Ni sawa Mwanaume kujipaka lipbum?

A4.

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2014
Posts
670
Reaction score
109
Ndugu wanaJF,

Kuna baadhi ya vitu huwa vinatumiwa tu na wanawake, lakini pia vipo vinavyotumiwa na wanaume tu, japo vipo ambavyo twaweza kutumia pamoja.

Sitaki kuzungumzia perfume maana nahc kutakuwa na ubishi sana.

Unakuta perfume imeandikwa 'for women' lakini mwanaume kajipulizia nyingi, vitu kama simu kutegemeana na rangi twaweza kutumia wote.

Hoja yangu ni matumizi ya LIPBUM kwa wanaume.

Mimi huwa nikienda salon nikipakwa najihisi kama njiani nasemwa kwasababu sijui.

Naomba tusaidiene hapa hasa wale wanaotupaka au wanaotengeneza au wauzaji.
 
Unaongelea kujipaka au kutumia???!!!

Maana kama ni matumizi basi haina sababu ya mjadala maana kitu hutumika penye uhitaji!!!!!
Kama ni kujipaka tu hili linajadilika
 
Na huu upepo....acha kujipaka uone lips zinavokuwa kama kisigino
mi sioni shida ila zisiwe za rangi kama wanazopaka kina ommy dimpoz na wabana pua wenzie

Ndio nini hizo...lipbum
 
Siyo urembo ile ina kazi, so kama inafanya kazi ina uhitaji hasa mazingira ya upepo.
 

kwa nchi za baridi hata wanaume wanatumia hio kwa sababu midomo inakauka hadi inapasuka,usipotumia hio utapasuka midomo hadi inatoa damu. ila kwa hapa dar tuwaachie dada/mama zetu.
 
Napita tuu
Wanaume njoon mseme kama mnatumia lip bum
 
Ehee kazi ipo kwelikweli, hakuna mbana pua pande hizi atueleze kuhusu hili.
 
kwa nchi za baridi hata wanaume wanatumia hio kwa sababu midomo inakauka hadi inapasuka,usipotumia hio utapasuka midomo hadi inatoa damu. ila kwa hapa dar tuwaachie dada/mama zetu.
Mkuu hata Dar kuna watu wanahitajika kutumia sababu ngozi na especially lips tunatofautiana sana kweli hali ya hewa ni moja ya sababu lakini pia wapo watu wana scally dry lips! !!
 
mie jana tu nimeona mtangazaji wa television moja hapa tz kapaka lipstic ya pink imemkolea kweli kweli sa sijui ndo fashion
 
mie jana tu nimeona mtangazaji wa television moja hapa tz kapaka lipstic ya pink imemkolea kweli kweli sa sijui ndo fashion
Huyo mtangazaji ni wa jinsia gani mamy?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…