Ni mbolea gani inafaa katika kilimo cha mpunga?

Ni mbolea gani inafaa katika kilimo cha mpunga?

ikinyunyi

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2017
Posts
1,062
Reaction score
941
Habari wana jamii,

Kama kinavyosomeka kichwa cha habari mimi ni mdau ambae ni mgeni katika mambo ya kilimo ila nimeamua niweke nguvu zangu huko.

Nimelima mpunga ekari 5 msimu huu na ninahitaji kuweka mbolea nikiamini nitapata mazao mengi ila naomba mnisaidie yafuatayo:-
1. Mbolea za aina ngapi znahitajika kuanzia upandikizaji hadi uvunaji.

2. Aina ipi ya mbolea inahitajika katika kila hatua hapo juu.

3. Muda gani ni muafaka kwa mimi kuweka mbolea hizo na napaswa kuzingatia vitu gani vya kitaalam ili nipate mazao mengi.

Natanguliza shukrani!
 
habari bwana Ikinyunyi; Shamba lako hilo la ekari 5 linalimwa kila mwaka au jipya kabla hujatajiwa mbole maana mbole nyingi katika shamba jipya si nzuri kabisa.
 
Kinyesi cha binadam ukikikausha ni nzuri zaidi na ni organic, Huku Moro ndiyo tunafanya na mchele unakuwa na harufu
 
habari bwana Ikinyunyi; Shamba lako hilo la ekari 5 linalimwa kila mwaka au jipya kabla hujatajiwa mbole maana mbole nyingi katika shamba jipya si nzuri kabisa.
Ahsante chief, shamba sio jipya....linalimwa kila mwaka
 
Habari wana jamii,

Kama kinavyosomeka kichwa cha habari mimi ni mdau ambae ni mgeni katika mambo ya kilimo ila nimeamua niweke nguvu zangu huko.

Nimelima mpunga ekari 5 msimu huu na ninahitaji kuweka mbolea nikiamini nitapata mazao mengi ila naomba mnisaidie yafuatayo:-
1. Mbolea za aina ngapi znahitajika kuanzia upandikizaji hadi uvunaji.

2. Aina ipi ya mbolea inahitajika katika kila hatua hapo juu.

3. Muda gani ni muafaka kwa mimi kuweka mbolea hizo na napaswa kuzingatia vitu gani vya kitaalam ili nipate mazao mengi.

Natanguliza shukrani!

MAHITAJI YA MBOLEA KATIKA KILIMO CHA MPUNGA

Mbolea za kupandia mpunga

Kabla ya kuweka mbolea hakakisha kuwa majaruba yanatengenezwa ili kuhakikisha maji hayaingii na kutoka kiholela. Mbolea ya kupandia huwekwa kwa kusia katika jaruba kabla ya kuchavanga. Kuchavanga husaidia kuchanganya udongo na mbolea na pia kutengeneza eneo zuri la kupandikiza miche. Baadaye miche hupandikizwa.

Viwango vya mbolea za kupandia mpunga
Kiwango cha mbolea za kupandia kilichopendekezwa ni kilo 20 phosphate (P) kwa hektari ambayo ni sawasawa na kiasi mifuko mitatu kwa hekta ya DAP (= mfuko mmoja kwa ekari), au mifuko miwili kwa hekta ya Minjingu Phosphate (= mfuko mmoja na nusu kwa ekari) au mifuko minne na nusu kwa hekta ya Minjingu Mazao (= mifuko miwili kwa ekari).

Mbolea za kukuzia mpunga
Ni mbolea zinazotumika baada ya mimea kuota kwa lengo la kuikuza mimea ili itoe mavuno bora. Mara nyingi mbolea hizi zinatoa kirutubisho cha naitrojeni. Kiwango kinachopendekezwa ni kilo 60 naitrogeni kwa hektari, ambacho ni sawasawa na kiasi cha mifuko miwili ya UREA au Minne na Nusu Ya CAN au Mitatu ya SA. Mbolea inayotumika mara kwa mara ni Urea. Hata hivyo mbolea zingine kama SA inaweza kutumika kama kuna mahitaji ya salfa. CAN inaweza kutumika kama kuna mahitaji maalum ya nitrate na ammonium. Kwenye mpunga, mbolea ya kukuzia inawekwa wiki mbili baada ya kupandikiza miche na irudie tena baada ya wiki nne.

