wiseboy.
JF-Expert Member
- Aug 11, 2014
- 2,931
- 4,549
Ukweli unauma na ndo tabia yake,wengi wetu tunauchukia ukweli kwa kuwa tu unauma,ni aibu sana kuzaliwa ktk taifa ambalo lina kila kitu lakini bado limeshindwa kusimama kiuchumi,ni aibu sana kuwa raia wa taifa ambalo gavana wa benk kuu anafariki ughaibuni halafu eti anazikwa huko kisa serikali haina hela ya kumsafirisha,ni aibu sana kuwa raia wa taifa ambalo gavana wake wa benk kuu anadai kuwa sh imeporomoka kwa kuwa wahisani hawajatoa misaada,tangu lini uchumi ukakua kwa kuomba omba badala ya kuwa na vitega uchumi?
Ni aibu sana kuwa raia wa taifa ambalo rais wake hajui kwanini nchi ni maskini,ni aibu sana kuwa raia wa taifa ambalo dhahabu zinaenda nje na kuwaacha wananchi ktk ufukara mzito,maeneo yote ya migodi wananchi wanaishi ktk nyumba za tope,nyasi na hakuna zahanati wala shule bora,ni aibu kuwa ktk taifa ambalo bunge linapoteza muda kutunga sheria ya kuminya uhuru wa kupashana habari na kuacha mambo ya msingi kwa taifa kama kulinda raslimali,ni aibu sana tena sana kuwa mtanzania,acheni ukweli usemwe.
Ni aibu sana kuwa raia wa taifa ambalo rais wake hajui kwanini nchi ni maskini,ni aibu sana kuwa raia wa taifa ambalo dhahabu zinaenda nje na kuwaacha wananchi ktk ufukara mzito,maeneo yote ya migodi wananchi wanaishi ktk nyumba za tope,nyasi na hakuna zahanati wala shule bora,ni aibu kuwa ktk taifa ambalo bunge linapoteza muda kutunga sheria ya kuminya uhuru wa kupashana habari na kuacha mambo ya msingi kwa taifa kama kulinda raslimali,ni aibu sana tena sana kuwa mtanzania,acheni ukweli usemwe.