Ng’ombe 1 = 900K kwa Mwezi!

kila biashara inalipa. Ni kweli?
Lakini sio kila biashara inalipa. Ni kweli?

Hoja:
ufugaji inategemea unaufanyia wapi? Unaufanyaje? Unauzia wapi? Unauzia akina nani?

Ebu nambie: mtu yupo kijijini unakuta lita ya maziwa elf 1 utalinganisha na yule wa lita ya maziwa elf 3?

Sio mtu unakuja na expectations ya kuingiza laki 9 kwa mwezi kizembe hivyo. Huo unakuwa ni uongo.

Bado ufugaji wa kisasa ni gharama sana hasa hao ng'ombe wanahitaji uangalizi mkubwa. Madawa n.k
 
Unachokisema ni kweli kabisa na ndio maana wataalamu tupo kuwasaidia
 
Kwa hiyo mafunzo yanalipa sana kuliko kufuga?

Kwa nini usifuge mwenyewe ili upate hizo 900k

Hii ni sawa na kumtoza mtu pesa ili umfundishe kubeti, kama unaamini beti Mwenyewe ili upate mihela mimgi


Motivation speaker in town
NDUGUU, UKISIKIA UNAITIWA FURSA, KUMBUKA WE MWENYEWE NDO FURSA..
YAANI HAPO NG'OMBE WA MAZIWA NI WEWE MWENYEWE UNAYEITWA
 
Unachokisema ni kweli kabisa na ndio maana wataalamu tupo kuwasaidia
Huo sio msaada mkuu.
Hapa unachokiangalia wewe ni kuuza bidhaa yako. Na kuvutia mteja kwa kumwambia laki 9 inaingia kizembe hivyo.

Ninyi ni moja ya watu mnao changia watu kupata hasara. Sasabu unatumia Sales pitch words katika biashara zenu bila kujali matokeo ya upande wa pili.

Sorry.: nimeongea kwa mtazamo wa wale motivation speaker
 
Uko sahii ila sisi sio motivation speakers ni wataalamu na wafugaji wa muda. Unaweza kufahamu zaidi kuhusu sisi. Youtube @RubabaTv Blog. Tanzania na Kilimo
 
HUJATUAMBIA PIA GHARAMA ZA MALISHO, CHANJO, nk ili tujue faida ya huyo ngombe
 
HUJATUAMBIA PIA GHARAMA ZA MALISHO, CHANJO, House boy, nk ili tujue faida ya huyo ngombe
Tumeshachambua hilo kwa kina katika post zetu za nyuma.
Pia katika group letu huko tunatoa mafunzo ya kina
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…