Ni Daktari gani aliyemshauri Hayati Magufuli kugombea Urais?

Kwa sababu ya sacrifice ya maisha yake, Watanzania wamekuwa masikini zaidi katika Kipindi cha uongozi wake na wataendelea kuwa masikini katika uongozi unaoanza leo. Uongozi unaoanza leo ni wa Awamu ileile ya Tano inayoishia mwaka 2025 lakini bahati mbaya, Kikatiba unaruhusiwa kugombea kuongoza Awamu ya Sita ya miaka 10. Rais mpya akisaidiwa na Makamu na Baraza la Mawaziri lililopo, kwa sababu nyingi tu, atalazimika kuendeleza misingi mibovu iliyowekwa na sacrifice ya mtangulizi wake. Makamu wa Rais anategemewa kuteuliwa na Chama kinachosimamia utekelezaji wa Ilani yake kupitia sacrifice ndo maana tulikuwa na Serikali ya Magufuli, Tanzania Mpya ya Magufuli, CCM Mpya ya Magufuli na Wapiga Kura wake. Binadamu yeyote ana manufaa kwake na Jamii akiwa hai!
Asipokuwa imara na akawa na misimamo tofauti tutanyongeka SANA,

Kiukweli naomba awe na washauri wazuri wenye nia dhabiti dhidi ya watanzania wa kawaida siyo watu wa mijini tu!
Arudishe mzunguko kwenye biashara za kawaida, aachane na sera kandamizi za kukamua ng'ombe wasio na malisho.

Aangalie HESLB! TRA! Ajira e.t.c
Aelewe shida zetu! Biashara kati ya watanzania, na majirani zetu!
Aondoe uchafu uliojaa barabarani kwa jina la umachinga!
Vibanda viondolewe biashara zifanyike maeneo halali!

Everyday is Saturday................................:cool:
 
Ndo maana Hayati alisema " Amejitolea maisha yake" kama sikosei one of his speech.
Au mlikua hamtaki ajitolee maisha yake Yani hamjamuomba au sio wadau.
 
Anajiandaa kuapishwa kuongoza malaika huko mbere kwa mbere.... Sijui akifa na huko ataenda kuongoza wapi???...
 
Ivi kwanini hakua akisafiri kwa ndege umbali mrefu???
Ukipata majibu ya swali hili utakua umejibu kwamba walikua wanajua au hawajui.....

NOTE.... Yote haya yalikua na hesabu zake shikamoo kinachoitwa KITENGO.
Mazingira ya ndani ya ndege za safari ndefu ni very artificial kwa hiyo hayafai kwa msafiri yeyote mwenye tatizo la kifua kwa sababu ndege zinapita kwenye ukanda wenye hewa pungufu. Mazingira artificial, moyo artificial haviendani!
 
Marehemu alikuwa hashauriki, alisema ukimshauri ndo unaharibu kabisaaaa...marehemu alisema yeye ni jiwe kweri kweri

Hivi ni system gani ya kiusalama iliyopo nchini ambayo ilikubali kumuingiza madarakani mtu mwenye matatizo ya moyo?
Nafikiri kwamba huenda system ya ki-usalama ya kwetu haikuweka kipaombele kwenye kipengere kinachohusu ubora wa afya ya mtu kwenye nafasi husika. Yawezekana pia taasisi husika na mifumo yake hadi sasa bado haina utaratibu wa kuwaandaa watu kwa ajili ya kushika nyadhifa nyeti hasa zile za kitaifa. Kuna taifa moja duniani lina utaratibu wa kuwaandaa wananchi wake toka wakiwa shule za awali hadi elimu ya juu kwa ajili ya kushika nyadhifa nyeti za taifa. Inapotokea mtu aliyeko madarakani kwa namna yeyote ile ameshindwa kutimiza majukumu yake au kufa,katika nchi ile huwa haipati wakati mgumu kumpata mtu sahihi au mwenye uwezo zaidi wa kurithi nafasi husika.
 
Mazingira ya ndani ya ndege za safari ndefu ni very artificial kwa hiyo hayafai kwa msafiri yeyote mwenye tatizo la kifua kwa sababu ndege zinapita kwenye ukanda wenye hewa pungufu. Mazingira artificial, moyo artificial haviendani!
Jibu zuri kwa wanahoji kwamba kitengo hawakua wanajua
 
Covid-19 ndiyo imeli bust hilo tatizo hadi kupelekea mauti !! washauri wake hawakutimiza wajibu wao ipasavyo!! Mtoa hoja una hoja ya msingi inayohitaji majibu ya kina.
 
