Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,138
Tangu kuzaliwa kwangu,zaidi ya miaka 30 iliyopita, sijawahi kuwa na chama cha siasa. Ingawa nimekuwa mfuatiliaji wa siasa tangu shuleni na chuoni,sijawahi kuwa na kadi ya chama chochote cha kisiasa. Sababu ni moja:sikuwa nimejiandaa kuwa katika harakati za kisiasa. Lakini sasa ni tofauti.Natamani kuwa na chama na kuwa mwanasiasa.
Ndiyo maana nilijipa muda wa kusoma Katiba,Kanuni,Ilani na Sera za vyama mbalimbali hapa nchini ili nichague chama cha kujiunga nacho. Kwa weledi wangu wa sheria,nimesoma kwa makini na kuelewa ipasavyo. Pia,nimehudhuria mikutano ya vyama tofauti hapa nchini ili kusikia kauli na hotuba zao. Kuna chama kimenivutia.
Hicho chama kina Katiba nzuri;Kanuni zilizo wazi;Ilani inayolenga mema kwa watanzania; na wanachama wanaokipenda chama chao bila kificho. Ni chama kinachoamua kikaamua;kusema kikasema;na kupanga kikapanga.Kimenivutia sana. Nami najiandaa,hata kama hakutakuwa na viongozi wa kitaifa na vyombo vya habari,kujiunga nacho.
Nikishajiunga, weledi wangu wa sheria nitautumia kukiimarisha chama na kukitangaza. Kukifanya chama kiimarike zaidi na kuaminiwa.Chama nitakiheshimu na kukilinda-chama na wanachama wake. Nitaanza na heshima na kumaliza na shukrani. Najua nitaaminika. Kama uongozi hata mimi nimewahi kushika shuleni,chuoni na Taasisi ya Mafunzo ya Sheria kwa Vitendo(Law School of Tanzania).Uongozi una miiko yake,mipaka yake na taratibu zake kuupata. Nikiutaka,nitazingatia hayo kwanza.
Kiukweli kabisa, chama hiki nakiona kama chama chenye dira na makini.Kinalenga watu wa aina na madaraja yote. Ni mdomo wa kila mtanzania. Nakaribia kujiunga na chama hiki. Taratibu za kuletewa kadi hata sehemu yangu ya kazi au nyumbani zinaendelea. Sibaki tena nyuma. Najiunga na wenzangu. Kwa ajili ya nchi yetu.
Nitajiunga kabla ya kuisha kwa mwaka huu. Waungwana,mtajua hapahapa chama nilichokichagua. Nadhani nitaungwa mkono kwa uchaguzi wangu na wengi wenu.
Asanteni kwa sasa!
Ndiyo maana nilijipa muda wa kusoma Katiba,Kanuni,Ilani na Sera za vyama mbalimbali hapa nchini ili nichague chama cha kujiunga nacho. Kwa weledi wangu wa sheria,nimesoma kwa makini na kuelewa ipasavyo. Pia,nimehudhuria mikutano ya vyama tofauti hapa nchini ili kusikia kauli na hotuba zao. Kuna chama kimenivutia.
Hicho chama kina Katiba nzuri;Kanuni zilizo wazi;Ilani inayolenga mema kwa watanzania; na wanachama wanaokipenda chama chao bila kificho. Ni chama kinachoamua kikaamua;kusema kikasema;na kupanga kikapanga.Kimenivutia sana. Nami najiandaa,hata kama hakutakuwa na viongozi wa kitaifa na vyombo vya habari,kujiunga nacho.
Nikishajiunga, weledi wangu wa sheria nitautumia kukiimarisha chama na kukitangaza. Kukifanya chama kiimarike zaidi na kuaminiwa.Chama nitakiheshimu na kukilinda-chama na wanachama wake. Nitaanza na heshima na kumaliza na shukrani. Najua nitaaminika. Kama uongozi hata mimi nimewahi kushika shuleni,chuoni na Taasisi ya Mafunzo ya Sheria kwa Vitendo(Law School of Tanzania).Uongozi una miiko yake,mipaka yake na taratibu zake kuupata. Nikiutaka,nitazingatia hayo kwanza.
Kiukweli kabisa, chama hiki nakiona kama chama chenye dira na makini.Kinalenga watu wa aina na madaraja yote. Ni mdomo wa kila mtanzania. Nakaribia kujiunga na chama hiki. Taratibu za kuletewa kadi hata sehemu yangu ya kazi au nyumbani zinaendelea. Sibaki tena nyuma. Najiunga na wenzangu. Kwa ajili ya nchi yetu.
Nitajiunga kabla ya kuisha kwa mwaka huu. Waungwana,mtajua hapahapa chama nilichokichagua. Nadhani nitaungwa mkono kwa uchaguzi wangu na wengi wenu.
Asanteni kwa sasa!