Ni miezi minne sijapata mshahara

Ni miezi minne sijapata mshahara

Joined
Jan 15, 2015
Posts
67
Reaction score
8
Ndugu wanajamvi mm ni mwalimu ajira mpya nimeripoti tarehe 3/5/2015 hapa kituoni na tangu kipindi hicho mpaka sasa sijapokea mshahara nifanyeje?

Naombeni ushauri!
 
Mwalimu Hauko Peke Yako.Kwanza Tujuze Kua Umeenda Kwa Afisa Utumishi Ama Laa.Pili Nijuze Kua Nini Tatizo Uliloambiwa Hadi Usipate Mshahara Hadi Leo.
 
mimi pia nina.tatizo kama.lako.mtoa post niliwahi kuripoti mapema kabisa tangu tarehe 5/5/2015 halmashauri ya ikungi singida lakini hadi sasa yapata miezi mi4 sjapata mshahara hata mmoja
licha ya kua nina Vigezo vyote ikiwemo vyeti vyote kuanzia sekondari,,cha kuzaliwa pamoja na cha chuo...
tumeshafatilia saana halmashauri lakini tatizo tunaambiwa kulkua na.errors katika utumaji wa taarifa zetu hazina na utumishi...

Jambo ambalo mimi binafsi siliafiki kwa sababu kwa nini tangu mwezi wa 5 wasingerekebisha hizo errors wanakuja kutuambia sasahivi ni tunaingia mwezi wa 9??alafu kwa nini baadhi wapate baadhi tukose??nadhani kilichotumika ni divide and rule...
Halmashauri inatuibia wazi wazi hapa....

#naomba mwenye uzoefu atupe ushauri tufate hatua gani maana kama kwa afsa utumishi na.mkurugenzi kote tumeshapita na.kuna.mmoja wetu alifika hadi hazina dar akakuta mshahara wake unaingia tangu mwezi wa 5 lakini halmashauri wanatupiga danadana
 
hii serikali ya mafisadi usipokomaa unapokwa haki yako mchana kweupe! hiyo kitu ilimtokea jamaa angu miezi miwili tangu alipoanza kazi hakupata mishahara yake, tulienda manispaa kuzingua kwa hoja,tulianza idara ya elimu sekondari, ofisi ya utumishi,tulipofika kitengo cha mishahara tuligoma kutoka ndani ya ofisi yao hadi saa kumi na mbili jioni ndipo afisa utumishi mkuu alipoitwa iliandikwa cheki pale pale na jamaa alichukua pesa yake kesho.

kapambane upate haki yako mwalimu acha nidhamu ya woga utakufa masikini!
 
hii serikali ya mafisadi usipokomaa unapokwa haki yako mchana kweupe! hiyo kitu ilimtokea jamaa angu miezi miwili tangu alipoanza kazi hakupata mishahara yake, tulienda manispaa kuzingua kwa hoja,tulianza idara ya elimu sekondari, ofisi ya utumishi,tulipofika kitengo cha mishahara tuligoma kutoka ndani ya ofisi yao hadi saa kumi na mbili jioni ndipo afisa utumishi mkuu alipoitwa iliandikwa cheki pale pale na jamaa alichukua pesa yake kesho.

kapambane upate haki yako mwalimu acha nidhamu ya woga utakufa masikini!

Asante kwa Ushauri wako aisee!!
 
Halafu Mkiambiwa mfanye mabadiliko mnazingua ona sasa cha moto mnakiona....
 
Singida kuna matatizo kibao!kwa uzoefu wangu ni mkoa ambao watu wanaoanza kazi hupelekwa ama wale wafanyakazi wanaopelekwa kwa adhabu!Sina hamu na mkoa huo!Nilipanda daraja cha ajabu marekebisho wakasema errors.mwaka mzima,error.Nikahamia halmashauri flani hv,mwezi uliofuata tu nikarekebishiwa mshahara!Chezea singida weye,changamka fatilia!
 
Back
Top Bottom