Kwa wanaojua njia zaidi ya kutunza siri nahitaji mawazo ili niweze kuwa mtunza siri mzuri..:embarrassed:
Habari zenu wana jamii, poleni na majukumu.
Kuna kitu kinanitatiza ni bora mnisaidie mawazo niwe na amani. Binafsi nina kanuni zangu flani za maisha, na kuna baadhi ya mambo ambayo ni binafsi sana napenda yawe ni siri ya moyo.
Sasa kilichotokea ni kwamba nilijikuta nikimwambia mtu wangu mmoja wa karibu siri yangu ambayo hua sipendelei baadhi ya watu wajue. Nilipomueleza niliumia sana nikasema ni mistake imetokea nitajitahidi nizibe mdomo.
Sasa hii mara ya pili nimejikuta nikimuelezea mtu mwingine siri nyingine tena sio ile ya kwanza, nimeumia sana lakini ndo imeshatokea sasa sijui nifanyaje.
Maana ni mambo binafsi sana sipati picha akiamua kushea na watu wengine japo sio mabaya lakini ndo hivo sipendi yafahamike. Siri nimeshindwa kutunza sasa najihisi vibaya.
Kwa wanaojua njia zaidi ya kutunza siri nahitaji mawazo ili niweze kuwa mtunza siri mzuri..:embarrassed:
Hazikuwa siri, believe me siri huwa hazitamkiki, hata kuiwaza tu unaona kama unasomwa mind
Chukua kijembe, toka nje ya nyumba yako, chimba kijishimo kidogo, taja siri zako zote humo ndani ya kishimo, halafu fukia...
hahaha pakiota mti hapo siri zitasambaa kama za yule mfalme mwenye masikio marefu kama ya punda
Pole, inategemeana Kuna wakati mwingine vitu vingine unaweza kufikiri kuwa ni siri kumbe unahitaji ku share,Kuna Tofauti ya Neno siri kati ya mtu na mtu, Kuna kitu unaweza kuona kuwa ni siri kwako lakini kwa mwinginee sio siri,Lakini lazima uwe na mtu ambaye anaweza kubeba mambo yako na uwe na uhakika naye!. Mfano mimi Kuna vitu nashare na Mke wangu tu, vingine rafiki tu. Ndugu? Kwa ndugu ni vitu vya kindugu mara nyingi hata nikigombana na mke wangu sitaki ndugu wajue.
Chukua kijembe, toka nje ya nyumba yako, chimba kijishimo kidogo, taja siri zako zote humo ndani ya kishimo, halafu fukia...