Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Umakini na uimara wa ulinzi kwa dr Ulimboka unahitajika mahali popote alipo. Hii ni kuwakumbusha watanzania wenzangu kuwa, huwa tuna tabia ya kujisahau sana na kujiamini ki usalama tunapokuwa nje ya nchi. Inawezekana adui akatumia nguvu na uwezo wake kupeleka mashambulizi huko huko bondeni na kuleta madhara. Tusisahau kuwa, majasusi dunia nzima wanashirikiana kwa karibu kufanikisha mipango yao. Anayesimami usalama awe makini sana, hasa na wageni wanaofika kumuona wakijifanya ni watanzania waishio huko, wawe wanaume au wanawake. Inawezekana pia adui kuigiza kama daktari, wawe makini kwa mambo kama hayo pia.. Huu ni ushauri tu.