Ni mwaka wa 6 sasa tangu nioe, lakini jinsi nilivyompata huyu mke imebaki ni kichekesho kwangu

Parabora

JF-Expert Member
Jul 6, 2019
1,504
2,180
Mwaka 2012 nikiwa niko chuo mwaka wa mwisho nilirudi nchini na nilienda field mgodini Bulyanhulu, nikiwa pale Namanga feli napumzika nasubiri muda wa kivuko niondoke kwenda upande wa pili ili nianze safari ya Kakola mgodini akaja mtoto wa kike akakaa karibu nilipokuwa mimi, huyu mtoto alikuwa mzuri kweli kweli, ni aina ya watoto ambao akipita lazma mwanaume uache mambo yako umtizame yeye.

Ghafla nikapata shambulizi la moyo.. nikawa nahisi kama unadunda dunda vile yaani ile mapigo " pwapwa pwapwa ", kama vijana wengine walivo na mimi niko moto kweli kweli sipitwi na watoto wazuri hata kwa gharama yoyote ile ninayoweza kuimudu. Nikamuanza salam, story zikaendelea mara muda wa kivuko kuondoka ukawadia. Tukaingia tukaenda kukaa siti moja, sound zikaanza mtoto akaonyesha kila dalili za kunielewa.

Tulishuka kwenye kivuko tukapanda basi tukakaa siti moja tukawa kama tushazoeana siku nyingi sana yule binti wa kisukuma alikuwa nae anasoma kozi za afya na alikuwa anaenda Geita field, na tulipofika Geita yeye akashuka safari yangu ikawa ndefu sana kila mda namuwaza nikajikuta nampenda sana sana sana.

Tukaendelea kuwasiliana, na mtoto naye kumbe alinikubali sana tukaahidiana siku ya kumaliza field tukutane Mwanza, kwa vile mimi mgodi walikuwa wananilipa pesa kwenye field yangu then kula na kulala ni bure (kwa walio fanya migodi ya Africani Barrick Gold sasa Acacia watakuwa wanaelewa) nikajimake ikawadia siku ya kuondoka mgodini na yeye ratiba yangu alikuwa anaijua muda mrefu nikamkuta Mwanza na jamaa yangu ndiye aliyempokea.

Nikala tunda kwa wiki 2 tuko nae pale mwanza mjini, toto la kisukuma aliumbika aisee. Nlimpenda japo baharia nilikuwa kitombi mtu wa kuchovya chovya hapa nikaahidi naoa. tTkaagana nikarudi Dar nikiwa na ahadi naoa kabisa hadi wazazi wangu niliwapigia simu nikawaeleza na namba zake nikawapa ... HAPA NI ILE UNASIKIA NILIKUFA NIKAOZA.

Nikiwa Dar bado tukawa tunakutana pale tulipopata muda na ahadi ilikuwa ni kuoana. Nikamaliza chuo sikukaa muda mrefu nikapata kazi . Kwa jinsi nilivyokuwa kitombi, nikaona ngoja tu nioe japo naweza kupunguza uhuni. Nikamtangazia ndoa huyu mwanamke cha ajabu akagoma eti mpaka na yeye apate kazi nikambembeleza wapi siku zikaenda nikitaka tunda napewa ila ndoa hataki anataka mpaka na yeye apate kazi.

Kuna siku nikaona meseji kwenye simu yangu namba ngeni "nipigie mimi flani, simu yangu imezima chaji" nikampigia tukaongea . Sasa kila nilipokuwa namkosa kwenye simu yake, namtafta kwenye hii namba napata taarifa za kilichomsibu. Sasa nikataka kufahamu huyu ninayeongea nae ni nani.. nikaanza kumchimba akawa ananiruka akanikwepa sana tu. Kila nikienda Mwanza nikimuita shemeji njoo tufahamiane ananikwepa. Huku ninaempenda bado amegoma kumuoa akitaka mpaka awe amepata kazi.

Kuna siku nikawa niko Mwanza mjini nikampigia simu akaniambia yuko pale mjini, nikamuomba tuonane nimpe maelekezo ampelekee rafiki yake maana simpati kwenye simu akagoma nikabemebeleza sana akakubali, mtoto akaja kweli ee bwana eeeeh ule usemi " Ndege wafananao huruka pamoja ni kweli" huyu duu alikuwa ni mkali hata Beyonce mwenyewe haingii ndani. Yaani hili toto shombe shombe la kinyamwezi na kisomali ni zuri aiseee.

