Ni mambo gani mazuri ya Kikwete tunayoweza kumshauri Magufuli kuyafuata na kuyaendeleza?

mpk

JF-Expert Member
Sep 26, 2012
3,115
3,864
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kwa miaka 26 madarakani alifanya mambo mengi mazuri na mengine ya kijinga na akaendelea kusema "Shida ninayoiona wanaacha mazuri na kuendeleza ya kijinga" Nadhani ni kauli ya mtu aliyejaa busara na ni msingi kwa viongozi waliofuata kama Mungu akiwajalia busara.

Kama watanzania bila kujali itikadi zetu tunajua Kikwete kuna vitu alifanya vizuri na kuna alivyofanya vibaya. Ni mazuri yapi tunamshauri Magufuli ayaendeleze? Nimeamua kuleta uzi huu baada ya rais wetu kusema jana anapata muda kupitia maoni yetu mitandaoni.

Mnajua msimamo na itikadi yangu lakini thread hii ni kwa faida ya taifa letu pendwa la Tanzania. Ningeomba tumshauri rais kufuata na kuendeleza mambo mazuri ya JK bila kufuata misimamo yetu kisiasa. KARIBU!
 
Mwl Nyerere aliwahi kusema kwa miaka 26 madarakani alifanya mambo mengi mazuri na mengine ya kijinga na akaendelea kusema "Shida ninayoiona wanaacha mazuri na kuendeleza ya kijinga" Nadhani ni kauli ya mtu aliyejaa busara na ni msingi kwa viongozi waliofuata kama Mungu akiwajalia busara.

Kama watanzania bila kujali itikadi zetu tunajua Kikwete kuna vitu alifanya vizuri na kuna alivyofanya vibaya. Ni mazuri yapi tunamshauri Magufuli ayaendeleze? Nimeamua kuleta uzi huu baada ya rais wetu kusema jana anapata muda kupitia maoni yetu mitandaoni.

Mnajua msimamo na itikadi yangu lakini thread hii ni kwa faida ya taifa letu pendwa la Tanzania. Ningeomba tumshauri rais kufuata na kuendeleza mambo mazuri ya JK bila kufuata misimamo yetu kisiasa. KARIBU!

Aruhusu vyama vya siasa kuandamana kila siku huku vikihamasisha vijana kutofanya kazi.
Arushus majambazi wajitawale
Asifukuze wavivu an amajzii kama wale wa TRA na TPA badala yake awe anapiga bit tu huku hachukui hatua
Awe anaongea maneno mazuri kwa wananchi huku akiwa hatekelezi alichoahidi.
Afukuze mawaiziri wote majembe ili abakize wale wakawaida ili sis upinzani tupate cha kusema na wafanya biashara wakubwa tupitishe mizigo bila kodi. Hivyo amuondoe prof Muhongo, Prof Mbawala,Prof Ndlaichako, Mh Lukuvi etc
 
Pachoto, nakubaliana nawe juu ya uhuru wa habari na kujieleza na kukosolewa! Ila hapo kwenye udini mmm
 
aache kubania ajira mpya. atuajiri tu maana metunyoosha vya kutosha kabisa. Mkuu Magu tafafhali tutazame na sie tuliosomeshwa kwa mbinde kwa pesa za kuuza mihogo na kunde. leo hii hadi tuliowaacha vyuo wanatukuta mtaani tunapigwa jua tu. Mkuu wetu tafadhali zingatia hili.
 
Ajue kuvaa na mwonekano wa Kipresidenti anayependa vijana. Suti zimkae, mara moja moja apige jeans. Abadilishe mawani. Ajiamini kuwa ni Rais. Asilipize visasi. Asijione au kuwa na hisia za Kingship. Akague gwaride hata mara moja tumuone. Ajichanganye hata gengeni ajionee maisha. Asiwe na mtu mmoja tu wa kumsikiliza, Bulembo.
 
Jamani muacheni kikwete afanye mambo yake,si mlisema ni dhaifu? Mnataka kumuambukiza Magufi udhaifu wa kikwete?
Mtamkumbuka sana professor Jk
Nimejitahidi kueleza lengo la uzi huu naona hukunielewa! Rudia kusoma utaekewa labda
 
Aruhusu vyama vya siasa kuandamana kila siku huku vikihamasisha vijana kutofanya kazi.
Arushus majambazi wajitawale
Asifukuze wavivu an amajzii kama wale wa TRA na TPA badala yake awe anapiga bit tu huku hachukui hatua
Awe anaongea maneno mazuri kwa wananchi huku akiwa hatekelezi alichoahidi.
Afukuze mawaiziri wote majembe ili abakize wale wakawaida ili sis upinzani tupate cha kusema na wafanya biashara wakubwa tupitishe mizigo bila kodi. Hivyo amuondoe prof Muhongo, Prof Mbawala,Prof Ndlaichako, Mh Lukuvi etc
Hayo yote aliyafanya Kikwete? Let's be serious!
 
