Ni nani mgombea bora CCM?

Ni nani mgombea bora CCM?

Joined
Oct 21, 2008
Posts
72
Reaction score
6
Wana JF,

Ni muda sasa tangu niandike thread yangu mwenyewe ila leo naomba hoja, tumeona mchakato wa kuwania nafasi ya kugombea Urais kupitia CCM na safari hii pia tumeshuhudia rekodi ya wagombea na hii bila shaka ni alama nzuri kidemokrasia ila nataka kujua, nani ndio mgombea bora?

Tumesikia "flani hafai" kwa hio nani anafaa kupeperusha bendera ya CCM? Ni yupi ana afadhali kwako?

Ni hilo tu,
Ahsanteni
 
Ni yeyote ambaye sio fisadi, ni jasiri, mwona mbali, ana historia ya kupinga ufisadi huko nyuma. Ni mtu ambaye watu wanamjua na CCM haitopata shida kumnadi kwa watu. Ni yule anayejua matatizo yetu, yanamkera na ana suluhisho la hayo matatizo kwa kutumia vitu vyetu - sio misaada na mikopo inayo tufukarisha siku baada ya siku. Ni yule atakaye dumisha umoja na amani tuliyonayo.
 
Augustino Ramadhani apeperushe bendera
Lowassa apumzishwe ili aje awe mgombea mwenza kutoka upande wa Bara km hataki basi aende ACT
 
Augustino Ramadhani apeperushe bendera
Lowassa apumzishwe ili aje awe mgombea mwenza kutoka upande wa Bara km hataki basi aende ACT

Akagombee kwenye nchi yao ya Zanzibar kwasababu wanayo nchi yao na sie tunatakiwa kuongozwa na rais wetu kutoka Tanganyika
 
Akagombee kwenye nchi yao ya Zanzibar kwasababu wanayo nchi yao na sie tunatakiwa kuongozwa na rais wetu kutoka Tanganyika
Agustino Ramadhani ni mzaliwa wa Bara
Mama yake kazikiwa Dsm
fuatilia Historia yake
 
Hakuna mgombea Bora kuna mgombea anayekubalika na wengi. Hii inatokana na historia yake.
 
Hakuna mgombea bora kaka, we jaribu kuangalia, kuna kiongozi gan wa ccm ambaye amepinga ufisad? Nchi ina kashfa kibao lakin hakuna kiongoz yeyote anayekemea zaidi ya kuungana mkono
 
Back
Top Bottom