John Malanilo
Member
- Dec 2, 2013
- 50
- 13
Makamanda, Nipende kuwapongeza wananchi wa wilaya ya Ngara maana wameonesha ukomavu wa kisiasa. Mwezi uliopita baada ya mkutano wa Mwenyekiti wa Taifa na makamanda wengine wa anga, tulifanya mikutano 14 kwenye ngazi ya vitongoji ambako chadema tulipata mwitiko mzuri sana. katika mikutano hiyo iliyofanyika maeneo mbalimbali kama Muchingili, Ntobeye Centre, Chivu, Kigina, Nyarutiti, Mrugalagala, Kumukaritusi, Kalemela, Chenda, na maeneo mengine, wananchi walifurahia elimu ya uraia inayotolewa na Chadema ikiwa ni pamoja na kukomesha kero mbalimbali.
- Tumetetea wananchi katika kesi mbalimbalikama ile ya mama mmoja aliyefiwa na mtoto wake na kudaiwa kulipa laki mbili iliaruhusiwe na viongozi wa CCM kuzikakatika kata ya Rusumo. Kesi hiyo tumeitetea CHADEMA na wamefungwa jela mwakammoja mmoja na wakitoka jela wataezeka nyumba hiyo.
- Tumeweza kuteteawananchi katika kata ya Nyakisasa ambakowakata mbao waliingilia misitu ya asili katika maeneo ya vyanzo vya maji.CHADEMA imeingilia kati na uharibifu huo umesitishwa na wananchi na uongozi wawilaya umeendelea kufuatilia na kuchukua hatua zaidi.
- Tumefungua kesi dhidi ya mtu aliyeng'oa bendera ya chama katika kata ya Mganza mpaka leoameshikiliwa na kesi inaendelea. Mpaka sasa mtuhumiwa amekiomba chama kimwoneehuruma kwa sababu chama kilichomshawishi kung'oa bendera hakimsaidii naamefahamu kuwa alifanya kosa.
- Kata ya Bukiriro, wananchi waliokuwawanachelewa kufika sokoni, walikuwa wanatozwa faini ya sh. 300 bila kupewastakabadhi na pesa hizo hazikufahamika zinaenda wapi. Jambo hilo CHADEMA tumelikomeshana wananchi sasa wana uhuru wa kuingia sokoni wakati wowote bila bughudha ya faini.
- Tumetetea wanawake wa kata ya Mrusagamba waliokuwawanatakiwa kwendaa klinik na jembe ili wamlilie nesi katika zahanati yaMagamba. Pamoja na kuwa viongozi wa CCM kama mwenyekiti wa kijiji na mtendajiwa kijiji wapo hawakitetea mpaka Chadema ilipozuia wanawake kupeleka majembe. Nanesi alipokuja juu, Chadema tukamtuliza. Mpaka leo ni marufuku kwenda na jembe klinik.
Attachments
-
Msafara ukimsubili Mh Mbowe Kumnazi.JPG33.1 KB · Views: 1,005 -
Ngara 25.2.14.JPG35.8 KB · Views: 963 -
Ngara.JPG31.6 KB · Views: 932 -
Wananchi wa Ngara wakifuatilia Mh Mbowe.JPG38.5 KB · Views: 953 -
Wazee hawakubaki nyuma.JPG44.9 KB · Views: 922 -
Kamanda Malanilo Akihutubia wananchi Kumnazi.JPG29.7 KB · Views: 910 -
Makamanda waliolinda Kajugujugu Ngara.JPG44.1 KB · Views: 899 -
Na watoto wajue CDM Vema.JPG41.2 KB · Views: 900