Nguvu za kiume ni nini hasa?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Tafadhali nisionekane mshamba...naomba nijulishwe.Hivi,nguvu za kiume ni nini hasa? Je,ni uwezo wa uume kutenda kazi bila kuchoka kwa muda mrefu? Je,ni uwezo wa uume kutema mara nyingi? Ni nini hasa?
 
Nguvu za kiume ni uwezo wa uume kusimama ktk majambozi,hakuna m/me kamili mwenye uwezo wa kufanya mmajamboz bila kuchoka! Usidanganyike na porno movie wale kina mandingo usikute lile bao moja wameunganisha clip za siku nzima au hata mbili.
 
Tafadhali nisionekane mshamba...naomba nijulishwe.Hivi,nguvu za kiume ni nini hasa? Je,ni uwezo wa uume kutenda kazi bila kuchoka kwa muda mrefu? Je,ni uwezo wa uume kutema mara nyingi? Ni nini hasa?

njoo ntakuonesha inakuaje!! regardless of your gender!
 
Nguvu za kiume ni uwezo wa uume kusimama ktk majambozi,hakuna m/me kamili mwenye uwezo wa kufanya mmajamboz bila kuchoka! Usidanganyike na porno movie wale kina mandingo usikute lile bao moja wameunganisha clip za siku nzima au hata mbili.

...nahisi kwa mtazamo wa wengi wanadhani 'akishacheua' tayari zile ndio mbegu!
:puke::mimba:.....

.......
 
Ni uwezo wa uume kusimama muda mrefu huku ukitenda kazi yake ki sawa sawa, mtu mwenye nguvu za kiume huchukua muda mrefu kiasi kabla hajapiga bao, na pia huwa na uwezo wa kurudia round ya pili hadi nne muda mfupi baada ya kumaliza bao.

Mtu mwenye upungufu wa nguvu za kiume, uume wake hausimami haraka hadi achezewe muda mrefu.

Tatizo lingine ni lile la kupiga bao haraka. kiingereza wanaita pre mature ejaculation. Yaani mtu akipiga nje ndani mara 2 tayari.
 
​
Njia za kulimaliza tatizo la upungufu wa nguvu za kiume

TATIZO la nguvu za kiume linaonekana kukua kwa kasi huku wengi wakiwa hawajui nini la kufanya. Kati ya wale ambao wanasumbuliwa na tatizo hilo ni vijana, hali inayofanya baadhi yao kubaki katika kitendawili wakijiuliza nini hasa kinasababisha wanakuwa katika hali hiyo.

Kuna kesi nyingi za wanaume kukimbiwa, sababu mojawapo ni baadhi yao kutokuwa na uwezo ambao mwanaume anapaswa kuwa nao, yaani kuwa imara. Wapo ambao kwa sababu ya tatizo hili, wamejikuta wanalazimika hata kujiua au kuchukua hatua yoyote mbaya.Lakini ukweli ni kuwa msingi wa maisha yenye mafanikio si kujiua wala si kujilaumu kwa kusumbuliwa na tatizo fulani, bali kuchukua hatua ili ulishinde tatizo hilo.

Tangu umezaliwa hadi leo umesumbuliwa na matatizo mangapi? Bila shaka ni mengi, na suluhu ya matatizo si kujiua, kujipa adhabu kwa kutokula ama kujilaumu kwa kuzaliwa, bila shaka hayo hayana msaada.

KWANINI KASI YA WANAUME KUWA NA TATIZO HILI INAONGEZEKA?
Ziko sababu nyingi, lakini zilizo kuu ni hali ya maisha, kwa maana ya mabadiliko makubwa ya matumizi ya vyakula, kwa mfano zamani wengi walikuwa wakitumia vitu vya asili, sasa wengi wanatumia vyakula vya kiwandani ambavyo kwa bahati mbaya baadhi yake havina ubora.Badala ya kutumia juisi za kutengeneza kwa kutumia maembe kutoka mashambani, wengi wananunua juisi za viwandani ambazo baadhi yake ni mchanganyiko wa rangi usio na faida yoyote katika mwili.