Kwa kweli tulikuwa na siku nzuri sana siku hiyo nilipotoka pale nikampigia demu wangu kuhusu kumuoa akajibu yale yale nikaona isiwe tabu nikaanza mazoea na rafiki yake mwisho wa siku tukawa tunakutana naye mara kwa mara nikaanza kumchombeza habari za kutaka kumuoa akanitolea nje kweli kweli na mazoea yakapungua. Mwanaume nikakaza wapi weka gia zote mwisho wa siku akaingia kingi nikaoa bila hata kula tunda kitu ambacho kwangu ni nadra kuwa na demu hata wiki kama sijala mzigo basi naachana na wewe.

Nimekuja kula tunda nimeshaweka ndani tena miezi 4 tu tangu tujuane, na walikuwa wanakaa nyumba zinazofuatana na yule mpenzi wangu wa mwanzo na hata majina yao yanafanana na mpaka naoa huyu mchumba wangu wa mwanzo hakujua kama mimi nimemuoa huyu rafki yake yaani hakujua chochote.

Mazoea nikaanza kupunguza kwa yule mpenzi wa mwanzo akawa akinipigia simu namwambia niko busy na alikuwa akionyesha kunipenda na sijui nini kilimsibu akawa hataki nimuoe kisa hana kazi, sasa baada ya kuona imefika muda ananihitaji mimi nikiwa sina uhitaji naye akapanick akaanza matusi ikafika point na mimi nikajikuta nina jazba nikamwambia ndio maana nimekuacha nimeoa rafiki yako flani. Aiseee demu aliwasha moto maana alikuwa na namba za wazazi wangu akawafuata ndugu wa mke wangu maana walikuwa wanakaa nyumba zinafuatana akawaambia mtoto wao kambebea mume wake akachafua mtaani kwao balaaa.

Sasa mwaka jana huyu demu tulipanga tukakutana naye mkoa flani hivi, alikuwa si yule wa zamani aisee amechoka yaani hakunivutia tena akawa anataka nimuoe awe mke wa pili anasema ananipenda na hawezi kuona naishi mbali na yeye wakati mimi hata dini yangu hairuhusu. Nikala mzigo kwa siku 4 halafu nikamsafirisha alivyorudi kwao akanitaarifu ana mimba yangu. Sikutaka kubisha cha ajabu nilidate naye mwezi wa pili mwezi wa nane akawa tayari ashajifungua na anadai mtoto ni wangu. Nikamruka kama simjui vile nikaja kupata habari kumbe alizalishwa mtoto kabla ya huyu anayetaka kunibambikizia now yupo kwao ni single maza wa watoto wawili.

Mimi nipo na mke wangu sasa. maisha yanaendelea.
 
sasa mwaka jana huyu demu tulipanga tukakutana nae mkoa flani hivi, alikuwa si yule wa zamani aisee amechoka yaani hakunivutia tena akawa anataka nimuoe awe mke wa pili anasema ananipenda na hawezi kuona naishi mbali na yeye wakati mimi hata dini yangu hairuhusu, nikala mzigo kwa siku4 halafu nikamsafirisha alivorudi kwao akanitaarifu ana mimba yangu sikutaka kubisha cha ajabu nilidate nae mwezi wa pili mwezi wa nane akawa tayari ashajifungua na nadai mtoto ni wangu, nikamruka kama simjui vile nikaja kupata habari kumbe alizalishwa mtoto kabla ya huyu anaetaka kunibambikizia now yupo kwao ni single maza wa watoto wawili.
Saafi.. naona unaitendea haki katiba yetu MABAHARIA
 
"In every action there is an equal and opposite reaction"

Usimalize maneno mkuu, mwanamke wa aina uliooa anaweza hata kuja kuwa mke wa rafiki yako.
mkuu kupigiwa kawaida ila nisijue tu hahaha
 
Hilo pepo lako limehamia kwangu aisee, nahitaji sana kumuoa mtoto mmoja hv ila ndo anadai et mpka apate masters yake, ila tunapendana kinoma ila ndo hvo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom