Hute
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,537
- 6,458
WAJAMENI, nimefanikiwa kuandika kitabu kizuri sana, viwili actually, na lengo langu ni kuvitoa vitabu hivyo ili niviuze. mambo niliyoandika ni marketable sana hapa tz tena nimeandika kwa kiswahili kiasi kwamba kila mtu akikiona atakinunua bila shaka. tatizo langu ni kwamba, sijawahi fanya hivi, naombeni kujua kwa wale mlionitangulia kuandika vitabu, au wenye knowledge yeyote kuhusiana na hili.
NB; sijataja nimeandika kitabu cha aina gani, najua nikitaja tu, watu wengine watatoa kitabu kama hicho hata kabla changu hakijatoka....nafikiri huu ni ulimwengu wa ushindani.
- sina pesa kulipia publishing, kuna kampuni yeyote inaweza kuingia mkataba nayo?
- hata kama nikijipinda nikapata milioni kadhaa kama tatu hivi, je? ma distributor wepi wazoefu/wazuri wanaofahamika ambao naweza kufanya nao kazi kunisambazia kitabu changu tz nzimba? au how does the distribution thing work?
NB; sijataja nimeandika kitabu cha aina gani, najua nikitaja tu, watu wengine watatoa kitabu kama hicho hata kabla changu hakijatoka....nafikiri huu ni ulimwengu wa ushindani.