Nguvu ya Lowassa ni zaidi ya kuingia ikulu

Nguvu ya Lowassa ni zaidi ya kuingia ikulu

sangwine

Senior Member
Joined
Jun 16, 2013
Posts
144
Reaction score
45
Kwa wote wanaofuatilia mchakato mzima wa uchaguzi kwa umakini watakuwashaelewa nini namaanisha. Tukianza na uchukuaji na urudishwaji wa fomu za uraisi, CCM walianza kwa umauti mkubwa na kusema Mh J Magufuri kaweka rekodi lakini siku ya kuchukua fomu Mh Lowassa habari za Mh Pombe Magufuri zilizima kabisa na habari ya mjini , kwenye mitandao na magazeti ilikuwa ni Lowassa tu.

Siku ya kusaka wadhamini Mh Magufuri alikuwa kashaanza saulika kwa Mh Lowasa alikuwa Hot kiasi kwamba kama CCM hawana mgombe vile, na ndo neno Mafuriko likaanza tumika kuanzia Mbeya, Arusha, na Mwanza.

Siku ya kuanza Kampeni Mh Magufuri alianza kwa mbwembwe za kuweka rekodi ya kujaza watu wengi jangwani lakini Umati huo kiukweli ulivuta watu kwa ujio wa wasanii wakubwa Tanzania kwa Diamond , Ali kiba , Ya moto band kwa kuwa kulikuwa na shoo kali kwa kiingilio cha miguu yako. Na umati ule CCM waliuita ni Mafuriko.

Lakini ujio wa Mh Lowassa nao katika Uwanja huohuo wa jangwani mambo yalibadilika na kuwa gharika au Tsunami.

Mh magufuri ameshapita katika Mikoa mitano ambayo ni Rukwa , katavi , Mbeya , njombe na Ruvuma lakini habari zake zishasaulika baada ya Lowasa kupita mikoa miwili. Nipo Njombe kwasasa na jumamosi Mh Magufuri alikuwa hapa Ujio wa Lowassa umefuta kumbukumbu za ujio wa Magufuri Ndani Njombe pia upepo umezidi kuwa mbaya hata kwa mgombea wa CCM Bw Mwalongo aka Kapi la Makinda.

Hadi wakati huu bado sijaona wapi kuna ngome ya Magufuri na CCM kiujumla kwani kila sehemu ni Lowassa, Mh Kikwete nae kasha soma alama za nyakati na kumtelekeza Mh Magufuri anae zunguka kama mkiwa. Pole sana CCM , Malofa wanazidi pendwa na ulofa wao.
 
Huko dar wanakwambia siku ya uchaguzi ni 'kuua'

Hakika Lowassa ni tishio.
 
Kiukweli tuseme ukweli hata kama sheria ya mitandao inaanza leo niko tayali kulitolea maelezo hili kuwa Lowasa anapendwa tena sana sasa sijajua ni kwann kwakweli CCM tunakazi ya kupambana na Supper power
 
yule mgonjwa wenu hatishi kwa lolote mtazika tu.

Afya njema ni majaliwa ya Mwenyezi Mungu. Sio haki wala busara kubeza afya ya mtu mwingine. Hatima ya mtu yeyote yule ukiwemo wewe mwenyewe iko mikononi mwa Mungu, na sio matakwa yako wewe.
 
yule mgonjwa wenu hatishi kwa lolote mtazika tu.

kwani wewe hutazikwa? Angalia fimbo ya Mungu isikurudi maana unaongea kwa jeuri kama vile uhai wako umeushikilia mwenyewe!
 
Hivi sheria ya mitandao imeanza kweli? Naona watu wanatukana bila kuchukuliwa hatua zozote ati.
 
Kwa wote wanaofuatilia mchakato mzima wa uchaguzi kwa umakini watakuwashaelewa nini namaanisha. Tukianza na uchukuaji na urudishwaji wa fomu za uraisi, CCM walianza kwa umauti mkubwa na kusema Mh J Magufuri kaweka rekodi lakini siku ya kuchukua fomu Mh Lowassa habari za Mh Pombe Magufuri zilizima kabisa na habari ya mjini , kwenye mitandao na magazeti ilikuwa ni Lowassa tu.

Siku ya kusaka wadhamini Mh Magufuri alikuwa kashaanza saulika kwa Mh Lowasa alikuwa Hot kiasi kwamba kama CCM hawana mgombe vile, na ndo neno Mafuriko likaanza tumika kuanzia Mbeya, Arusha, na Mwanza.

Siku ya kuanza Kampeni Mh Magufuri alianza kwa mbwembwe za kuweka rekodi ya kujaza watu wengi jangwani lakini Umati huo kiukweli ulivuta watu kwa ujio wa wasanii wakubwa Tanzania kwa Diamond , Ali kiba , Ya moto band kwa kuwa kulikuwa na shoo kali kwa kiingilio cha miguu yako. Na umati ule CCM waliuita ni Mafuriko.

Lakini ujio wa Mh Lowassa nao katika Uwanja huohuo wa jangwani mambo yalibadilika na kuwa gharika au Tsunami.

Mhmagufuri ameshapita katika Mikoa mitano ambayo ni Rukwa , katavi , Mbeya , njombe na Ruvuma lakini habari zake zishasaulika baada ya Lowasa kupita mikoa miwili. Nipo Njombe kwasasa na jumamosi Mh Magufuri alikuwa hapa Ujio wa Lowassa umefuta kumbukumbu za ujio wa Magufuri Ndani Njombe pia upepo umezidi kuwa mbaya hata kwa mgombea wa CCM Bw Mwalongo aka Kapi la Makinda.

Hadi wakati huu bado sijaona wapi kuna ngome ya Magufuri na CCM kiujumla kwani kila sehemu ni Lowassa, Mh Kikwete nae kasha soma alama za nyakati na kumtelekeza Mh Magufuri anae zunguka kama mkiwa. Pole sana CCM , Malofa wanazidi pendwa na ulofa wao.

Anaitwa Magufuli na siyo Magufuri!

Ni Sahaulika na siyo Saulika!

Duh! Wewe kweli unahitaji mabadiliko siyo siri kama hata haujui ni wapi pa kuweka herufi kubwa na wapi ndogo, tofauti ya ,,a" na ,,ha" au ,,l" na ,,r" ningekushauri ulifanyie kazi hilo kwanza, kajifunze kuandika vizuri kwanza, halafu ndiyo uingie kwenye mambo mengine kama siasa kwa maana unaonekana kituko tu!"
 
Back
Top Bottom