Kwa hali yake hakupaswa kufanya kazi nzito za stress, ilitakiwa atulie tu.
Mnatakaga maisha mareeefu Ili iwe nini Wakati kila kitu ambacho Mungu kakupa kufanya umekifanya

Mungu alimpa nafasi hiyo si Kwa Tanzania pekee Bali ni Kwa ajili yake Mungu, na muda ulipowadia kamchukua Kwa ajili yake, sasa hayo mengine ni yenu mliobaki hapa

Ukiangalia Kwa jicho la mbali, JPM hakuwa Raisi pekee Bali pia alikuwa ni Mleta ujumbe wa maisha ya kila mtu kutoka Kwa aliyeamua awe Rais wetu kwamba, kufa tutakufa Tu, eidher Kwa malalia, magonjwa ya moyo, Corona au ajali pengine kupitia magumu saaana, Ila tusimwache Mungu basi kazi yake nyingine ilikuwa ni hiyo, sasa, shauli yako kuchagua ama kupuuza, yeye Kesha maliza kazi, nasi Je, ni nini tutajivunia kwamba Kwa Yale tuliyofanya, jamii inafurahia uwepo wetu, au Sisi kazi yetu ni kuwaponda waliodhubutu kufanya mambo japo kidogo Kwa ajili ya wengi?

Labda Anza Kwanza wewe kujiuliza, umefanya nini kikubwa ambacho jamii itakukumbuka pindi ukifa na kumbukumbu lako kutoweka hapa duniani?
 
Hata mabingwa wa moyo walivyomwambia Mzee inabidi tukupeke India kwa wataalamu zaidi alikataa
 
Kwa wenzetu daktari wake anges1
Mnatakaga maisha mareeefu Ili iwe nini Wakati kila kitu ambacho Mungu kakupa kufanya umekifanya

Mungu alimpa nafasi hiyo si Kwa Tanzania pekee Bali ni Kwa ajili yake Mungu, na muda ulipowadia kamchukua Kwa ajili yake, sasa hayo mengine ni yenu mliobaki hapa

Ukiangalia Kwa jicho la mbali, JPM hakuwa Raisi pekee Bali pia alikuwa ni Mleta ujumbe wa maisha ya kila mtu kutoka Kwa aliyeamua awe Rais wetu kwamba, kufa tutakufa Tu, eidher Kwa malalia, magonjwa ya moyo, Corona au ajali pengine kupitia magumu saaana, Ila tusimwache Mungu basi kazi yake nyingine ilikuwa ni hiyo, sasa, shauli yako kuchagua ama kupuuza, yeye Kesha maliza kazi, nasi Je, ni nini tutajivunia kwamba Kwa Yale tuliyofanya, jamii inafurahia uwepo wetu, au Sisi kazi yetu ni kuwaponda waliodhubutu kufanya mambo japo kidogo Kwa ajili ya wengi?

Labda Anza Kwanza wewe kujiuliza, umefanya nini kikubwa ambacho jamii itakukumbuka pindi ukifa na kumbukumbu lako kutoweka hapa duniani?
Nimezaa
 
Hata mabingwa wa moyo walivyomwambia Mzee inabidi tukupeke India kwa wataalamu zaidi alikataa
Alijua kilichotakiwa kitokee Kwa Wakati huo, kwani Hata wangelimpeleka huko kisingelisaidia Kwa kuwa Madactari wa huko na kokote Dunia hakuna wa kurudisha uhai!!!

Mbona ni wengi tu ambao huumwa moyo na kutibiwa hapa hupona?

Nyakati za umauti ukifika, kila mtu hufahamu, Mpendwa wetu alifahamu Hilo na ndiyo maana hakuona shida sjui apelekwe wapi!

Alipatikana Kwa miujiza, kafanya kazi nyingi kimiujiza na ameondoka kimiujiza, ni kama masikhala vile!!

Kumbe mwenzetu Yuko kwenye Ufalme mwingine kabisa ule wa milele
 
Covid-19 ndiyo imeli bust hilo tatizo hadi kupelekea mauti !! washauri wake hawakutimiza wajibu wao ipasavyo!! Mtoa hoja una hoja ya msingi inayohitaji majibu ya kina.
Alipoingia tu madarakani alitamka wazi kabisa kuwa hashauriki kwa hiyo inawezekana washauri wake walikuwa wanamshauri na kupuuzwa au waliogopa kumshauri ili wasitumbuliwe. Mgonjwa wa kwanza wa Covid-19 alipogundulika nchini Serikali yake iliuchukulia ugonjwa huu very seriously na kuagiza watu wafuate ushauri wa WHO wa kujikinga. Ulikuwa huingii Ofisi yoyote ya Serikali bila Barakoa na nje ya jengo kulikuwa na mfanyakazi wa kuhakikisha wageni wenye Barakoa wananawa kwa sabuni mikono yao ndo waingie. Mara Rais alibadilika na kuita ugonjwa ni Mafua madogo na kutuma Ndege Madagascar kuleta Dawa na upimaji ukasitishwa na kuanza kukejeli ushauri wa WHO na kutaka wananchi wajifukize na kutumia madawa mengine ya kienyeji. Kosa kubwa kabisa Serikali ikatangazia ulimwengu kuwa Tanzania hakuna Covid-19 kwa hiyo nchini njia zote za kujikinga pamoja na Barakoa zikatupiliwa mbali lakini watu waliendelea kufa ikiwa ni pamoja na vigogo. Wakati viongozi wa Nchi kubwa na ndogo duniani wakivaa Barakoa Rais wetu mpendwa na waliomzunguka kikazi hawakuwahi kuvaa licha ya maambukizi kuzidi nafikiri kujaribu kuonyesha uwezo wa Tiba zake mpaka zikahamia Hospitalini. PhD na Mitishamba matokeo ndo hayo!
 
