Ni kweli sisi ni "CCM B"

Ni kweli sisi ni "CCM B"

youngsharo

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2015
Posts
2,491
Reaction score
500
Baada ya baadhi ya wana CCM kukihama chama, kumeanza kuzuka kauli ambazo naweza kuziita ni "kauli za mfa maji" wakidai kuwa Chadema sasa ni CCM B.

Nini maana ya upinzani? ni hali ya kupinga jambo fulani linalofanywa na mtu/watu fulani.
Naomba nieleweke hapa;kabla ya upinzani watanzania wote tulikuwa chama kimoja "CCM", ambae hajawahi kuwa mwana CCM labda aliyezaliwa miaka ya 90 na kuendelea, hivyo hata mimi nathubutu kusema "MIMI NI CCM B, NILIYEJIPA JINA LA CHADEMA".

Hao akina Slaa, Lipumba walianzia wapi siasa? je ni nani ambaye sio CCM?
Kabla ya kuundwa NCCR Mageuzi wafuasi wake walikuwa chama gani?
Kabla ya kuundwa CUF wafuasi wake walikuwa chama gani?

Kabla ya kuundwa CHADEMA wafuasi wake walikuwa chama gani? au ni wapi "source" ya wafuasi wa vyama vya upinzani? Maana nyingine ni kuwa sisi ni CCM B tunaopingana na CCM A kwa mambo wanayofanya.

Hivyo napenda kuwapa ukweli wanaCCM wote kuwa; Hatutishwi na kauli zenu kuwa CHADEMA imekuwa CCM B.

Nawasilisha youngsharo.
 
mtu akihama ana acha chama chake haondoki na chama, na chama cio mtu kma chama ni mtu bac tuseme ccm imekufa coz wa anzilishi wake washa kufa...
viva ukawa
 
mtu akihama ana acha chama chake haondoki na chama, na chama cio mtu kma chama ni mtu bac tuseme ccm imekufa coz wa anzilishi wake washa kufa...
viva ukawa

yes, pale kaja lowassa haijaja ccm, kaja sumaye haijaja ccm, ila walikuwa wanaccm kama sisi tulivyokuwa wanaccm miaka ya 9o.
 
ACT ni chadema B pia? Maana walojitoa CDM ndio wameunda ACT. So kujitoa chama kimoja kwenda kingine ni kwa kutofautiana hoja na mitazamo.
Hata Dini ni hivyo hivyo mtu akihama dini moja kwenda dini nyingine ahami na dini yake ya mwanzo atokako bali hufuata utaratibu wa dini aliyohamia.
 
ACT ni chadema B pia? Maana walojitoa CDM ndio wameunda ACT. So kujitoa chama kimoja kwenda kingine ni kwa kutofautiana hoja na mitazamo.
Hata Dini ni hivyo hivyo mtu akihama dini moja kwenda dini nyingine ahami na dini yake ya mwanzo atokako bali hufuata utaratibu wa dini aliyohamia.

Mkuu mi nawashangaa sana wanapong'ang'ania Lowassa au Sumaye ni CCM B.
 
[h=3]
12079268_1033153493371586_8970307654917834309_n.jpg
12072748_1033153550038247_2873476544750732661_n.jpg
[/h]
 
Chadema siyo wapinzani tena, ieleweke hivyo, ACT wazalendo ndiyo chama cha upinzani!
 
Chadema siyo wapinzani tena, ieleweke hivyo, ACT wazalendo ndiyo chama cha upinzani!

Aah Kweli najisahau sana ndugu yangu, Chadema siyo wapinzani tena ni chama tawala.
CCM na ACT ndo wapinzani
 
Mbona kila siku mnamsakama Zito, kumbe na nyie mmo

Tuko wapi? sisi tumejitenga, ila Zitto tunamuona mnafiki kwanini anaiunga mkono Ccm? je kulikuwa na haja gani kuanzisha ACT si angehamia moja kwa moja CCM?
 
Chadema siyo wapinzani tena, ieleweke hivyo, ACT wazalendo ndiyo chama cha upinzani!
Upo sawa Kabisa mheshimiwa, CHADEMA haiwezi kuwa chama tawala kisha hapo hapo iwe upinzani! CHADEMA SIYO WAPINZANI, lakini uhalisia huo ni kuanzia tarehe 25!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom