Niambieni Hii inakuaje?

Niambieni Hii inakuaje?

Sodoku

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2016
Posts
1,277
Reaction score
2,933
Kama isingekuwa Mungu. Mimi na wengine wengi tusingekuwa na uwezo wa kuishi
Hebu angalia tu jinsi mambo yalivyo. Nini kinaendelea?

Niambie inakuaje hapa Tanzania bado watu wengi wanapinga upinzani. Niambie inakuaje kwenye mshahara kodi wanakatwa walalahoi wabunge hawakatwi

Niambie inakuaje Hospitalin maskini wanalipia Wabunge hawalipii huduma. Niambie inakuaje bado kuna watu wanashangilia chama twawala. Walio Madarakani hawaonekani kujali

Maisha hayatendi haki Katika nchi hii kama Paradiso. Haya ndiyo yanayoendelea nchini
Katika watu wengi mwenye utu ni mmoja

Unaweza yaona haya kila sehemu kila mtu ahudumiwe kwa usawa na ndo maana watu wengi wanafariki
Na kuwaacha wengi wakilia

Niambie inakuaje watoto wa maskini hawapati Elimu bora kama watoto wa viongozi. Niambie inakuaje mnyonge wanafungwa gerezani na hakimu anajua hakupaswa kufungwa

Niambie inakuaje mitaani watu wana njaa wamechoka. Lakini mababiloni yanajifanya kama vile hayaoni
Inakuaje watu wanaona na hawataki kusema?


Inspiration by the song Tell Me How Come - Morgan Heritage
 
Back
Top Bottom