Kwanza Kabisa Nitoe Pole Kwa Watanzania Wote na Wapenda Maendeleo wote kwa Kuondokewa na Rais Wetu Mpendwa John Joseph Magufuli. Kwa Tamaduni za Kitanzania Si Vizuri kumuongelea Marehemu kwa Mabaya aliyoyafanya. Na Ni wasisitize watanzania Wenzangu Kuzingatia Utamaduni Wetu.

Ni Rudi kwenye Mada, Imesemwa Sababu Iliyopelekea Kifo cha Mpendwa Wetu Kuwa ni Matatizo ya Moyo aliyokuwa Nayo Toka Zamani, Japo niweke Wazi Kuwa Sina Imani na Hii sababu Ya Kifo Cha Mpendwa Wetu, huenda Imetumika Kwasababu ni tatizo alilokuwa nalo muda Mrefu. Imani yangu Inanituma Kuwa Kuna Sababu/Ugonjwa Mwingine ambao huenda ndio umesababisha kifo cha Mpendwa Wetu Japo kuthibitisha Hilo Itakuwa ni Ngumu sanaa. Nimefikiria hivyo kwasababu viongozi wote 2 tuliokuwa Tumewapoteza kwa Mwezi wa Pili walifariki kwa Shida Moja Ya Tatizo la Upumuaji, ambao kiutendaji walikuwa ni watu wa karibu wa Mpendwa Wetu ambao tuseme mara zote walikuwa wakionana mbele ya Camera Au nyuma Ya Camera.

Na Tatizo hili la Upumuaji Kwa Mtu mwenye matatizo ya Moyo huwa ni ngumu sana “KUCHOMOKA”. Kama Tuliweza kuambiwa kuwa haumwi wakati anaumwa si ajabu hata sababu iliyopelekea Umauti kumkuta isiwe sahihi. Ukweli Wa haya Yote wanao “WAO” pia Niongeze Kama Watanzania Wengi tulikuwa Tunafahamu kuwa Mpendwa Wetu anakifaa kwenye moyo wake ambacho kinamsaidia moyo wake Kufanya kazi naona hakukuwa na Ugumu wa Sisi Kuambiwa Kuwa Mpendwa Wetu anaumwa. Kitendo cha Kuficha basi ni ishara tosha Kuwa Huenda kuna kingine ambacho Kilikuwa kikimsumbua Mpendwa Wetu. Nakumbuka Maneno Ya Mama Yetu mpendwa kuwa kwa Mwanadamu ni kawaida mwili wake kwenda kukaguliwa na kupata “VIMAFUA KIDOGO” na hakukuwa na kauli ya kuonesha kuwa “MOYO” ndio Shida.

Nije kwenye Swali La Msingi. Nimekaa nakujiuliza kuwa NI DAKTARI GANI AMBAYE ALIMSHAURI MPENDWA WETU KUGOMBEA URAIS huku akijua Fika kuwa Mpendwa Wetu anakifaa kwenye Moyo wake kinachomsaidia kufanya kazi kutokana na Shida ya HCM aliyokuwa Nayo mpendwa wetu. Nimeona Kipande cha Gazeti kikitembea kwenye mitandao ya kijamii ambacho kikionesha Kua mpendwa Wetu alikuwa Na Tatizo ya Moyo kwa Muda mrefu kitaalamu lilojulikana kama HYPERTROPHIC CARDIOMYOPATHY (HCM), kitaalamu tatizo hili huathiri Misuri ya Moyo ambayo husaidia moyo kusukuma damu na Moja Ya matibabu yake ni Kuweka kifaa kitakacho saidia Misuri ya Moyo kufanya kazi kwa Niaba.

