Ni wakati wa wanawake wa tanzania kufunga vilemba vya maarifa.

Mbelwa Germano

JF-Expert Member
May 7, 2011
789
289
Ni dhahiri jamii yoyote dhaifu ni jamii isiyo na utamaduni wa kupenda kupata taarifa kwa maana ya kupata maarifa. Uzoefu unaonyesha kwamba wanawake wengi wanapenda taarifa za udaku zaidi kuliko zinazohusu maendeleo ya kisiasa na kiuchumu. Wao kwao ni bora liende.

Kwa kuwa wanawake ni sehemu ya jamii ya watu wa Tanzania na kwa kuwa viongozi wetu wanapenda kuongoza jamii dhaifu na kukumbatia ufisadi na kwa kuwa kwa miaka mingi wanawake wamekuwa wakifungwa vilemba vya kijani na kudumazwa kifikra juu ya mustakabali wa maisha yao na kufikia hatua wa kuwadhalilisha kwamba wameolewa na CCM, imefikia wakati muhimu wa kuachana na vilemba vya kijani na kufunga vilemba vya maarifa. Huu ndio utakuwa mwanzo wa ukombozi wa kweli ndani ya Taifa letu.NAWASILISHA.
 
Back
Top Bottom