muhogomtamu
JF-Expert Member
- Apr 5, 2012
- 412
- 69
Vitambulisho vipo vya aina mbili. Vya raia na wageni. Je alipewa kipi kati ya hivyo?
Hivi hawa kina NIDA, hivi vitambulisho wa Utaifa kwa nini vimechukua muda sana?
Na inaonekana ni kama hili halionekani kuwa tatizo! Kwa utafiti mdogo sana na wa kawaida, vitambulisho kama vya benki/ card za benki, hutengenezwa kwa muda mfupi sana! tena siku hizi vinakuwa tayari vimetengenezwa nawe unapewa tu siku unayojiunga na benki hiyo , hasa CRDB! hata passport au pasi za kusafiria, mbona hutengenezwa kwa haraka tu na aina ya taarifa tunazotoaga ni hizi hizi kama za vitambulisho vya Taifa, SASA TATIZO nini hasa, mimi nashindwa kabisa kuelewa, kwamba kuna nini hasa maalumu kinachohitajika ili kutengeneza kitambulisho cha Taifa? Pengine mimi sielewi mambo mengi juu ya mchakato huu, naomba kusaidiwa.