Lakini Watalaamu Wa Afya watanisaida kuwa mtu mwenye Tatizo hili la HCM huwa kwenye HIGH RISK kama Sio wote Huishia kupata tatizo jingine lijulikanao kama ATRIAL FIBRILLATION na Huweza kuwa ACUTE au CHRONIC. Kuepuka Athari hizi ambazo zinaweza kupelekea mtu kupata Stroke, Embolism, Heart Failure au Muda mwingine japo sio sana ni Cardiac Arrest. Wagonjwa Watatizo hili kitalaamu huwa Wanafundishwa namna Ya Kuishi na Tatizo hili kwa Kupewa DO’S and DONT’S ili kuepuka madhara hayo niliyoyataja Hapo Juu. Moja Ya vitu ambavyo hushauiriwa kuepuka ni pamoja na STRESS, Kukasirika Mara Kwa Mara, kushtukashtuka pamoja na Vitu vingine kwani hivyo vyote husababisha Mapigo ya Moyo kwenda Kasi na Kufanya moyo ufanye kazi Mara 2/3 ya Kawaida yake, Sasa kwa Mtu ambaye ana HCM huwa Na Athari zaidi.

Kwa Mtu mwenye Tatizo hili mara nyingi huwa na MADAKTARI WAO ambao Huwasiliana Mara kwa Mara na kufanya Consultation Ya Mambo Mbalimbali kuhusu afya yake ikiwa ni pamoja na kumpa ushauri wa kitalaamu, kufuatilia maendeleo ya mgonjwa wake na Vingine. Kwa Kutambua UGUMU, UKUBWA na UZITO wa Nafasi ya Urais Naamini Fika Kabisa kabla ya Mpendwa wetu kuamua kwenda kuchukua Form ya Kugombea Uraisi alifanya Consultation Na Daktari wake kuona kama Anaweza kuendelea Na Majukumu hayo au hawezi kuendelea nayo ikiwa Atafanikiwa. Na kama Hakufanya Hivyo basi alikosea na Kama Alifanya Najiuliza JE DAKTARI ALIE MRUHUSU MPENDWA WETU KUGOMBEA NAFASI HIYO alikuwa Anamtakia Nini Mpendwa Wetu? Hakujua Kama Haya Yatatokea? Hata kama Isingekuwa Ya Moyo basi STROKE ingetokea. Je, ni Mpendwa Wetu Alidharau ushauri wa Kitalaamu?, Je Ni Mpendwa Wetu hakushauliwa na Watalaamu Wa Afya? Au ni nini kilitokea.

Kwa Tatizo ambalo Mpendwa Wetu amekuwa nalo kwa muda Mrefu ni kiri kwa Kusema kuwa Mungu ni Mkuu amemsaidia sana Kuishi miaka Mingi ndania Ya NAFASI ya URAIS kwasababu ni kazi ya STRESS ambayo kwatatizo hilo kuchukua Miaka 6-7 ndani ya Nafasi Hiyo ni NEEMA za Mungu Tuu hakuna Uchawi wala Uwezo Binafsi. Matatizo Mengi ya Moyo huwa hayakai sehemu moja Na STRESS ni Lazima Stress zitadominate na Mwisho wake huwa Hivi.

Ni Vyema tukaheshimu Ushauri wa Wataalamu Wa Afya ili Tuishi miaka mingi zaidi, Na Ni vyema Watalaamu wa Afya wakatushauri vuzir bila woga bali kwa kufuata Taaluma zao ili Sisi Wananchi wa Kawaida tuweze kuishi maisha Marefu.

Bwana Alitoa na Bwana Ametwaa Jina La Bwana Lihimidiwe.

Amen
Yeye mwenyewe alitaka kwa sababu Afya yake akijua mapema kabisa
 
Kwa sababu ya sacrifice ya maisha yake, Watanzania wamekuwa masikini zaidi katika Kipindi cha uongozi wake na wataendelea kuwa masikini katika uongozi unaoanza leo. Uongozi unaoanza leo ni wa Awamu ileile ya Tano inayoishia mwaka 2025 lakini bahati mbaya, Kikatiba unaruhusiwa kugombea kuongoza Awamu ya Sita ya miaka 10. Rais mpya akisaidiwa na Makamu na Baraza la Mawaziri lililopo, kwa sababu nyingi tu, atalazimika kuendeleza misingi mibovu iliyowekwa na sacrifice ya mtangulizi wake. Makamu wa Rais anategemewa kuteuliwa na Chama kinachosimamia utekelezaji wa Ilani yake kupitia sacrifice ndo maana tulikuwa na Serikali ya Magufuli, Tanzania Mpya ya Magufuli, CCM Mpya ya Magufuli na Wapiga Kura wake. Binadamu yeyote ana manufaa kwake na Jamii akiwa hai!
Wewe na ndugu zako ndo mmebaki maskini

Sent from my Infinix X5515 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom