Mlitika
JF-Expert Member
- Mar 23, 2012
- 457
- 260
Nilikuwa napita tu nakatiza mtaa mmoja hivi, mara paaa! nikamwona huyu mtoto live. Gazabu ilinishika ingawa simfahamu nikakata fimbo nimcharaze maana nilihisi hako katabia kanahitaji tukio chungu la kumkumbusha asithubutu kufikilia kufanya hivyo tena. Nakata fimbo nikakumbuka kumbe viboka vilishakatazwa shuleni na majumbani. Nikabaki nimeduwaa tu. Swali ninalojiuliza mpaka sasa ni hili: "Mtoto wa namna hii kweli utatumia njia gani kuiumba hiyo akili yake ikue na kukomaa katika uzani wa kimaadili?" Ebu nisaidieni kabla sijachukua maamuzi ya ajabu.