Tatizo hili pia linatokana na ulaji usiofaa na usiofuata misingi ya afya bora; wengi wanakula ili tumbo limejaa, si wengi ambao wanaangalia kwanza chakula kabla ya kula. Ukweli ni kwamba kila chakula kina msaada wake, vingine vinasaidia mafuta, vingine nguvu, chuma na kadhalika.Lakini pia tafiti nyingi zinaonyesha kuwa wengi wanaolalamikia kupungukiwa nguvu za kiume, hawajui hasa sababu na nini wafanye. Lakini ukweli ni kuwa baadhi yao wana tatizo hili kwa sababu wenzi wao si wenye kuwasaidia, si wajuzi.

Ndio kusema kama mwanaume anasumbuliwa na tatizo la nguvu za kiume, ni vizuri kuangalia limeanza lini, na kwanini. Wakati fulani wanawake kwa kauli zao zisizo za ushirikiano na matendo yao, yaweza kuwa ni sababu mojawapo ya kusababisha wanaume kutokuwa na nguvu katika tendo.Maana utakuta wanawake wengine wanawaambia waume zao “haya unataka, njoo basi nataka kuwahi au hutaki niondoke”…kauli kama hii haitii raha. Pia wengine hawana ushirikiano, yuko tu kama hayuko.

Raha ya ndoa haiko hivi, ni lazima mshirikiane vizuri, si ndio jamani? Raha ya ndoa ujuzi.Kwa bahati mbaya baada ya ndoa, si wengi ambao wanaendelea na ubunifu, tena kuna wengine ukiwaambia leo twende na ubunifu wa aina hii utasikia “eeeh weee unataka kunivunja kiuno mwenzako, haya mambo ya vijana haya”. Je, hali ya ndoa yako ikoje?


Mapenzi yanahitaji usafi, lakini wapi bwana kuna mwingine ukiwa naye unaomba Mungu akuachie haraka….ananuka, hakuna maandalizi, anakuvamia bora hata kuku atacheza huku atacheza kule.
Kwa bahati mbaya zaidi kuna wengine wakiambiwa ukweli utasikia wanasema kwa nyodo, aaah bwana eeeh wafuate hao wanaojua!Ndugu yangu raha ya ndoa mpate muda wa kucheza, kuzungumza mazuri na kuonyeshana upendo wa dhati, ikiwa ni pamoja na kutimiza mazuri mliyoahidiana wakati mnaingia kwenye ndoa.

Sio wanaume wengi wenye sababu za kibaiolojia zinazowafanya wakose nguvu za kiume, isipokuwa wengi wao huwa na matatizo ya kisaikolojia zaidi ambayo wahusika wanaweza kujiponya nayo bila hata kutumia dawa za miti shamba.

Kuna sababu kadhaa za wanaume kuwa na tatizo la nguvu za kiume kama vile matatizo ya kisaikolojia, kuwahi kujichua, baadhi ya matatizo ya magonjwa ya moyo, kisukari, shinikizo la damu, magonjwa ya zinaa, unene wa kupita kiasi, umri mkubwa, ulevi, kuacha mazoezi na ulaji usiofaa.

Kimsingi ziko tiba za mchanganyiko wa vyakula, lakini pia ili kuondoa tatizo wakati unaendelea na tiba kama ambavyo nimewahi kuzitaja katika matoleo kadhaa yaliyopita, unapaswa kufanya mazoezi na kula vyakula, vinywaji vyenye nguvu ili kujipa nguvu zaidi.

Pia kama mwanaume ameishi na mwanawake kwa muda mrefu na amekuwa na desturi ya kufanya mepenzi mara kwa mara katika mazingira yale yale anaweza kukumbwa na kasoro hiyo.

Dawa za Nguvu za Kiume Kwa Anaye Taka! bonyeza hapa https://www.jamiiforums.com/jf-doctor/196934-dawa-za-nguvu-za-kiume-kwa-anaye-taka-2.html
 
Back
Top Bottom