii, inafanywa kwa upendo na ushirikiano, sio jukumu lako ku show up ktk majanga yao, wewe yako wanaweza kuyashiriki?.

Msaada wowote ukweni ,sio jukumu lako, ni yeye na kete zake za ujanani hadi uzeen au watoto wake wafanye hayo, ishu sijui hujaenda kutoa pole sijui nn, hoja za kitoto.

Hawezi kukutreat kama muharifu, hukubaka mwanae, ni maelewano na alikuja kwa ridhaa yake yeye. Hakuna jeuri uliyofanya. Je, alitaka before kukaa na mwanae au kulala naye ungetuma barua ya maridhiano,?.

Ukiangukia ktk huu mtego,jiandae kuja kubuluzwa ktk maamuzi hata familia yako. Utapewa majukumu ya ukoo au mashemej, utasikia tu, shemej yako anakuja mpokeen hiyo ni final.

Chekecha akili, simika dominance yako hapo, yeye kasusa, hajasusa ni ego tu ya hao watu viburi tu,wabishi sanaaa. Vungaaa cheza na akili yake like u don't care.

Harafu usitishwe na sijui uchawi na nini, angekuwa na uwezo na kila kitu , asingekuwa bush huko,asingekuwa na mawenge aliyo nayo. Usitukuze uchawi wala kuhusudu ishu zao. Ogopa MUNGU pekeeeee, weee kaa vizuri na MUNGU, hakuna boya wa kuchukua uhai wa familia yako.

Damu nzito kuliko maji, unaambiw tu ,et kama mama mkwe yuko poa sijuii nini, oyaaa huyo ni mumewe hawez kumsaliti over you, kuhusu binti sijuii wewe wamjua vyemaa.

Tafuta ushauri wa kiroho ,uone ktk lipi utakuwa safe zaidiiii, wanawake wapoo tu, kama vipi anza life lako, watakuja wenyeweee. La msingi timiza jukumu lako lea mtoto wako, tuma matumizi, then mengin waachie wao. Ukiulizwa waambie sina Milion 4, niliyo nayo nimewapa yote. Kuna maisha nje ya ndoa na mapenzi.
 
Sasa akiachika halafu akaja hapa JF kutafta mume si mtaanza ooh tuonyeshe kabuli la mume wako, mala ooh kwanini uliachika mala single mother sijui laana. Yaani humu ndani JF hakuna jema wakat mungine. Na niliwahi kusema kabla hujamhukumu single mother chunguza kwanza Nani kapelekea kua single mothers.


NB:
Mkataba
Waarabu
Bandali
Miaka 100

Mbowe na lisu wanatucheleweshea sana maendeleo ya hii nchi
Sio wote wanakuwa single mother kwa scenario Kama hiyo
 
Kwa hiyo baada ya kuzaa nilitakiwa kutokomea siyo?
ukitokomea ni hasara yako mwenyewe,maana ukimtelekeza toto linakuwa tajili la kutisha afu baba mtu unakuwa na maisha ya digidigi una baki kulia lia kwenye media eti mwanao hakujali, mi ni muha .ki kwetu nikosa kumzalisha mwanamke kabla ya kumuoa kwani ina hesabika ni dharau kwa familia ile
 
Kwa hiyo kwa mtazamo wako sisi kutoka Dar mpaka Kigoma kwenda kuyajenga tulikuwa wapumbavu?
Ilikuwa busara kuona dhamira yetu na kuwa muungwana, ila kwa réaction aliyoonyesha atabaki n'a mtoto wake tu, siwezi kuwa n'a baba mkwe wa aina yake

Unasemaje atabaki na mtoto wake ilhali uliondoka naye na upo naye.!

Kama una akili timamu ungeshajua kuwa imeisha hiyo, mzee hataki tu kukuchekea ila mkeo hapo hatoki…. ulishindwa kumwacha kwao siku hiyo huwezi kumtimua.
 
Kweli mkuu jamaa walimfanyia makusudi kama kumkomoa kwa kuchelewa kujitambulisha ukweni na kama angeweza kuwa nao karibu kipindi cha nyuma hyo mahari isingefika gharama hzo tatizo lililokuwepo yeye kutojitambulisha mapema na kuzalisha mtoto wao pasipo yeye kufahamika ukweni wamefanya kwa kumkomesha tuu
 
Back
Top Bottom