Mi nina mengi ya kumshauri lakini nianze na mawili. Awe mwanasiasa lakini asionyeshe kuchukia upinzani kiasi hicho. Kikwete aliwateua Jusa Mbatia kuwa wabunge lakini leo tunaambiwa anafukuzwa mtu kwa ukurugenzi kwa sababu ya itikadi yake

Aanzishe upya mchakato wa katiba uliokwama na kwa vile watu wameanza kuwa na wasi wasi naye kupendelea watu wa chama chake basi aache mchakato uwe huru
 
Mwl Nyerere aliwahi kusema kwa miaka 26 madarakani alifanya mambo mengi mazuri na mengine ya kijinga na akaendelea kusema "Shida ninayoiona wanaacha mazuri na kuendeleza ya kijinga" Nadhani ni kauli ya mtu aliyejaa busara na ni msingi kwa viongozi waliofuata kama Mungu akiwajalia busara.

Kama watanzania bila kujali itikadi zetu tunajua Kikwete kuna vitu alifanya vizuri na kuna alivyofanya vibaya. Ni mazuri yapi tunamshauri Magufuli ayaendeleze? Nimeamua kuleta uzi huu baada ya rais wetu kusema jana anapata muda kupitia maoni yetu mitandaoni.

Mnajua msimamo na itikadi yangu lakini thread hii ni kwa faida ya taifa letu pendwa la Tanzania. Ningeomba tumshauri rais kufuata na kuendeleza mambo mazuri ya JK bila kufuata misimamo yetu kisiasa. KARIBU!


Magufuli si mjinga kihivyo na ndiyo maana anapangua mambo yote katika utawala wa Kikwete kwani hayastahili kuigwa. Kikwete will go down as the most useless president Tanzania has ever had. Jiulize wewe mwenyewe: kipi kizuri alikifanya Kikwete katika utawala wake? Au hata kina Mkapa na Mwinyi, walifanya nini cha maana zaidi ya kuididimiza hii nchi? Nawaunga mkono wasomi wote wanaoshauri katiba ipitiwe upya ili viongozi walioboronga wafunguliwe mashitaka na kuhukumiwa kama nchi za wenzetu walioendelea ili iwe fundisho kwa viongozi wengine wakaokuja.
 
Leo Magufuli yupo Bize Nchi nzima kutengeneza Madawati kwa kuwa Jakaya alishatengeneza Madarasa ya kukaa hayo Madawati.
Magu leo anasisitiza kutumia EFD Machine kwa kuwa hiyo system tayari kaikuta ka introduce Jakaya.
Tumuacheni Jakaya Kikwete maana ana majikumu mazito kimataifa leo Msumbiji wanamtaka akawasuluhishe Frelimo na Renamo, jana nimetazama moja ya Documentary ya Aljazeera nimestuka kuona Jk ni miongoni mwa wanaotajwa kumrithi Ban ki moon nikamtania Rafiki yangu anieleze siri ya kung'aa nyota ya huyu Mzee akaniambia siri ya mafanikio yake ni Maombi mabaya ya Gwajima.
Ukitaka Maombi Mazuri ya Gwajima yatakukuta kama ya Lowassa na ukitaka akuombee maombi mabaya yanakukuta kama ya Kikwete chaguo ni lako
 
Magufuli si mjinga kihivyo na ndiyo maana anapangua mambo yote katika utawala wa Kikwete kwani hayastahili kuigwa. Kikwete will go down as the most useless president Tanzania has ever had. Jiulize wewe mwenyewe: kipi kizuri alikifanya Kikwete katika utawala wake? Au hata kina Mkapa na Mwinyi, walifanya nini cha maana zaidi ya kuididimiza hii nchi? Nawaunga mkono wasomi wote wanaoshauri katiba ipitiwe upya ili viongozi walioboronga wafunguliwe mashitaka na kuhukumiwa kama nchi za wenzetu walioendelea ili iwe fundisho kwa viongozi wengine wakaokuja.
Unaruhusiwa kuamini kuwa Jk hajafanya kitu ila unapaswa kujua hata kama hupendi kuwa Madawati yote anayohamasisha Magufuli kutengenezwa hayawekwi chini ya Miti yanapelekwa kwny Madarasa ambayo kakuta yameshajengwa.

Chuki zinakufanya uamini anaekunulia kiti cha kuweka chumbani kwako kafanya kazi kubwa kuliko yule aliyojenga chumba cha kuweka kiti hicho!

Unamsifia Magu kupangua yote ya Jk yakiwemo

1) Upatikanaji wa Sukari
2) kusitishwa Ajira Serikalini
3) Bunge live
4) Uhuru wa kukosoa Serikali
5) kukatwa Mishahara Madaktari wa Referal hospital
6) Madakatari Wanafunzi kufutiwa Posho
7) ......
 
Back
Top Bottom