Heshima kwenu wakuu,
Me Mtanzania mwenzenu nimepatwa na janga la aina yake! Kwa hapa nilipo, nipo nje ya nchi, wakati naondoka nilimwacha wife nyumbani, baada ya kukaa kdg kwa kua wife ni mjamzito alienda nyumbani kwetu. Pale home kulibaki mama mwenye nyumba na wapangaji wenzangu, so week tatu sasa yapita wezi waliingia wakabeba vitu kama Radio, Tv, Home theater n.k. ila basi wapangaji wenzangu wakampa taarifa wife na wife akanijuza mimi.
Sasa cha ajabu ni nini, nimepigiwa simu leo wife anadai ATM Cards hazioni pale tuwekapo na zoote ni zangu mie. Nipo nimeshindwa nifanyaje kwani nahis ziliibwa pia, naogopa kama n nitakuta hamna kitu kwenye akaunti zangu na wakati huu mgumu.
Nisaidieni nifanyaje jamani
Hvi mtu anaweza kuchukua fedha kwa ATM bila kujua No yako ya Siri? Manake me no yangu ya Siri hata ujaribu Mara 100 huwezi patia.
Feedback
Wakuu nashukuru sana kwa maoni yenu na mashauri nilifika jana na nilipitia bank NBC nikawapa taarifa baada ya mda kidogo zikaletwa card zile zinazo mezwa na Atm na yangu ikitolewa maelezo kwamba alikuja mdada wa kati ya miaka 28 to 30 alikua anataka kutoa pesa kwa cachier lakini alikataliwa na baada ya siku mbili alikuja tena kijana wa kati ya miaka 16 to 20 lakini alipofika kwa cashier alijieleza kama ametumwa na mwenye card lakini wafanyakazi wakamtilia shaka na kumuuliza kwanini hakuenda kutolea kwa Atm mashine? Akasema amesahau password wakamwambia aende kumwita mwenye card basi kijana mpaka kesho hakuwahi kuonekana
kwa ile ya crdb mpaka sasa ipo kwenye taratibu ya kunitengezea mpya na masalio yapo salama asanteni