Doh hili balaa.
Kuna mdada niko nae kwa ofisi. alikua anaonyesha dalili zote za kuvutiwa
nami, Ikiwemo mitego mbalimbali Nami nikavutika na tayari taratiibu
moyoni akachukua nafasi. Kutokana na utamaduni wetu wa kitanzania
niliamini kua kwa dalili hizi anasubiria tu mimi ndio nitamke kua
namzimika.
Sasa last week nikaona nianze kumtongoza kupitia simu yake ya mkononi.
Halahaulaa kumbe ni mchepuko wa bosi mkubwa. Nasikia hata kazi yenyewe
ndo kampachika yeye. Si akamwonesha hizo meseji za mahabaati!
Bosi akanichimba biti. Mbaya zaidi kila mtu hapa ofisini amefahamu.
Yaani maisha yamekua magumu kwa kweli.
Kila nikijaribu kujikaza lakini wapi.