JipuKubwa
JF-Expert Member
- Jun 1, 2013
- 2,342
- 2,390
Ndugu wanabodi leo nikiwa ofisi za mamlaka ya vitambulisho Kinondoni,nimeshuhudia mgeni akipigwa picha tayari kupatiwa kitambulisho.Aliletwa na Mtanzania na wala hakukaa kwenye foleni,alipofika kwa mpiga picha aliulizwa umeajiriwa? hakujibu ndipo afisa akauliza tena kwa kizungu cha ugoko "you employed? mzungu hakujibu,afisa mwingine mnene mweupe akambonyeza mwenziye aendelee na zoezi.Mzungu akafanikiwa akasepa huku akisindikizwa na wabongo wawili.Jamani NIDA waangaliwe vizuri.