Nimekata tamaa sana nakufikia kuona kifo ndio suluhisho

Nimekata tamaa sana nakufikia kuona kifo ndio suluhisho

Abti

Senior Member
Joined
Feb 27, 2025
Posts
101
Reaction score
182
Mimi sio mjuzi wakuandika uzi JF hii ndo mara yangu ya kwanza na inaweza kuwa ya mwisho kama kuna makosa jitahidini kuelewa.

Niende moja kwa moja kwenye mada, nahisi leo inaweza kuwa siku yangu ya mwisho kwenye huu uso wa dunia ila nitakuua nimeacha maumivu makubwa sana kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki.

Najua nina makosa mengi sana nitakuwa nimefanya niliowakosea naomba radhi mnisamehe kwa dhati na mniombee kwenye safari yangu.

Kosa langu kubwa ni kushindwa kuelezea mambo nayopitia, kiukweli nimeshajaribu kujitoa uhai zaidi ya mara nne lakini ikashindikana na kuona Mungu ana kusudio na mimi ila bado kwa upande wangu nimeshindwa kukaa sawa mpaka nahisi kuwa nina shida ya akili ama kuna kitu kingine

Sijui napoenda kama kuna mapumziko ya kweli ama laa, umri bado ni mdogo miaka 29 naingia ila sina uelekeo wala utulivu wa akili kutokana na wakati mgumu naopitia akili mwangu na moyoni mwangu.

Nimeona hata ikitokea nimeondoka kwenye hii dunia niache uzi huu nikiondoka nitakuwa nimeacha binti yangu mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi minne aliyeanza kuita baba na mama tu atakuta historia ya baba yake kwa namna tofauti kwamba hakua jasiri ama kifo kilimshinda.

Ndugu jamaa na marafiki binti huyu ni dhamana yenu nawaomba uangalizi wenu kwake akiwa mdogo na hata akikua.

Watu wa mzaha nitaona ni kawaida hii ila mwisho mtakuta habari tu yalioadikwa yametimia japo namuomba Mungu anitie nguvu kuniepusha na hili tendo nawapenda sana wote.

Kama kuna mtu amebarikiwa kunipa ushauri utakaogeuza mawazo yangu nipo hapa kwa masaa machache kupokea jitihada zako.

Asanteni sana DEPRESSION IS REAL.
 
Mara 4!, ya 5,utafaulu, but never gives up as real man. (unapimwa tu ujasiri)
Omba kazi hata za ulinzi, aidha jiingize kwenye bodaboda, Hawa bodaboda ndio matajiri wa kitaa siku hizi, (wanakula wake za wakubwa)
You are born a man, you must act like man, and that's g_d will.
 
Kama kuna mtu amebarikiwa kunipa ushauri utakaogeuza mawazo yangu nipo hapa kwa masaa machache kupokea jitihada zako.

Asanteni sana DEPRESSION IS REAL.
Miaka ya babu zetu hakukuwa na huu Usenge wa Depression, wewe una tatizo la Afya ya akili. WAHI HOSPITAL.

USHAURI AU NENO LA MWISHO KWA MAREHEMU MTARAJIWA.
Dogo wewe ni Mwanaume, japo ninafikiri 88% umelelewa na Mama pekee(kanusha hili). Kwenye maisha kama mtoto wa kiume hupaswi kuwa laini laini. Matatizo ni sehemu ya maisha ili uweze kukua na kufikia malengo yako.

Changamoto pekee inayoweza mkuta mwanaume akaishindwa ni ile inayohusisha AFYA. Lolote tofauti na afya huwa linatatulika chini ya jua. Unapaswa kukubali, kulipokea na kupambana kutatua na sio kulia lia upuuzi.

