Pole sana Mkuu, tambua ya kuwa haupo mwenyewe katika hali hiyo. Wapo wengi sana wasio tena la tumaini la kutimiza ndoto zao baada ya hali kubadilika.
Cha msingi usikate tamaa, fight to the last drop. Kama hutafanikiwa mwaka huu, amini utafanikiwa kwa kipindi kinachofata. Pigana Mkuu, kama hali bado itakuwa tete omba usaidizi kutoka kwa ndugu zako japo najua ugumu wake ama hairisha mwaka mpaka pale hali ya anayekuwezesha itakapotengamaa.
Muombe sana Mungu huku ukipambana naye hatakuacha. Mpe pole mzazi na augue vema na apate nafuu mapema.