Nilichogundua kwa siku ya leo

Nilichogundua kwa siku ya leo

Hahahah!!!

Mkuu uwepo wa mafuriko si suluhisho la foleni barabarani, mwarubaini wa foleni ni kuongeza tu idadi ya barabara na kuboresha zilizopo...pia kupunguza utegemezi wa eneo moja kuwa ndio kitovu cha shughuli za kiofisi au kibiashara.
ni kweli, suluhisho la haya matatizo ni kuboresha miundombinu yetu....
 
Kumbe chanzo cha foleni morogoro road ni malory

Yanatakiwa kuwa na njia zake za kupita, siyo kuchanganyikana na magari madogo na public transport kwa sehemu za mijini, hii hali iliyopo ya kuchanganyikana ilitakiwa iwe nje ya maeneo ya jijini yaani barabara za masafa marefu
 
Kuna siku Dar es salaam itabaki kama kisiwa. Hebu fikiria kama Morogoro road, Bagamoyo road na Mbagala zikifungwa tutatokea wapi?
una apply mode nyingine ya usafiri,fast jet to mby then unarud kwa basi km ni iringa or moro,k'njaro then unarud kwa basi km km ni moshi arusha,tanga nk na mwz or shy,then unarud kwa basi tbr,singida dom nk.
note:
1.mvua zinazoendelea nchi nzima ziwe hazijabomoa madaraja mengine huko upcountries.
2.muda wa safari utaongezeka na nauli itaongezeka.
 
Kuna siku Dar es salaam itabaki kama kisiwa. Hebu fikiria kama Morogoro road, Bagamoyo road na Mbagala zikifungwa tutatokea wapi?

Tutatokea Julius Nyerere International Airport
 
Mkuu kwa leo Mbezi Mwisho hadi Posta ukiwa na private car unatumia dakika 30 hadi 40 wakati siku nyingine huwa ni dakika 90 hivi.

Ni kweli sababu ni hiyo ya kutokuwepo kwa malori yanayoingia jijini, kwa kawaida kuanzia alfajiri ya saa 11 msururu wa malori huwa unaanza kujilimbikiza pale Kimara Mwisho na kadiri muda unavyojongea foleni nayo hukua taratibu na baadaye huamia Ubungo.

hii hali iendelee waonaje...? ndio maana huku kwetu njia panda segerea haina magari yatokeayo huko...

Hii hali ya mafuriko isiendelee ila serikali ijifunze kitu kuona jinsi ya kukabiliana na changamoto za foleni kwa kutumia hii model ya sasa hivi. Namaanisha kuona mchango wa uwepo wa malori kwenye suala zima la foleni. Unajua wakati mwingine matatizo yanakuja kukufumbua macho na kukufanya ufikirie kwa mtazamo tofauti.
 
Back
Top Bottom