Nilimwalika Sheikh aje anifanyie dua mahali pangu pa biashara, wakasema naroga biashara zao. Leo kila mtu anamwaga maji na mafuta kwenye frem

Nilimwalika Sheikh aje anifanyie dua mahali pangu pa biashara, wakasema naroga biashara zao. Leo kila mtu anamwaga maji na mafuta kwenye frem

KING MIDAS

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2010
Posts
10,569
Reaction score
21,075
Nikipomleta Sheikh anifanyie dua kwenye biashara yangu, watu wote wakanichukia na kuanza.kusema Mimi ni mchawi.

Kuanzia siku hiyo kila MTU anamwaga maji na mafuta kwenye frem yake kama wamepagawa, wengine wanaongea maneno hayaeleweki, wengine wanaimba, wengine wananong'ona, mie niko zangu kimyaaaaaaa, najiokotea mbilimbili zangu kwa raha zangu.
 
ulifanya vyema, japo bandiko lako limeegama upande kwamba hapo hawapo wa dini yako ni wewe tu walio baki ni wa imani ya maji na mafuta

ivi dua kama albadiri sio uchawi kweli ule
 
hakuna mungu, hakuna uchawi....ni UPUMBAVU tu wa watu,....
Ila peponi kupo na unapewa mabikira 72 uwahudumie peke yako. Usitamani kabisa starehe zetu za peponi.

Tena kuna mito ya pombe tamu, nzuri sana. Na upo MTO wa maziwa.

Kuna chemchem zitoa supu ya kila aina uipendayo
 
Halafu wachungaji wanategua na kuuharibu uganga wa mashehe?
Hao wenzako hawataweza kukuamini tena kutokana na huyo sheikh wako ingawa wewe unasema ilikuwa unafanya dua lkn wenzio wanaamini wewe ni mchawi...
Hilo lipo wazi hao masheikh ni watu hatari usifikiri hao wenzio watakuchekea Tu... Kama mufti wenu mkuu bado mpaka Leo ni mganga ni Nani anaweza kuwaamini?
 
Nikipomleta Sheikh anifanyie dua kwenye biashara yangu, watu wote wakanichukia na kuanza.kusema Mimi ni mchawi.

Kuanzia siku hiyo kila MTU anamwaga maji na mafuta kwenye frem yake kama wamepagawa, wengine wanaongea maneno hayaeleweki, wengine wanaimba, wengine wananong'ona, mie niko zangu kimyaaaaaaa, najiokotea mbilimbili zangu kwa raha zangu.
Wakristo tuna mtazamo mbaya kuhusu Uislamu. Hapa mtaani kuna duka la jamaa fulani ustadh. Jamaa ni mtu poa sana sana. asubuhi akifungua huwa anawasha ubani nadhani anakuwa anasoma dua. hata ukimwongelesha hajibu au atakupa ishara kuwa usubiri kidogo. Wanazengo sasa wanasemaga anaroga eti ukizingatia ni muha wa kigoma.
Shida kubwa ya Wakristo huwa tuna uelewa finyu kuhusiana na Uislamu na mengi tunayoongea huwa ni story tu za kusadikika wakati wenzetu ni kinyume chake.
Mimi niko comfortable sana kuhusu Waislamu kwa sababu toka nasoma asilimia 90 ya rafiki zangu walikuwa Wasilamu kiasi kwamba hadi mzee alihisi nitaslimu so hizo story za majini sijui nini mimi kwangu naona kama wanaosema wananichekesha tu.
by the way sipendi harufu ya ubani na udi kabisa.
 
Katika uislam kila mtu ana wajibu wa kuomba dua yeye mwenyewe kumuomba Mungu kile anachohitaji, kuhusiana na biashara zako ilikua hamna haja ya kumpeleka sheikh akuombee dua, wewe unatakiwa ujiombee mwenyewe
 
Back
Top Bottom