Nifanyeje?

Acuity

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2013
Posts
391
Reaction score
118
Heshima kwenu wadau,

Mwaka 1990 marehemu baba yangu aliamua kuoa mke wa pili. Miaka mitatu baadaye (1993) yule mke wa pili akafanikiwa kumhamisha kimapenzi baba yangu, akaamua kuondoka kabisa pale nyumbani. Mimi na wadogo zangu tumeishi maisha ya kutokumwona baba akitoa huduma yoyote kwetu toka wakati huo hadi kifo kilipomfika yeye na mkewe huyo wa pili mwaka 2011 kwa kukatwakatwa na majambazi kwa madai kwamba ni wachawi. Wameacha watoto watano. Mimi ndiye kijana pekee wa kiume mkubwa na ambaye ndiye pekee mwenye elimu ya Chuo Kikuu na uwezo kidogo kifedha. Mama yetu mzazi bado yupo hai. Toka 2011 ndugu zangu walitamani sana tuwatelekeze wale watoto wa yule mama wa kambo. Mimi nilikopa roho ya simba, nikaingilia kati. Nilimjengea nyumba mama yetu mzazi (70 yrs) na hao watoto walioachwa. Wanaishi pamoja japo kwa taabu sana. Kwenye uzao wa mama yetu mzazi sote ni watu wazima. Hakuna hata mmoja anayeishi karibu na mzazi wetu huyo. Tumemwekea mfanyakazi wa ndani kumsaidia huku hao watoto wote bado wanasoma.

Leo kinachonisukuma kuja kuomba msaada wa mawazo hapa ni: kila siku hao watoto wamekuwa wasumbufu kwa mama yetu. Wanamtukana, wanamsema vibaya na hata kumsingizia kuwa ndiye aliwaua wazazi wao. Kila msichana ninayempeleka pale, wanamtukana hadi anatoroka. Hivi ninavyoongea mama yangu anaishi bila msaidizi. Ninaumia kuona mama anapata shida. Ninaumia kuwaza kumwondoa pale mama maana tunaua mji wa urithi na watoto watakosa msaada. Ndugu zangu hawanielewi japo wananiheshimu kama mtoto wa kiume. Wnashauri niwatelekeze wale watoto kwa kumwondoa mama yetu. Nipo njia panda. Naomba ushauri wenu wadau.
 
Kama washajua matusi ina maana wameshakuwa.

Its time for them to leave ili mama nae apumue.

Mtoto mkubwa anasoma Diploma in Accountancy (namsomesha kwa kinguvunguvu maana ndugu zangu wote hawapendi). Huyu yupo chuoni. Wa pili amemaliza VETA (naye nililipa karo mpaka dadazangu wengine wamentenga), huyu ndio tatizo. He is 19 now. Wengine wawili wapo Sekondari Form 3 kitindamimba yupo Std 6. Huyo wa VETA ana walioko Sekondari wamekuwa mwiba sana kwa mama yangu. Lakini niwafanyeje??
 

shukrani ya punda hiyo .... achana nao...au waite ongea nao waeleze ukweli mother atasepa hapo ubaki na hivo vidubwasha visivyokuwa na shukrani huku ukikosa baraka za mama kwa kuwa kasha tangulia ...
 
rafiki pole, ndio maisha yakupaswa kusimama imara, kwa maana hao watoto wanapaswa kumuheshimu mama yao na sio vinginevyo, hayo unapaswa kuwaeleza ukiwa macho makavu kwani nyie mmekuwaje si kwa shida tupu....?
waeleze ukweli vinginevyo beba mama yako usepe nae....
 
Kama kuna mali marehemu Baba yako na huyo mama wa Kambo waliacha, fanya utaratibu wa Kisheria kwa kukamilisha taratibu zote za kufungua Kesi ya Mirathi na kugawa/kuwagawia urithi wao hata kama ni jembe la mkono. Kisha waite wanaukoo/Viongozi wa Kidini wakabidhi rasmi mara baada ya kuweka bayana uliyowatendea na wanayokutendea. Fungua ukurasa mwingine wa maisha vinginevyo watahisi misaada yako sio bure labda una urithi wao au uliwafanya wazazi wao misukule unavuta mpunga
 
Kwanza! Utambue hao watoto ni ndugu zenu wa damu kabisa!
...
Pili! Mtoto hakurupuki tu na kumrushia mkubwa wake matusi! (hapa simanishi huyo mama yenu matusi kayatafuta mwenyewe) namanisha watu wakiishi pamoja, hawatoacha kukwaruzana! Matusi ya watoto ni kwa sababu ya kutojitambua!
...
Busara na njia mzuri ya kutatua tatizo ni muhimu kuliko kuhitimisha kwa kuwatimua wadogo zako!
...
Suluhisho:
watenganishe mama na hao watoto!
Ongea na mama na umuombe kuwasamehe hao watoto!
Ongea na watoto kwa lugha mzuri na kuondoa chuki dhidi ya mama!
...
Aisee ukifanya hivyo Mungu atakubariki sana!
 

Ahsante kwa ushauri. Bahati mbaya au nzuri baba yetu alikuwa mkulima tu. Hata mifugo ilibaki miwili tu na kwa namna alivyokuwa hatujali sisi hao mifugo ni mali ya hao watoto, sisi hatukuambulia chochote maana alikwisha gawanya kabisa toka mwanzo wa matatizo. So aliacha shamba tu.
 
Mchukue mama uishi nae....afu sitisha huduma zote kwa hao watoto...kama wana uwezo wa kumtukana mama kiasi hicho basi wana uwezo wa kujipatia huduma zote muhimu.....na na huyo konikodi wa matusi ndo awahudumie wadogo zake.....mpaka akili itakapomkaa sawa na atakapojua umuhimu wako na huyo mama....
 

Mkuu nakushukuru. Japo naishi mbali huwa najitahidi sana kwenda nyumbani kusalimia. Kila nikienda huwa tunafanya vikao vya familia kupitia mambo yote hayo. Wazee mashuhuri marafiki zetu ninawaita ili watoe ushauri kwa hao watoto lakini ikipita wiki tu mambo yanaanza. Kwa ujumla nimejitahidi sana lakini sioni mafanikio. Unaweza kufanya ,azungumzo nao, mfano siku moja.....baada ya kuongea nao, wiki moja baadaye nilikuta barua ameandika mtoto mmoja akisema....nanukuu"wadogo zangu hapa tunapoishi ni kama ndege tu. Huyu kaka yetu anatusaidia lakini hatupendi. Tujihadhari naye" Kwakweli nilitaka kuchanganyikiwa kwa kusoma ujumbe ule!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…