NHIF Maoni na Kero wanazokumbana nazo wanachama wao

Mwana Ilala

JF-Expert Member
Jan 29, 2013
1,287
483
Kwa nn tunalazimishwa kununua Baadhi ya dawa tunapoenda kutibiwa sisi wanachama wa Bima
Afya!?

Hili ni tatizo sugu sana linalo wakabili Wanachama wa Mfuko wa NHIF. Unaenda hosp. Dr. ana-recommend utumie dawa Fulani, ukienda huko pharmacy za ndani ya hosp, unaambiwa dawa hizi Unatakiwa kulipia Cash, huku wakiendelea kusisitizia kuwa hata Hazina Bei. Sasa kama Hazina Bei!!? Kwa nn ulazimishwe kulipia/nunua dawa za Elfu 15 huku consultation ya Dr. Ikigarim hadi Elfu Arobaini!?
Hapo Bado hujafanya vipimo Kibao. Halafu Mwisho wa siku unaambiwa hizi dawa hata Hazina Bei, ni Elfu saba tu. Ila zinapatikana kwa Cash. It doesn't make Sense.

Ukiomba ile form ambayo inakuruhusu uende nayo kwenye maduka yao wanakuambia pia form hawana au zimewaishia.

Hiii ni kero Kubwa sana. Ambayo inatupata sisi wanachama wao.
 
Back
Top Bottom