Jamani wana MMU habari zenu,
Waungwana naomba ushauri wenu kwani mimi nimetokewa kupendwa na dada mmoja ambae anasomea nursing na atakua anahitimu mwezi wa sita na amekuwa akiambia anataka aolewe nami, pia anasema kuwa kwa hali yoyote ile lazima atafanya ili kuhakikisha namuoa, kiukweli hata mimi nampenda sana huyu mwanamke ila tatizo ni kwamba nina mke tayari ambae nimemuoa na tumebahatika kuwa mtoto mmoja wa kiume na bado nampenda mke wangu. Dini yangu inaruhusu kuwa na wanawake wa ndoa zaidi ya mmoja, isitoshe huyu mwanamke namuambia kuwa nimeoa ila adai yeye yuko tayari hata wakiwa wawili lakini mimi kwa upande wangu siko tayari kuwa na wanawake zaidi ya mmoja. Naombeni ushauri nifanyaje?