Jinsi ya Kuweka mbolea: Mbolea ya kukuzia hutiwa kwa kusia wiki mbili baada ya kupandikiza, na kurudia mwezi mmoja baadaye. Ni vyema kuweka mbolea za kukuzia mara mbili ya kiasi kinachopendekezwa.

Source: Kilimo cha Kisasa cha Mpunga | Mogriculture Tz
 

Mbolea za kupandia mpunga

Kabla ya kuweka mbolea hakakisha kuwa majaruba yanatengenezwa ili kuhakikisha maji hayaingii na kutoka kiholela. Mbolea ya kupandia huwekwa kwa kusia katika jaruba kabla ya kuchavanga. Kuchavanga husaidia kuchanganya udongo na mbolea na pia kutengeneza eneo zuri la kupandikiza miche. Baadaye miche hupandikizwa.

Viwango vya mbolea za kupandia mpunga
Kiwango cha mbolea za kupandia kilichopendekezwa ni kilo 20 phosphate (P) kwa hektari ambayo ni sawasawa na kiasi mifuko mitatu kwa hekta ya DAP (= mfuko mmoja kwa ekari), au mifuko miwili kwa hekta ya Minjingu Phosphate (= mfuko mmoja na nusu kwa ekari) au mifuko minne na nusu kwa hekta ya Minjingu Mazao (= mifuko miwili kwa ekari).

Mbolea za kukuzia mpunga
Ni mbolea zinazotumika baada ya mimea kuota kwa lengo la kuikuza mimea ili itoe mavuno bora. Mara nyingi mbolea hizi zinatoa kirutubisho cha naitrojeni. Kiwango kinachopendekezwa ni kilo 60 naitrogeni kwa hektari, ambacho ni sawasawa na kiasi cha mifuko miwili ya UREA au Minne na Nusu Ya CAN au Mitatu ya SA. Mbolea inayotumika mara kwa mara ni Urea. Hata hivyo mbolea zingine kama SA inaweza kutumika kama kuna mahitaji ya salfa. CAN inaweza kutumika kama kuna mahitaji maalum ya nitrate na ammonium. Kwenye mpunga, mbolea ya kukuzia inawekwa wiki mbili baada ya kupandikiza miche na irudie tena baada ya wiki nne.

Jinsi ya Kuweka mbolea: Mbolea ya kukuzia hutiwa kwa kusia wiki mbili baada ya kupandikiza, na kurudia mwezi mmoja baadaye. Ni vyema kuweka mbolea za kukuzia mara mbili ya kiasi kinachopendekezwa.

Source: Kilimo cha Kisasa cha Mpunga | Mogriculture Tz
Umenipa darasa zuri na msaada mkubwa mkuu, shukran sana
 
Habari wana jamii,

Kama kinavyosomeka kichwa cha habari mimi ni mdau ambae ni mgeni katika mambo ya kilimo ila nimeamua niweke nguvu zangu huko.

Nimelima mpunga ekari 5 msimu huu na ninahitaji kuweka mbolea nikiamini nitapata mazao mengi ila naomba mnisaidie yafuatayo:-
1. Mbolea za aina ngapi znahitajika kuanzia upandikizaji hadi uvunaji.

2. Aina ipi ya mbolea inahitajika katika kila hatua hapo juu.

3. Muda gani ni muafaka kwa mimi kuweka mbolea hizo na napaswa kuzingatia vitu gani vya kitaalam ili nipate mazao mengi.

Natanguliza shukrani!

Kuna jamaa nilikuwa naongea naye yeye ana mashamba Igunga anasema kinyesi cha Popo ni mbolea nzuri sana kwa kupandia.......tatizo ni upatikanaji wake.
 
Back
Top Bottom