Maelezo yako yanaonyesha ni mtu wa lawama na kulia lia sana kupenda kuonewa huruma, wewe ndio wale wa "Mjomba hanisaidii", "Shemeji ana hela ila hanijali". Acha kukata tamaa kijinga ilihali tayari una mtoto umemleta Duniani. Unafikiri ukiondoka ni nani atamlea, na kwanini utuletee sisi mtoto wakati ulijua utajiua, Dunia ilivyoharibika unataka wahuni wamshenyente?. KAMA SIO USENGE NI NINI? - Nape nnauye.

Usimletee Binti yako upuuzi ukamkimbia, Magumu huyapitii peke yako na hakuna ambaye hajatoka mbali.

Be a Man, embrace challenge.
 
Mkuu, pole sana naomba kabla hujachukua huo uamuzi mfikirie mtoto mdogo aliye anza kuita baba. Kujiua siyo kutatua tatizo bali ni kuongeza tatizo kwa wanao baki hasa mtoto.
Jikaze na vumilia kwa sababu kila jaribu lina mlango wa kutokea.
 
Kuna jamaa alileta uzi humu akielezea magumu anayopitia na dhamira yake ya kujipokonya haki ya kuishi, baada ya siku chache, akajitangazia umauti Kwa ID nyingine akaanza kujipigia rambirambi kama DR Steve ake..Kuna mahala alijichanganya na modes walivyofatilia huko kibaha wakagundua ni muhuni mmoja na hakuna msiba, akala BAN na maombolezo na rambirambi zikaishia hapo.
 
Mkuu,
Maisha hayajawahi kuwa mepesi, hata hawa unaowaona barabarani wana yao mengi sana, kila mtu anapitia jambo fulani katika maisha. Ni kosa/dhambi kubwa kukata tamaa ya kuishi, muhimu sana kupambana, kutatua changamoto na kuzishinda. Huo ndio uanaume, unqchofanya hapo ni kushindwa kuwa mwanaume, be a man, pambana.
 
Mimi sio mjuzi wakuandika uzi JF hii ndo mara yangu ya kwanza na inaweza kuwa ya mwisho kama kuna makosa jitahidini kuelewa.

Niende moja kwa moja kwenye mada, nahisi leo inaweza kuwa siku yangu ya mwisho kwenye huu uso wa dunia ila nitakuua nimeacha maumivu makubwa sana kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki.

Najua nina makosa mengi sana nitakuwa nimefanya niliowakosea naomba radhi mnisamehe kwa dhati na mniombee kwenye safari yangu.

Kosa langu kubwa ni kushindwa kuelezea mambo nayopitia, kiukweli nimeshajaribu kujitoa uhai zaidi ya mara nne lakini ikashindikana na kuona Mungu ana kusudio na mimi ila bado kwa upande wangu nimeshindwa kukaa sawa mpaka nahisi kuwa nina shida ya akili ama kuna kitu kingine

Sijui napoenda kama kuna mapumziko ya kweli ama laa, umri bado ni mdogo miaka 29 naingia ila sina uelekeo wala utulivu wa akili kutokana na wakati mgumu naopitia akili mwangu na moyoni mwangu.

Nimeona hata ikitokea nimeondoka kwenye hii dunia niache uzi huu nikiondoka nitakuwa nimeacha binti yangu mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi minne aliyeanza kuita baba na mama tu atakuta historia ya baba yake kwa namna tofauti kwamba hakua jasiri ama kifo kilimshinda.

Ndugu jamaa na marafiki binti huyu ni dhamana yenu nawaomba uangalizi wenu kwake akiwa mdogo na hata akikua.

Watu wa mzaha nitaona ni kawaida hii ila mwisho mtakuta habari tu yalioadikwa yametimia japo namuomba Mungu anitie nguvu kuniepusha na hili tendo nawapenda sana wote.

Kama kuna mtu amebarikiwa kunipa ushauri utakaogeuza mawazo yangu nipo hapa kwa masaa machache kupokea jitihada zako.

Asanteni sana DEPRESSION IS REAL.
Usijiue mkuu jipe muda kaka inshallah mambo yatakuwa safi
 
Back
Top Bottom